I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Saturday 3 December 2016

TUNASHANGAA YAMEOTAJE, NA TUMEYAPANDA WENYEWE

Kila  mtu amejeruhiwa/kuathiriwa na janga la UKIMWI kwa namna fulani.

Habari. Bila shaka unafahamu tarehe 1 Desemba ya kila  mwaka ni siku ya UKIMWI duniani. kabla sijaanza kuzungumzia lengo langu hasa kukihusu kichwa cha mada yangu, basi pitia takwimu hizi hapa chini juu ya hali ya UKIMWI Tanzania Bara zilizotolewa Dec 1 2016 na TACAIDS kupitia viongozi mbalimbali na vyombo vya habari:

Takwimu
Maelezo
5.3%
 Maambukizi ya UKIMWI kwa Tanzania bara. Sawa na watanzania 5 kati ya kila watanzania 100
6.2%
 Wastani wa wanawake walioathirika na maambuziki ya UKIMWI.  Sawa na wanawake 6 kati ya kila wanawake 100
3.8%
Wastani wa wanaume walioathirika na maambuziki ya UKIMWI. Sawa na wanaume 4 kati ya kila wanaume 100
10.6%
Vijana kati ya umri wa miaka 15-24 wanamambukizi ya UKIMWI, sawa na vijana 11 kati ya kila vijana 100

Ikumbukwe takwimu hizi ni kwa wale ambao wamepimwa iwe ni upimaji wa hiari wa kawaida, kabla ya kufunga ndoa, wakati wa uchangiaji damu au wakati wa ujauzito. Utakubaliana na mimi kuwa kuna kundi kubwa sana la waathirika hasa maeneo ya vijijini ambako watu wanapata maambukizi ya ukimwi lakini hawana elimu juu ya utambuzi wa afya na wengine huishia kudhani wamelogwa na kujikuta wanafakamia miti shamba au kwenda kwa waganga wa kienyeji kupiga lamri nakadharika. Kwa lugha rahisi mimi naamini hali ya maambukizi ni  mbaya zaidi ya inavyodhaniwa kwa takwimu.

NANI MCHAWI?
Sio mimi ni wewe. Hapana ni wewe sio mimi

Sisi wenyewe na serikali yetu. Ndio ni sisi wenyewe tunajiloga na kuitmbukiza jamii yetu katika shimo la huzuni na giza totoro inayoumiza na kuangamiza kizazi hiki na kijacho. Kundi kubwa la watu wanapigia debe maisha ya kufanya ngono kama ni utaratibu wa kawaida wa maisha ya watu hasa vijana. Watu wenye ushawishi mkubwa wamefumba mdomo kuongea ukweli na hali halisi ya mambo kwenye visababishi vya kuenea kwa UKIMWI, na badala yake wamejikita zaidi kutoa matamko ya kulalamika matokeo yake na kuomba, kutafuta na kutumia fedha nyingi kushughulikia matokeo ya UKIMWI.

Kwa macho yangu nimeshuhudia shirika fulani linatembelea mashuleni na makundi ya vijana wa kucheza ngoma za burudani, mashindano ya kucheza na kimba kisha kutoa zawadi za mabox ya kondom kwa vijana hao. Kama hiyo haitoshi, pembeni waliweka banda na kuwaalika vijana wa kike kwa wakiume waende ili wakafundishwe namna ya kufanya ngono kwa kondom, tena taasisi ya kielimu. Na nilishuhudia vijana wasio na mpango mkakati wa maisha yao wakimiminika kwenda huko, halafu bila aibu tunashangaa kwanini maambukizi yanapanda?. Kisingizio cha kondomu kimetumika sana kukoleza moto wa ngono kwa vijana, na asilimia kubwa ya vijana wamenasa kwa mtego huo na bado wakayabeba maambukizi. Kondom hazijafika leo, zipo kabla ya UKIMWI na bado maambukizi yanazidi kupanda,  bado hatufungui macho na kuelewa kuw tunawekeza kwenye mradi usiozalisha. 
Muda wa kunyoosheana vidole haupo. Tumia akili yako kuweka malengo ya kujitoa kwenye ngono. Mungu atakuepusha tu. Ni kweli na hakika. Jionee huruma wewe ,kizazi chako na cha wengine.

Kupitia takwimu hizo hapo juu unaona vijana ambao tunawaita 'sexually active group' ndio vinara wa maambukizi. Maambukizi hayo yanachochewa na wao wenyewe pia mabinti kufanya ngono na watu wazima ambao wanamaambukizi ya UKIMWI na hutumia fedha zao kama ulimbo wa kuwanasa wasichana wadogo.

KWANINI WANAWAKE WANAONGOZA KWA MAAMBUKIZI ?

Katika vitu vya kuchekesha na kuudhi ni uchambuzi wa watu tena wasomi juu ya swali hili, 'kwanini wanawake wanaongoza kwa maambukizi ya UKIMWI'. Nasema inachekesha kwakuwa hakuna hata mmoja niliyemsikia akigusia chimbuko na mzizi wa tatizo hili,bali wote waling'ang'ana kwenye matokeo, isipokuwa baadhi ya viongozi wa dini walisema ukweli. Nilikuwa nawafuatilia kwa karibu sana. Wengi walitumia kigezo cha unyanyasaji wa kijinsia, ubakaji, umasikini nakadharika, vitu ambavyo vinachangia kwa kiai kidogo sana.

 Inachekesha zaidi kwakuwa sikusikia hata mmoja akihoji kwanini kwenye nyimbo na miziki wanaume wanavaa suti na kupendeza  lakini wasichana wanavaa nguo za ndani pekee na visidiria  na kuachia maungo yao nje? Hakuna aliyesema kwanini wanawake wa sasa hawaoni thamani tena ya miili yao na kutembea uchi barabarani huko na kuamsha hashiki za wanaume pia kutoa mafunzo ya udadisi waa ngono kwa watoto wadogo? Nyie mnojiita watetezi wa haki za ujinsia hasa haki za mwanamke na unyanyasaji, hapa huwa mnavaa miwani ya tinted sio? Ukweli ni kwamba tabia ya wasichana na wanawake kujianika miili yao na kuona wao ni bidhaa inayohitajika sana kwa wanaume (highly demanded commodity) kumefanya wanaume wengi kuwa na mahusiano na wanawake zaidi ya mmoja. Ni wanawake wachache sana wenye mahusiano na wanaume zaidi ya mmoja, lakini wanaume wengi wamejilundikia wanawake kwakuwa wanawake wenyewe (sio wote) waamekuwa mawakala kamili wa kusajili wanaume kwa mavazi yao na kushindwa kusema HAPANA kwa ngono. Hivyo mwanaume mmoja anayeishi na maambukizi ya UKIMWI ni rahisi kusambaza kwa wanawake wengi zaidi kuliko uwezekano wa mwanamke mmoja anayeishi na maambukizi kusambaza kwa wanaume wengi zaidi. Hii inatokana na sababu za kimaumbile pia, ukichanaganya na maelezo yangu hapo juu basi unapata HADITHI NJOO ,UTAMU KOLEA.
Wanawake ni waleta uhai mpya. Ni wasaidizi kamili wa Mungu kuleta watu duniani huku. Tabia ya kujitoa ufahamu na kujidharirisha kunafanya hata watoto walio matumboni kuanza kulia kwa hofu kwakuwa wamebebwa na wazazi maharamia wasiojali utu na kujisitiri kwa heshima. BADILIKA LEO

Kwa mtindo huu, suala la UKIMWI litabaki kuwa miradi ya watu ya kujitengenezea fedha, na kufurahia maambukizi kupanda kwakuwa bila UKIMWI na wao watakosa kazi. Ni bora tukaongozwa kwa busara binafsi, na kujifunga mkanda, yani KUSEMA HAPANA KWA TABIA YA NGONO NA TABIA AMBATANISHI. Nikisema haya kwa mtu ambaye anjiona amekubuhu kwenye tabia hii, huenda anashangaa na kuona naandika nadharia, lakini huu ni ukweli ambao huenda ukawa ni mgumu kuumeza lakini hamna namna, utabaki kuwa ukweli. Kwani ukisema HAPANA KWA NGONO unatoka vidonda sehemu fulani ya mwili? Mwanamke ukiamua kusema hapana, mwanaume hana jipya. Hisia za wanaume huwa zinapanda haraka, na ukisema hapana na kuondoka, huwa zinashuka haraka pia na ufahamu kurejea kama ilivyo sufuria iliyotolewa kwenye jiko la moto. Wakati wanawake hisia zao hupanda taratibu (hasa pale unapompa nafasi mwanaume ya kujieleza na kujiweka karibu na wewe), kisha mkifika juu, huwa zinabaki juu hukohuko kwa muda mrefu kama chungu kilichotolewa kwenye jiko la moto. Ndipo hapo utasikia mara wanaume baba yao mmoja, oh, nataka mtoto  tu, lakini sitaki kuolewa,, sitakuja kumwamini mwanaume yoyote, kwa maana wote ni waongo, oh,,,,,, ah,,,,, nakadharika. Kuongezeka kwa watoto wa je ya ndoa au wasio na mlezi ya moja kwa moja kutoka kwa baba zao, kunatoa picha halisi ya hili jambo. Wazazi wengi au hawataki au hawawezi kuzungumza ukweli na mabinti zao, na wakijitahidi sana wanaishia tu kusema UWE MAKINI, AU TUMIA AKILI. Maneno ambayo hayaakisi kabisa kuwa mzazi unataka binti yako au kijana wa kiume aepukane na janga hili la UKIMWI.

Ukweli ni kwamba mimi ni mmoja kati ya watu ambao hawashangai kabisaaaaaaaaaaaaaa juu ya idadi ya wanawake wenye maambukizi ya UKIMWI kuwa kubwa kuliko wanaume, kwasababu wao ndio huchochea hurka ya wanaume kuwapapalikia. Kwa sentensi hiyo sijasema wanaume hatuna makosa, hapana, nasi pia tunatakiwa kupambana na udhaifu wa miili yetu, kujifunza kuuthibiti mwili kwa maana ni ukweli wa mchana kuwa changamoto ni nyingi, kichwa kinavurugika unapoona miili ya wanawake waziwazi, lakini jikubali, badili mazingira, mshirikishe Mungu, sema HAPANA PIA KWA VISHAWISHI, usitumie pesa zako ili kukoleza mapambano na mikikimikiki ya ngono. Kama umeoa basi ridhika na mke wako kwa maana ndiye Mungu aliyekupangia. Kma hujaoa basi timiza malengo yako na baadaye fanya uchaguzi sahihi.

Sitaki kusema imani za dini zinasemaje juu ya hili, lakini nijuavyo mimi HAKUNA DINI HATA MOJA INAYOSHABIKA NGON KABLA NA NJE YA NDOA. KUSUBILI INAWEZEKANA, SEMA HAPANA KWA NGONO ILI KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI NA KUEPUSHA MATUMIZI YA FEDHA NYINGI AMBAZO ZIMEKUWA ZIKIELEKEA HUKO. Kumbuka kwa Tanzania kuanzai DEC 1, 2016 serikali imezindua Bodi ya udhamini wa mfuko wa UKIMWI ambako mabilioni ya fedha yanakusanywa kutoka vyanzo vya ndani ili kushughulikia mambo ya UKIMWI na kupunguza utegemezi kwa wahisani wa nje ambao vigezo vyao hubadilika mara kwa mara..
Nikutakie tafakari njema na tufanye maamuzi ya busara ili kuzikomboa familia zetu. Mungu akubariki.

Eng Nguki wa Malekela
0763 639 101/ 0679 639 101
ngukiherman@ymail.com
UCE Tanzania-Volunteer
03 Dec 2016
Thank you for visiting my blog. Click home/ view the web version to see other topics on list ( in case you don't), which have been categorized by months posted. Eg to see the topics posted last month, just click November.  The same for October. You are welcome. Also for Professional information about Agriculture, water resources, soil and environmental conservation visit www.wadcotanzania.blogspot.com  Eng Nguki  

Ili ufanye vizuri unahitaji juhudi, ili ufanye vizuri  zaidi unamuhitaji Mungu.Hauwezi kufeli darasani kwasababu unatoa sehemu ya muda wako kufanya kazi za Mungu. Usikate tamaa., angalia unakosea wapi na urekebishe. Huenda ukapitia Chamgamoto kidogo na ukaanza kumlaumu Mungu au mtu fulani, hapana, utapita tu, kaza mwendo. 25 Nov 2016-SUA