I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Friday 5 January 2018

Heh! Kumbe Wavaa Hirizi Bado Wapo?

Kwa dunia ya sasa kubadili fikira zetu ni lazima sio ombi!
Habari. Namshukuru Mungu pamoja nawe kwa kutuwezesha kufika mwaka mpya wa 2018, hakika ni neema ya upendeleo kabisa kutoka kwa Mungu wetu. Na sio jambo la kulichukulia kawaida hata kidogo, bali litutafakarishe na kutufanya tuishi  vyema kwa busara na mipango akinifu.
Sasa tuje kwenye mada yetu ya kufungulia mwaka!. Kwa kipindi kirefu nimekuwa nikisikia tu neno hirizi na kwamba kuna watu wanavaa kama kinga kwa imani za kishirikina, wakiamini kuwa zinawakinga au kuwalinda dhidi ya  maadui wanaotaka kuwadhuru. Nilipoendelea kudodosa, nikasikia hizo hirizi watumiaji huwa wanavaa kwa kificho maeneo ambayo sio rahisi kuonekana kama viunoni nakadhalika.

Kwa bahati mbaya huwa sijichoshi sana kufuatilia kama nikiona jambo halina tija au haliwezi kuniathiri kwa namna yoyote (labda iwe ni kwaajili ya kuwatahadharisha wengine au kujifunza). Sasa juzijuzi hapa nikiwa ugenini mkoa fulani, kunarafiki yangu  mmoja tulikuwa tunafanya naye kazi akawa ananisimulia juu ya mdada mmoja ambaye ametokea kumpenda, na mdada mwenyewe kaanza kuonesha ukaribu japo bado hajamwambia. Kwakweli alinisimulia jinsi huyo mdada alivyo mzuri na ambavyo akimsogelea tu network inakata na anasahau kila kitu na kumuwaza yule mdada; hahahaaa

Akaniambia niende mtaa anakokaa (rafiki yangu) ili nimuone huyo mdada kwa maana akitoka kazini huwa wanapiga stori na ni nyumba jirani, nikamkubalia. Basi nikaenda kama tulivyokubaliana, na nilimkuta yule mdada hapo. Ki ukweli hana tatizo, ni mzuri wa sura na ni haki yake yule jamaa kuchanganyikiwa. Yule dada alivaa gauni la mikono ya kukatwa (nakosa jina zuri, lakini naamini umenielewa), wakati namuangalia vizuri nikaona kwenye mkono wake wa kushoto katikati ya kiwiko na bega amejifunga kamba nyeusi kama rangi ya kaniki zile za zamani na inakitu fulani kimefungwa. Mhhhhh,

Nikamuliza mtu fulani alikuwa karibu kuwa kile ni nini alichojifunga yule mdada? Akajibu ‘HIRIZI’, ati nini??? Mbona nilisikia wavaaji huwa wanaficha? Imekuwaje huyu ana ujasiri wa kuvaa hadharani na tena ni binti mdogo kabisa, anaoneka mjuaji wa vitu vingi, na muonekano wa kimjini-mjini. Duh, niliishiwa pozi aisee.
Ujue kuna vitu vingine kuvielewa kuwa huo ni ujinga na ni utumwa kifikra sio lazima uwe mtu wa kanisani au msikitini. Kwa elimu na utandawazi ulipofikia sasa kubadili mmfumo wa kufikiria sio ombi tena bali ni lazima. Sasa inapotokea kuna mtu tena kijana anaamini juu ya kuvalishwa hirizi leo hii eti awe salama? Mwisho  wa siku unakuwa mtu wa kujihami na kutuletea shida tu kwenye jamii yetu.
Jamii ya kishirikina ni jamii 'sindikizaji'. Haitafanya maendeleo kamwe!!

 Ikitokea malaria imekushika ghafla unaanza kuwaza labda anakuchezea mtu mwenye hirizi kubwa kuliko yako. Ikitokea umepata ajari, watu wanakuja kukuokoa wanakuta umejifunga hirizi lako, nao watahusisha ajari hiyo na ushirikina. Ikitokea Mungu kakuita ghafla ndio kabisaaaa, ndugu waliobaki wanaaanza kutafuta mchawi utadhani wao wataishi milele. Dunia ya leo kuwa na imani za mfumo huo ni mzigo na nikujitengenezea mabalaa na kurithisha watoto na wajukuu ujinga. Nasema hili kwa maana hata huyu binti niliyemuona mimi mwenyewe najua fika haya atakuwa amejifunza kwa wazazi wake tangu utoto na hapa tayari amekomaa na imani hiyo, hivyo ukijichanganya tu na kumuoa wakati kafungamana na hayo madudu yao lazima watatafuta mbinu kuyaapenyeza kwa watoto wenu ili urithi uendelee kwa maana watoto watakuwa wanaenda kumtembelea bibi mzaa mama yao. Mama weeeeeee, !!!!

Wakati tunataka kuanzisha mahusiano yenye tija, kama vijana, tusijisahau na kuangalia uzuri wa sura pekee au elimu. Kipengere cha mila na desturi pia tamaduni zao huyo mwenzako jitahidi uzifahamu. Inaweza isiwe rahisi sana kutokana na baadhi yao kuficha na utakuja kustukia madhara, lakini tumuombe tu Mungu atusaidie katika kipengere hicho ili ukigundua usipoteze muda wako na kujikuta anakuja na begi ukidhani ni nguo kumbe ni mihirizi ambayo haimsaidii chochote zaidi ya kumpa presha tu kisaikolojia. Na ndio maana kuna mtu fulani aliniambia kwamba mtu ambaye ana amini katika hirizi, ikitokea siku hajavaa au imepotea katika mazingira yasiyoeleweka, mhusika ataugua hoiiiii napengine kufa kabisa. Sio kwasababu hajavaa, bali kwasababu anaamini hayuko salama.


Hebu huu mwaka 2018 uwe mwaka wa mabadiliko kwa wenye imani za ajabu na zisizo na tija kama hizi. Inasikitisha sana na wakati fulani inachekesha. Tumuombe Mungu kwa imani zetu atusaidie kutuongezea uelewa kuwa hatuwezi kukimbizana katika safari ya  maendeleo na uzalishaji mali kama bado mawazo na fikira zetu zipo kwenye imani za kishirikina. Natafuta mbinu za kuongea na yule mdada ili nimuulize mimi mwenyewe kuwa ‘kile ni kinini na kwanini kakivaa’ huenda ni ki-kuku cha kiasili, hahahaaaa. Akiijibu nitakuja ku-edit hii mada yangu. Sikubali nataka kupata majibu kutoka kwenye kinywa chake!!! Sasa kali ya mwaka mpya ni kwamba yule rafiki yangu hajawahi kujisumbua kuumiza kichwa kuliwaza lile lihirizi la yule mdada japo lipo waziwazi na kila siku linaonekana,yeye kapoteana na sura tu ya yule mdada hahahaaaaaaa, Khaaa!! Hatari sana.

Eng Nguki Herman. M
Instagram: @eng.ngukiwamalekela
Phone: 0763 639 101/ 0679 639 101
Asante kwa kusoma katika blog hii.Unaweza kusoma mada mbalimbali kwa kuchagua mwaka/mwezi kwenye eneo la chini (footer block) ambapo baada ya kusoma bofya neno older post na zitakuja nyingine na uendelee kwa mfumo huo kupata mada za awali ambazo hukubahatika kuzisoma.Au kama hauoni hilo neno bofya kwanza 'view the web version' ndipo utakuja mfumo utakaokuonesha neno older post kwa chini. Kwa elimu na ujuzi kuhusu maji, kilimo, udongo na mazingira tembelea blog: www.wadcotanzania.blogspot.com