I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Saturday 19 May 2018

Comments zinavyoweza kuvunja mahusiano/ ndoa

Mungu ndio anajua siri ya wapendanao


Rafiki yako akipost picha katika mitandao ya kijamii, kabla ya kuwaza kusema chochote kuihusu (ku-comment) huwa unachukua hata dakika moja kuwaza madhara yatakayotokana na comment yako? Au huwa unatiririka tu kuandika, tafakari itafuata badaye? Mara ngapi umeshuhudia comment ya mtu kwenye post ya mtu mwingine imezua varangati na majibizano yanayoashiria mmoja kaumizwa nafsi?
Nitajikita sana kwenye matukio ambayo ni ya kawaida kwa mapito ya mwanadamu kulingana na mazigira aliyopitia na watu aliokutana nao (exposure). Mara kadhaa nimekua nikisema kuwa mambo tunayofanya hayafutiki mioyoni mwa watu, ndio yanakaa na kuhifadhiwa. Na ndio maana kama ulikuwa na tabia fulani nzuri au mbaya wakati unasoma, basi hata kama baada ya miaka ishirini, wale uliosoma nao wanaweza wakawa wanawasimulia watu wengine ile tabia yako kwa maana wanaikumbuka! Ndio maana vijana tunatakiwa kuwa makini sana na kila tunachokifanya ili watoto wetu wakija kusimuliwa tusiumie mioyo au wakaona kumbe baba/mama yao alikuwa hamnazo.

Inakuwaje hii?
Inakuwa hivi: Unakuta Mkaka/mdada kapost picha yake mtandaoni anavalisha/anavalishwa pete ya uchumba (engagement) au amefunga ndoa safi kabisa. Ndio amefunga ndoa Mungu kambariki na kufikia hapo. Sasa mtu mwingine labda kasoma naye sekondari huko anakuja na kuona ile picha, na anakumbuka tabia za yule mdada/mkaka kuwa labda zilikuwa mbaya, au alikuwa na mahusiano motomoto na mkaka/mdada mwingine ambaye sio huyu aliyefunga naye ndoa! Bila hata kufikiria mara mbili unakuta anadondosha comment kama hii hapa:

v  Heh! Jamani mbona huyu sio yule shemela XY mliyekuwa naye shule jomoni? Mm we mdada/mkaka mhuni jamani, kha! Mlivyokuwa mnapendana vile kumbe ni uzushi tu? Hongera lakini.

v  Wacha weee, kumbe XY ulimpiga chini, koh,koh,koh simpatii picha povu lake akiona jamaa mwingine kakubeba.

v  Wapi XY?? Nani kamasaliti mwenzake?

v  Mhhhh, sitaki kuamini, yani XY alikuwa anakuhudumia hadi ukiugua, kumbe ilikuwa drama tu?
v  Hivi huyu ni XY kweli? Au macho yangu yananidanganya? Teh,the,teh

v  Duuuhhh kweli mapenzi ni kizungumkuti, kumbe XY mlikuwa mnachezeana tu, hongera lakini mwaya.

v  Heh, jomoni, wewe si ulitutambulisha XY kuwa ndio shemela mtarajiwa? Mliishia wapi tena? Hihihiiiii

v  Mwingine anaamua kuchukua hiyo picha na kupost kwenye ukurasa wake au kwenye magrupu ambako wewe huna uwezo wa kufuta comments wala kuona ili wakujadili vizuri. Tena anasindikiza na vi-emoji vya kinafikiii!!

Ukiangalia kwa makini hizo comments zinaonnesha huyu mtu anamfahamu vizuri mhusika na mapito yake. Na ukweli ni kwamba comment yake ipo sahihi kabisa!! Lakini je, unajua madhara yake kwa mhusika?
Mahusiano yana siri kubwa. Usiwavuruge waliopiga hatua chanya


Sikiliza kwa makini! Kila binadamu ana mapito yake aliyopitia, napengine aliingia kwenye mahusiano kwa sababu ya ujinga, shinikizo, kuiga , kujaribu au kwa nia njema lakini humo njiani akakuta mambo siyo yenyewe na kubadili gia angani. Ni kweli msichana au mvulana huyo alikuwa hivyo sekondari au chuo, lakini je, unajua yaliyomkuta? Wakati tunaongea na vijana huwa mara zote tunasisistiza kugeuka iwapo wapo kwenye mahusiano yasiyo na tija (Second chance). Hii inamaana kama ulijipachika mahala na ukagundua ulikurupuka au mambo tu huyaeleweki, basi jitoe ili upate nafasi ya kukua zaidi na kufanya uchaguzi mwingine.

Kuna mtu anasema;  ‘weeeee, maumivu yake ni hatareee!!!’ Ndio, kuna maumivu makubwa sana, utalia, utaapiza, utatoa matamshi ya laana, utajiona mjinga, hufai na mengine mengi, na kubwa zaidi unaumizwa na maswali ya waliokuwa wanajua mko pamoja! Lakini hayo yote ni mapito tu, chukua hatua, utapona na kuendelea kusonga mbele! Ukiona hauna amani, unaenda tu kama unamsindikiza mtu, na matarajio yako huyaoni au yule uliye naye analalamika kuwa matarajio yake hayaoni na mnasukumwa na huruma tu, chondechonde (kama maridhiano yamegonga mwamba) vunjeni huo uhusiano kabla hamjafika mbali kwa maana mnatengeneza bomu la kuja kusalitiana badaye. Haijalishi wangapi wanajua, sio marafiki, unaosali nao, wazazi wako, umempost sana mitandaoni nakadharika, HAO WOTE HAWATAKUJA KUISHI NA NYIE, NI WAPAMBE TU, LAKINI CHUMBANI MTAJIFUNGIA WAWILI PEKE YENU NA MUNGU WENU!

Acha akili za kijinga kucomment negative side ya mtu ambaye kapiga hatua. Ulitaka umuoe wewe? Au ulitaka akuoe wewe? Au ulikuwa unampenda akakugomea? Ameshavalishwa pete sasa! Unasemaje? Ndio ameshaoa/olewa, unatakaje? Unaandika maneno yanaingiza ndoa ya watu migogoro, mtoto wa watu anapata kazi ya kujielezaaaa kwa mume wake kisa nyau tu mmoja umekurupuka huko. Ulilazimishwa U-comment?? Wao wanajua walielezanaje mapito yao ya nyuma, na wamekubali kubebeana mizigo. Uliacha kumsema kipindi kile kapotea, sahizi kabadilika ndio unaleta maneno yako kwa reference ya mambo ya nyuma! Stop it please! Waache waoane, waache waoaneeeee!!
Ndoa na iheshimiwe na watu wote. Mambo waliyopitia kila mmoja huko nyuma hayakuhusu wewe mwingine (Third party)


Kitu cha msingi ukiwa kwenye mahusiano ni kuepuka kufanya ngono! Hii itakupunguzia maumivu siku ukiona mahusiano hayana tija na unaamua kuyavunja. ‘Nyanyachungu and 12 others reacted to your photo’, Heh, sawa tu endelea ku-react but wenzako wameshapanda madhabahuni na wanaazisha familia!! Sio lazima u-comment, unaweza kupita tu na kuacha kuwaza. Mwingine wanaonana kwenye daladala anaanza kumhoji, Oh fulani vipi, XY yuko wapi, Siamini kama hamkuoana naye, ilikuwaje , ooo,, iiii , kwikwiiii, Heh! Kazi ipo.

Kama unataka kujua yaliyowakuta, mitandao yooote ina inbox. Nenda huko inbox kamuulize nini kilitokea kwenye mahusiano yao, hata hivyo sio lazima akuambie kwa maana wewe sio stakeholder wa maisha yake. Na sio kukurupuka ku-comment maneno yatakayozua mzozo kati yake na mwenzi wake. Na bahati mbaya zaidi siku hizi unakuta karibu familia nzima ipo mtandaoni (pande zote mbili). Wazazi, wakwe, mashemeji, mawifi wote wapo huko. Sasa wewe unaleta comment kwenye post ya uchumba au ndoa ya mtu kutoa kashfa na ndugu wa upande wa pili wanaona, hapo lazima utaanzisha mjadala huko kwamba mtoto wetu kaoa/olewa na mtu asiyefaa na kuna uwezekano mkubwa wa ndoa kuingia shubiri kuanzia mwanzo kabisa!!

MWANAMKE: Furaha yako, amani ni zaidi ya mtu! Hivyo usiyumbishwe au kutishwa na mtu kwa maamuzi uliyofanya na umejiridhisha kuwa yana tija.
MWANAMME:Ujasiri wako na amani yako ni muhimu kuliko mtu. Ikiwa unaona matarajio ya binti wa watu huyafikii na unaishia kumtesa tu kwa mawazo ni bora umuache ili akajitafutie mtu ambaye atampa amani.
Ikumbukwe pesa, elimu au kazi ya mtu haina mchango mkubwa kwenye upendo, bali ni amani uliyonayo kuwa na mtu na matarajio ya hatua chanya mtakazopiga kwa pamoja.
Hata hivyo haya ni mawazo  yangu tu, sio lazima yafanane na ya kwako! Kwa moyo mkunjufu nikutakie tafakari njema.

Eng Nguki Herman. M

Instagram: @eng.ngukiwamalekela
Phone: 0763 639 101/ 0679 639 101

Asante kwa kusoma katika blog hii.Unaweza kusoma mada mbalimbali kwa kuchagua mwaka/mwezi kwenye eneo la chini (footer block) ambapo baada ya kusoma bofya neno older post na zitakuja nyingine na uendelee kwa mfumo huo kupata mada za awali ambazo hukubahatika kuzisoma.Au kama hauoni hilo neno bofya kwanza 'view the web version' ndipo utakuja mfumo utakaokuonesha neno older post kwa chini. Kwa elimu na ujuzi kuhusu maji, kilimo, udongo na mazingira tembelea blog: www.wadcotanzania.blogspot.com