I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Saturday 22 April 2023

Je kushika/kutumia au kuwa na mazoea na simu ya mumeo/mkeo kunaweza kuvunja ndoa?







Nimejaribu kutafakari juu ya jambo hili ambalo kwakweli sio jipya miongoni mwa jamii yetu. Ni kawaida kusikia makundi mawili yakikinzana juu ya kuwa na mazoea na simu ya mwenza wako hasa mke amekuwa akionywa sana kutokuwa na mazoea na simu ya mumewe. Hoja zimekuwa nyingi sana ambapo nyingi zimekuwa za kufikirika zaidi na zimejaa hofu ya kupigwa na adui usiyemjua.

Usiri kwenye simu ni uchochoro wa usaliti na kuishi kinafiki kwenye ndoa. Kwa bahati mbaya na jamii inawadanganya, Ohh usishike usije kupata presha, oh ana mambo yake sio lazima uyajue, what? Unapoingia kwenye ndoa hakuna mambo yako, kila kitu lazima kifahamike kwa wote. Ofcourse kuna vingine sio vya maana sana hata ukiviacha havina madhara. Nasisitiza kama hauna uhuru na simu ya mwenza wako, hujuwi password wala huwezi kuitumia, umepigwa marufuku kupokea wala chochote "basi mnaishi maigizo kwa asilimia kadhaa. 

NB: Kama uko comfortable keep going na maumivu yako.

Natoa pole kwa dada zangu ambao kwenye kitchen party na sendoff wamama wanawaambia simu ya mumeo ni sumu, sasa unakwenda kufanya nini kwa mtu mwenye sumu? halafu hapohapo wanakwambia nyie ni mwili mmoja, mwili what? mwili who? where? Which mwili my friend,  hakuna mwili wala ubavu hapo, ni maigizo mwanzo mwisho. Watu wakosee namba kwako/kwake tu? Mwenza ni wakili (advocate) lazima ajue vyote na ndio atakuwa wa kwanza kuulizwa/kukutetea likitokea lolote. Ni ngumu kumeza lakini ndio ukweli utakuja kuelewa siku moja.

Ok sawa, ulikuwa na mahusiano kabla ya huyu, si unasema tu? Na si unawaambia tu hao X,Y na Z kwamba sasa umeshaoa/olewa na unakata rasmi mawasiliano ya mahusiano  nao?. Kama hatakuelewa ujue na yeye hajakomaa kuwa mke/mume. Mpasuko unaanza mara tu utakaposema 'tunachat tu kwa siri, hatajua, siku unaumbuka ndio unasema 'tulikuaga.....au she/he is just a friend'

'Ee Bwana ukiokoe kizazi chetu'. Ni kweli hakuna mtu mkamilifu lakini mengine ni ujeuri wetu, kiburi chetu, ujinga wetu na kusahau au kujisahaulisha maana halisi ya agano la ndoa.

Ok bado hamjafunga ndoa, vipi ukimuuliza mtakuwa huru kila mtu kwenye simu ya mwenzake mkishafunga ndoa? Nasisitiza mkishafunga ndoa kwasababu kama sijafunga ndoa na wewe maana yake bado niko mawindoni at any time t seconds akipatikana aliyekuzidi vigezo nitafunga naye ndoa. Hivyo wakati huo kuna uwezekano wa kuwa na mitego mingi. Swali hapa ni ndani ya ndoa anasemaje? Majibu yake tu yatakupa picha kama hapa ni tia-maji tia-maji au la! Sasa jichanganye 'oh mapenzi upofu, hayaangalii sijuwi nini" sawa mwiba ukiingia vizuri I tell you utaona hata kwa lazima na utalia machozi! Nasema 'maacho yatafongokaaaaa'

Ee Bwana utuokoe sisi!

Nguki Herman.M

Instagram: @eng.ngukiwamalekela
Twitter: @engngukiherman

Asante kwa kusoma katika blog hii.Unaweza kusoma mada mbalimbali kwa kuchagua mwaka/mwezi kwenye eneo la chini (footer block) ambapo baada ya kusoma bofya neno older post na zitakuja nyingine na uendelee kwa mfumo huo kupata mada za awali ambazo hukubahatika kuzisoma.Au kama hauoni hilo neno bofya kwanza 'view the web version' ndipo utakuja mfumo utakaokuonesha neno older post kwa chini