I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Wednesday 28 June 2017

MWANAUME, KUMUOMBA MSAMAHA MWANAMKE NI HESHIMA.

Mwanaume anayejitambua haoni shida kuomba msamaha

Salamu. Leo nataka nizungmze na wanaume wenzangu. Hivi karibuni niliandika tafakari fupi juu ya mapishi na wanawake. Japo sikuweka huku kwenye blog, kule kule kwenye facebook, instagram na watsup kila mtu alitoa mtazamo wake, hasa watsup uliibuka mjadala mkali kwenye baadhi ya makundi ambako nilishirikisha. Na kiukweli lengo langu halikuwa kumaanisha kuwa mapishi ni ndoa, bali ndoa ni composite function ambayo ndani yake kuna vitu vingi sana, na lengo ni kuweka vitu vingine vyote sawa (keeping other factors constant /CETERIS PERIBUS) na kuangalia athali za mke ambaye hapendi au ni mvivu kupika.

Wakati wa kuchangia mada hiyo, wapo waliosema mbona umewazungumzia wasichana pekee? Nikaahidi kuja na ugonjwa unaowasumbua wanaume wengi kama compensation, kwa maana lengo ni kujenga na sio kushushua au kuhukumu. Sasa nizungumze juu ya suala la wanaume kuona ugumu kuomba msamaha kwa wanawake pale wanapowakosea. Ni ukweli usiopingika wanaume wengi hudhani wao kuomba msamaha kwa wanawake ni kujishushia hadhi au kuonesha udhaifu. Wengi hujitutumua na kuishia kusema ‘POTEZEA TU, au VUNGA, au YAISHE au KAUSHA’. Sasa sijui nini kinakaushwa hapa, ni mishikaki au chipsi? Sijuwi mimi.

Kwa haraka mtu anaweza kudhani hii ni kwenye ndoa tu, lakini hata kwa vijana ambao hawajaoa, inaweza kutokea mkakwaruzana au kukwazana na msichana yoyote mnayesoma naye au rafiki wa kawaida ambapo wanaume wengi hupata ukakasi kutamka neno ‘nisamehe dada yangu, nisamehe rafiki yangu’. Huu ni ujinga, na ujasiri wa hasara kwa maana haijaandikwa kuwa wanawake tu ndio watakuwa wanakosea. Ni vyema wanaume kujifunza kuomba msamaha pale unapomkosea mwanamke yoyote ili isikupe shida hata ukiingia kwenye ndoa na kufanya kosa fulani kwa mkeo, kisha kuanza kuona ukakasi kuomba msamaha. Ukiulizwa kitu ambacho unajua kabisa umefanya kosa, unaanza kujitutumua kuonesha hasira na kutengeneza mazingira kuwa kwa wanaume ni kawaida kufanya hicho kitu, hapana, hiyo sio kweli.
Kuomba msamaha hakukupunguzii kitu. Kwani hujuwi kuwa umekosa ?

Kwa mwanaume kuomba msamaha kwa mwanamke hakupunguzi uanaume wako wala kukudisqualify kutoka kwenye nafasi uliyopo, bali ni tendo la kijasiri na ukomavu kifikra , kimtazamo na maamuzi. Ile amani anayopata mwanamke baada ya kuombwa msamaha ni baraka kwako. Halafu masikini ya Mungu wanawake hata hawaoni kazi kusamehe, hasa ukionesha kweli umeelewa kosa. Mara nyingi kwasababu ya kujiona dhaifu hujikuta wanasamehe hata bila kuombwa msamaha, sawa hili ni zuri sana kuwa nalo hata kwa wanaume, lakini wakiombwa msamaha  inakuwa jema zaidi.

Hata huko kwenye ndoa mara nyingi baadhi ya dada zetu walioingia huko wanatushirikisha, utasikia ‘Weee baba fulani hata akirudi usiku usijaribu kuuliza, atakuwashia moto hadi ujikute wewe ndio unaomba msamaha kwa kumuuliza, amesema wanaume huwa hawaulizwi’, mhhh, hii sio sifa njema, sasa kama mnajiita nyie ni mwili mmoja, halafu unasema usiulizwe, basi na wewe usimuulize kitu. Ni kweli mwanaume ni kichwa cha nyumba na hilo ni agizo la Mungu mwenyewe, sawa lakini ukimkosea mkeo au mwanamke yoyote ufahamu kuna ubinadamu, na nafsi yake inafukuta na kujikuta anawaza  mambo mengi ya ajabuajabu ambayo angekufanyia kama angekuwa na huo uwezo.

Ushauri wangu kwa wanaume wote tujifunze kuomba msamaha kwa jinsia zote, na sio kwa mwanaume mwenzako tu kisa umeona ana minguvu kuliko wewe kwamba akiamua anaweza kukugeuzia betri na umeme ukashindwa kuwaka? Mhhh, hapana. Kama ambavyo inakukereketa mtu aliyekukosea asipoomba msamaha, ndivyo ilivyo kwa wanawake ukiwakosea na ukatia mgomo kuomba msamaha eti unaogopa kujishushia heshima, nani kakudanganya? Wewe omba tu msamaha kwa unyenyekevu wote, utajiongezea heshima kwake na kujitofautisha na wengine wanaochukulia kila kitu generally bila kuwa na unique behaviours.
Mwingine akijipapatua weee anaamua kuandika kaujumbe kamsamaha na kuweka mezani. Teh,teh, sawa ni jambo jema, lakini jifunze kutamka kwa kinywa chako then suppliment na hayo maandishi mazuri.

Kwa upande wangu sioni shida kuomba msamaha endapo nitagundua nimemmkosea mtu wa jinsia yoyote kwa maana hainipunguzii kitu chochote zaidi ya kuniongezea tu reputability na kutowaza kuwa hivi ananifikiriaje nilipofanya kosa au kumkwaza bila kuomba msamaha. Wafundisheni watoto wakiume kujua umhimu wa kuomba msamaha kwa vinywa vyao kwa jinsia zote pale wanapofanya makosa kama ilivyo kwa watoto wa kike. Hapo tutakuwa tunajenga jamii inayojielewa na kuifanya jamii kukalika na kuwa na mapatano pasi na kuwa na ubabe na unyanyasaji kwa watu fulani. Mtu anayeomba msamaha akikosa yupo kwenye nafasi nzuri ya kushirikishwa mambo mengi mazuri kwa maana anazungukwa na watu wasio na kinyongo. Usiombe mwanamke akuchukie kisawasawa kisa ulimkwaza na kugoma kuomba msamaha weeee, huwa wanachefuka hao balaa tupu. Tuwapunguzie mizigo ya kuwaza mengi, tuwaombe msamaha kila tuwakoseapo. OMBA MSAMAHA KILA UKIFANYA KOSA BILA KUJALI NI KUBWA AU DOGO. Tafakari njema.

Eng Nguki Herman.M
Phone: 0763 639 101/ 0679 639 101

Instagram: @eng.ngukiwamalekela
Unaweza kusoma mada mbalimbali kwa kuchagua mwaka/mwezi kwenye eneo la chini (footer block) ambapo baada ya kusoma bofya neno older post na zitakuja nyingine na uendelee kwa mfumo huo kupata mada za awali ambazo hukubahatika kuzisoma.Au kama hauoni hilo neno bofya kwanza 'view the web version' ndipo utakuja mfumo utakaokuonesha neno older post kwa chini. Kwa elimu na ujuzi kuhusu maji, kilimo, udongo na mazingira tembelea blog: www.wadcotanzania.blogspot.com

No comments:

Post a Comment