I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Sunday 20 August 2017

SABABU KUU MBILI ZA KUPENDA

Busara inatakiwa sana kuelewa mantiki ya upendo kwa mtu

Suala la kupenda ni suala mtambuka ambalo wakati fulani watu hutumia nguvu nyingi kujitahidi kutetea mantiki yake na kujikuta wanaishia kuongea uongo au kuharibu uhalisia. Kwa kawaida mtu akiulizwa sababu za kumpenda mtu fulani, anaweza kutoa majibu haya au yenye mlengo huu:

  • Kwasababu nayeye ananipenda
  • Kwasababu ni mzuri (mrembo/ handsome)
  • Kwasababu amewahi kunisaidia nilipokuwa na shida
  • Kwasababu anaonekana atakuja kuwa baba/mama bora wa familia
  • Kwasababu ana akili sana darasani
  • Kwasababu anaonekana mpambanaji sana na anajituma
  • Kwasababu ana pesa nyingi sana, nikiwa naye siwezi pata shida
  • Kwasababu ni mpole na sio mlevi
  • Na mengine mengi


Sawa lakini yote hayo huenda ukawa ni ushawishi wa kupenda, lakini sio sababu ya kupenda. Kuna utofauti kati ya sababu ya kufanya kitu na ushawishi wa kufanya kitu. Sababu ni hamu na muwako wa ndani wa kufanya kitu, kumbe ushawishi ni kitu ambacho kinakufanya uamini kuwa utakuwa salama baada ya kufanya hicho kitu.
Mfano rahisi. Tamaa ni sababu ya kufanya ngono, lakini matumizi ya kondomu ni kishawishi cha kufanya ngono. Nadhani hapo umeelewa utofauti kati ya haya maneno mawili
Upendo ni lazima uwafaidie wote , na sio wa kibinafsi


Sasa sababu mbili kuu za kupenda ni hizi hapa:
  1. Ni hitaji la kila kiumbe hai
  2. Ni amri


KUPENDA KAMA HITAJI
Hili lipo wazi  kabisa, hakuna mtu asiyetaka kupendwa. Ndio hata mimi najisikia raha sana ninapogundua mtu fulani ananipenda. Kuanzia wazazi wangu, walezi wangu, wanafamilia, walimu na marafiki wa jinsia na kada zote. Kupendwa kunaleta msisimko wa aina yake na kukufanya uone uko ‘PROTECTED AND SECURED’  kwa sala za wanaokupenda na unaamini muda wowote ukiwashirikisha jambo wataitikia kwa muitikio chanya (positive response). Ni wazi mtu kama hakupendi hawezi kukuombea kwa Mungu mafanikio au hata afya njema. Fuaraha yake ni kuona unaishi kwa wasiwasi, mateso na maumivu au hata kutoweka kabisa. 

Hili halipo tu kwa binadamu, hata mifugo yako nyumbani, ikigundua unaipenda na kuihudumia, utaona kabisa inaonesha ishara ya kukufurahia na kila mara urudipo nyumbani lazima irukeruke miguuni pako. Najaribu kuwaza hata miti na maua ya nyumbani ambayo kila siku unayatunza, kuyamwagilia na kuyawekea mbolea, laiti yangekuwa na mdomo yangezungumza na kukubali (appreciate) upendo unaoonesha kwayo.
Ukifahamu hilo ndivyo inavyokuwa upande wa pili, kama unafurahia kupendwa basi na wewe kuwapenda wengine ni lazima, kwa maana wanahitaji hilo, na ni la kudumu.  Watu wanapata vidonda vya tumbo, presha na msongo wa mawazo na wengine afya zao kuzorota mara wakigundua hawapendwi au kutothaminika na watu walio karibuu nao. Ulishajiuliza siku mtu wako wa karibu akikutamkia ‘SIKUPENDI WEWE, YANI NATAMANI KAMA NISINGEIONA HIYO SURA YAKO’ utajisikiaje? Wakati fulani sio lazima mtu atamke, lakini mambo yake tu yanatoa picha kuwa hampendi mtu fulani.


Na wapo wengine wako katikati (neutral), yani yeye anajipenda yeye mwenyewe tu, mweee jamani, sasa si uende baharini huko utafute kisiwa ukae huko peke yako? Kama unaona hilo ni gumu, tafsiri yake ni kwamba tunahitajiana na kutegemeana. Unapotembea tu huko nje na kuona watu wamefurahi, hawana huzuni, hiyo ni dawa pia na fundisho kuwa huwezi kujifurahisha mwenyewe, ili mtu ucheke, lazima uchekeshwe na mtu mwingine, kama sio mko uso kwa uso basi hata kwa message tu mnazochati. Kwa lugha rahisi tujifunze kuwapenda watu pasi na kujali matabaka ya aina fulani

Angalizo: Kwakuwa kupendwa ni hitaji, wapo wanaotumia mgongo wa uhitaji huo na kupeleka kwa watu upendo nusu kilo,  mateso na maumivu kilo hamsini. Hiyo ni dhambi kwa maana mpokeaji alijiandaa kuwa aliyemuendea ni mtu mwema anayefahamu kuwa kupenda na kupendwa ni lazima kati ya mtu na mtu au jamii na jamii.
Ni rahisi kutamka neno NAKUPENDA, lakini ukweli tunao wenyewe mioyoni


KUPENDA KAMA AMRI
Upendo ni amri ya Mungu. Nimejaribu kufuatilia mawaidha ya dini zote, mathalani Wakristu na Waislamu, wote wameagizwa kupenda, na kwamba kama wasipowapenda binadamu wenzao basi na Mungu hatawapenda wao. Ahaaaaa, kumbe kama hujui kupenda basi huwezi kuambatana na baraka za Mungu. Upendo hauhitaji pesa au mazingira maalumu au kuwekewa mikakati kama bajeti ya kujenga reli ya standard gauge, la hasha! Ukitambua tu kuwa ni amri ya Mungu , basi ni kujifunza tu kuwa ni sehemu ya maisha yako.


Upendo unaozungumzwa hapa hauna masharti, vionjo tatanishi na vitenzi vichokozi vyenye mlengo wa kumuinua shetani. Kwani hujawahi kuona mtu anasema ‘nilimuua mume wangu ili niishi kwa amani na mtu NINAYEMPENDA’, Sasa huo ni upendo? Hapana, ni ushetani kwa maana huyu wasasa akibadilika kidogo tu na akaja anayejali zaidi, basi atamuua na huyu ili afurahie na huyo mwingine. Hivyo ndugu zangu ni bora tukafahamu jambo hili kinagaubaga ili tusichanganye mambo na kudhani kupenda ni hiari, hapana. KUPENDA NI LAZIMA, lakini KUHUSIANA NI HIARI YA MTU. Kumpenda mtu sio lazima muhusiane, au kuzoeana bila mipaka, hapana, tupendane, tushirikiane, lakini mipaka na heshima iwepo ili kulinda utu wa mtu, misingi ya kijinsia, utamaduni na uhuru wa kuamua juu ya msatakabali wa maisha ya baadaye ya mtu binafsi. Kama una swali, hoja au maoni, kuwa huru hapo chini eneo la comments. NAWAPENDA WOTE

Eng Nguki Herman. M
Instagram: @eng.ngukiwamalekela
Phone: 0763 639 101/ 0679 639 101
Asante kwa kupitia na kusoma haya.Unaweza kusoma mada mbalimbali kwa kuchagua mwaka/mwezi kwenye eneo la chini (footer block) ambapo baada ya kusoma bofya neno older post na zitakuja nyingine na uendelee kwa mfumo huo kupata mada za awali ambazo hukubahatika kuzisoma.Au kama hauoni hilo neno bofya kwanza 'view the web version' ndipo utakuja mfumo utakaokuonesha neno older post kwa chini. Kwa elimu na ujuzi kuhusu maji, kilimo, udongo na mazingira tembelea blog: www.wadcotanzania.blogspot.com

9 comments:

  1. Ni kweli kabisa kiongozi, Hatuwezi kuifanya dunia sehemu yenye Amani kama hakuna upendo Lets love one another as God did it to us. Pamoja sana my brother.

    ReplyDelete
  2. ������
    Kupenda ni AMRI
    Asante kaka

    ReplyDelete
  3. That Great Bro...Kikubwa ni hii iwe ni uhusiano wa kimapenzi au uhusiano wa kindugu/kirafiki we can'nt love by our own, when Jesus is inside of me I can Truely love this is because Jesus is Love... when one missing Jesus in His heart its difficult for him/her to love is like he/she missing love.... that why most of people now they don'nt love because they mising Love(Jesus). The big deal is Jesus inside of the heart of a person.When Jesus inside of a person love is guaranteed.I witness when I did not received Jesus i did not love my fiancee who is now my wife ...the day I received Jesus the love was started to flow to her and everybody and now I count myself as nothing before others.

    ReplyDelete