I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Saturday 3 December 2016

TUNASHANGAA YAMEOTAJE, NA TUMEYAPANDA WENYEWE

Kila  mtu amejeruhiwa/kuathiriwa na janga la UKIMWI kwa namna fulani.

Habari. Bila shaka unafahamu tarehe 1 Desemba ya kila  mwaka ni siku ya UKIMWI duniani. kabla sijaanza kuzungumzia lengo langu hasa kukihusu kichwa cha mada yangu, basi pitia takwimu hizi hapa chini juu ya hali ya UKIMWI Tanzania Bara zilizotolewa Dec 1 2016 na TACAIDS kupitia viongozi mbalimbali na vyombo vya habari:

Takwimu
Maelezo
5.3%
 Maambukizi ya UKIMWI kwa Tanzania bara. Sawa na watanzania 5 kati ya kila watanzania 100
6.2%
 Wastani wa wanawake walioathirika na maambuziki ya UKIMWI.  Sawa na wanawake 6 kati ya kila wanawake 100
3.8%
Wastani wa wanaume walioathirika na maambuziki ya UKIMWI. Sawa na wanaume 4 kati ya kila wanaume 100
10.6%
Vijana kati ya umri wa miaka 15-24 wanamambukizi ya UKIMWI, sawa na vijana 11 kati ya kila vijana 100

Ikumbukwe takwimu hizi ni kwa wale ambao wamepimwa iwe ni upimaji wa hiari wa kawaida, kabla ya kufunga ndoa, wakati wa uchangiaji damu au wakati wa ujauzito. Utakubaliana na mimi kuwa kuna kundi kubwa sana la waathirika hasa maeneo ya vijijini ambako watu wanapata maambukizi ya ukimwi lakini hawana elimu juu ya utambuzi wa afya na wengine huishia kudhani wamelogwa na kujikuta wanafakamia miti shamba au kwenda kwa waganga wa kienyeji kupiga lamri nakadharika. Kwa lugha rahisi mimi naamini hali ya maambukizi ni  mbaya zaidi ya inavyodhaniwa kwa takwimu.

NANI MCHAWI?
Sio mimi ni wewe. Hapana ni wewe sio mimi

Sisi wenyewe na serikali yetu. Ndio ni sisi wenyewe tunajiloga na kuitmbukiza jamii yetu katika shimo la huzuni na giza totoro inayoumiza na kuangamiza kizazi hiki na kijacho. Kundi kubwa la watu wanapigia debe maisha ya kufanya ngono kama ni utaratibu wa kawaida wa maisha ya watu hasa vijana. Watu wenye ushawishi mkubwa wamefumba mdomo kuongea ukweli na hali halisi ya mambo kwenye visababishi vya kuenea kwa UKIMWI, na badala yake wamejikita zaidi kutoa matamko ya kulalamika matokeo yake na kuomba, kutafuta na kutumia fedha nyingi kushughulikia matokeo ya UKIMWI.

Kwa macho yangu nimeshuhudia shirika fulani linatembelea mashuleni na makundi ya vijana wa kucheza ngoma za burudani, mashindano ya kucheza na kimba kisha kutoa zawadi za mabox ya kondom kwa vijana hao. Kama hiyo haitoshi, pembeni waliweka banda na kuwaalika vijana wa kike kwa wakiume waende ili wakafundishwe namna ya kufanya ngono kwa kondom, tena taasisi ya kielimu. Na nilishuhudia vijana wasio na mpango mkakati wa maisha yao wakimiminika kwenda huko, halafu bila aibu tunashangaa kwanini maambukizi yanapanda?. Kisingizio cha kondomu kimetumika sana kukoleza moto wa ngono kwa vijana, na asilimia kubwa ya vijana wamenasa kwa mtego huo na bado wakayabeba maambukizi. Kondom hazijafika leo, zipo kabla ya UKIMWI na bado maambukizi yanazidi kupanda,  bado hatufungui macho na kuelewa kuw tunawekeza kwenye mradi usiozalisha. 
Muda wa kunyoosheana vidole haupo. Tumia akili yako kuweka malengo ya kujitoa kwenye ngono. Mungu atakuepusha tu. Ni kweli na hakika. Jionee huruma wewe ,kizazi chako na cha wengine.

Kupitia takwimu hizo hapo juu unaona vijana ambao tunawaita 'sexually active group' ndio vinara wa maambukizi. Maambukizi hayo yanachochewa na wao wenyewe pia mabinti kufanya ngono na watu wazima ambao wanamaambukizi ya UKIMWI na hutumia fedha zao kama ulimbo wa kuwanasa wasichana wadogo.

KWANINI WANAWAKE WANAONGOZA KWA MAAMBUKIZI ?

Katika vitu vya kuchekesha na kuudhi ni uchambuzi wa watu tena wasomi juu ya swali hili, 'kwanini wanawake wanaongoza kwa maambukizi ya UKIMWI'. Nasema inachekesha kwakuwa hakuna hata mmoja niliyemsikia akigusia chimbuko na mzizi wa tatizo hili,bali wote waling'ang'ana kwenye matokeo, isipokuwa baadhi ya viongozi wa dini walisema ukweli. Nilikuwa nawafuatilia kwa karibu sana. Wengi walitumia kigezo cha unyanyasaji wa kijinsia, ubakaji, umasikini nakadharika, vitu ambavyo vinachangia kwa kiai kidogo sana.

 Inachekesha zaidi kwakuwa sikusikia hata mmoja akihoji kwanini kwenye nyimbo na miziki wanaume wanavaa suti na kupendeza  lakini wasichana wanavaa nguo za ndani pekee na visidiria  na kuachia maungo yao nje? Hakuna aliyesema kwanini wanawake wa sasa hawaoni thamani tena ya miili yao na kutembea uchi barabarani huko na kuamsha hashiki za wanaume pia kutoa mafunzo ya udadisi waa ngono kwa watoto wadogo? Nyie mnojiita watetezi wa haki za ujinsia hasa haki za mwanamke na unyanyasaji, hapa huwa mnavaa miwani ya tinted sio? Ukweli ni kwamba tabia ya wasichana na wanawake kujianika miili yao na kuona wao ni bidhaa inayohitajika sana kwa wanaume (highly demanded commodity) kumefanya wanaume wengi kuwa na mahusiano na wanawake zaidi ya mmoja. Ni wanawake wachache sana wenye mahusiano na wanaume zaidi ya mmoja, lakini wanaume wengi wamejilundikia wanawake kwakuwa wanawake wenyewe (sio wote) waamekuwa mawakala kamili wa kusajili wanaume kwa mavazi yao na kushindwa kusema HAPANA kwa ngono. Hivyo mwanaume mmoja anayeishi na maambukizi ya UKIMWI ni rahisi kusambaza kwa wanawake wengi zaidi kuliko uwezekano wa mwanamke mmoja anayeishi na maambukizi kusambaza kwa wanaume wengi zaidi. Hii inatokana na sababu za kimaumbile pia, ukichanaganya na maelezo yangu hapo juu basi unapata HADITHI NJOO ,UTAMU KOLEA.
Wanawake ni waleta uhai mpya. Ni wasaidizi kamili wa Mungu kuleta watu duniani huku. Tabia ya kujitoa ufahamu na kujidharirisha kunafanya hata watoto walio matumboni kuanza kulia kwa hofu kwakuwa wamebebwa na wazazi maharamia wasiojali utu na kujisitiri kwa heshima. BADILIKA LEO

Kwa mtindo huu, suala la UKIMWI litabaki kuwa miradi ya watu ya kujitengenezea fedha, na kufurahia maambukizi kupanda kwakuwa bila UKIMWI na wao watakosa kazi. Ni bora tukaongozwa kwa busara binafsi, na kujifunga mkanda, yani KUSEMA HAPANA KWA TABIA YA NGONO NA TABIA AMBATANISHI. Nikisema haya kwa mtu ambaye anjiona amekubuhu kwenye tabia hii, huenda anashangaa na kuona naandika nadharia, lakini huu ni ukweli ambao huenda ukawa ni mgumu kuumeza lakini hamna namna, utabaki kuwa ukweli. Kwani ukisema HAPANA KWA NGONO unatoka vidonda sehemu fulani ya mwili? Mwanamke ukiamua kusema hapana, mwanaume hana jipya. Hisia za wanaume huwa zinapanda haraka, na ukisema hapana na kuondoka, huwa zinashuka haraka pia na ufahamu kurejea kama ilivyo sufuria iliyotolewa kwenye jiko la moto. Wakati wanawake hisia zao hupanda taratibu (hasa pale unapompa nafasi mwanaume ya kujieleza na kujiweka karibu na wewe), kisha mkifika juu, huwa zinabaki juu hukohuko kwa muda mrefu kama chungu kilichotolewa kwenye jiko la moto. Ndipo hapo utasikia mara wanaume baba yao mmoja, oh, nataka mtoto  tu, lakini sitaki kuolewa,, sitakuja kumwamini mwanaume yoyote, kwa maana wote ni waongo, oh,,,,,, ah,,,,, nakadharika. Kuongezeka kwa watoto wa je ya ndoa au wasio na mlezi ya moja kwa moja kutoka kwa baba zao, kunatoa picha halisi ya hili jambo. Wazazi wengi au hawataki au hawawezi kuzungumza ukweli na mabinti zao, na wakijitahidi sana wanaishia tu kusema UWE MAKINI, AU TUMIA AKILI. Maneno ambayo hayaakisi kabisa kuwa mzazi unataka binti yako au kijana wa kiume aepukane na janga hili la UKIMWI.

Ukweli ni kwamba mimi ni mmoja kati ya watu ambao hawashangai kabisaaaaaaaaaaaaaa juu ya idadi ya wanawake wenye maambukizi ya UKIMWI kuwa kubwa kuliko wanaume, kwasababu wao ndio huchochea hurka ya wanaume kuwapapalikia. Kwa sentensi hiyo sijasema wanaume hatuna makosa, hapana, nasi pia tunatakiwa kupambana na udhaifu wa miili yetu, kujifunza kuuthibiti mwili kwa maana ni ukweli wa mchana kuwa changamoto ni nyingi, kichwa kinavurugika unapoona miili ya wanawake waziwazi, lakini jikubali, badili mazingira, mshirikishe Mungu, sema HAPANA PIA KWA VISHAWISHI, usitumie pesa zako ili kukoleza mapambano na mikikimikiki ya ngono. Kama umeoa basi ridhika na mke wako kwa maana ndiye Mungu aliyekupangia. Kma hujaoa basi timiza malengo yako na baadaye fanya uchaguzi sahihi.

Sitaki kusema imani za dini zinasemaje juu ya hili, lakini nijuavyo mimi HAKUNA DINI HATA MOJA INAYOSHABIKA NGON KABLA NA NJE YA NDOA. KUSUBILI INAWEZEKANA, SEMA HAPANA KWA NGONO ILI KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI NA KUEPUSHA MATUMIZI YA FEDHA NYINGI AMBAZO ZIMEKUWA ZIKIELEKEA HUKO. Kumbuka kwa Tanzania kuanzai DEC 1, 2016 serikali imezindua Bodi ya udhamini wa mfuko wa UKIMWI ambako mabilioni ya fedha yanakusanywa kutoka vyanzo vya ndani ili kushughulikia mambo ya UKIMWI na kupunguza utegemezi kwa wahisani wa nje ambao vigezo vyao hubadilika mara kwa mara..
Nikutakie tafakari njema na tufanye maamuzi ya busara ili kuzikomboa familia zetu. Mungu akubariki.

Eng Nguki wa Malekela
0763 639 101/ 0679 639 101
ngukiherman@ymail.com
UCE Tanzania-Volunteer
03 Dec 2016
Thank you for visiting my blog. Click home/ view the web version to see other topics on list ( in case you don't), which have been categorized by months posted. Eg to see the topics posted last month, just click November.  The same for October. You are welcome. Also for Professional information about Agriculture, water resources, soil and environmental conservation visit www.wadcotanzania.blogspot.com  Eng Nguki  

Ili ufanye vizuri unahitaji juhudi, ili ufanye vizuri  zaidi unamuhitaji Mungu.Hauwezi kufeli darasani kwasababu unatoa sehemu ya muda wako kufanya kazi za Mungu. Usikate tamaa., angalia unakosea wapi na urekebishe. Huenda ukapitia Chamgamoto kidogo na ukaanza kumlaumu Mungu au mtu fulani, hapana, utapita tu, kaza mwendo. 25 Nov 2016-SUA

Wednesday 23 November 2016

SIO RAHISI HATA KIDOGO.

Mungu yuko upande wetu. Tujibidiishe kusali na kufanya kazi.

Tumsifu Yesu Kristu.
Namshukuru Mungu paoja nanyi kwa neema ambazo anatujalia kila siku ingawa hatustahili. Maovu yetu mara kadhaa yametutenga mbali na Mungu na kutusogeza kubaya ambako haukuwa mpango wa Mungu Zaburi  103:12 Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi
Ni kweli, tumefanya maovu na lazima tukiri wazi kwa vinywa vyetu
Zaburi 106:6 Tumetenda dhambi pamoja na baba zetu, Tumetenda maovu, tumefanya ubaya.
Isaiah 59:12 Maana makosa yetu yamezidi kuwa mengi mbele zako, na dhambi zetu zashuhudia juu yetu; maana makosa yetu tunayo pamoja nasi, na maovu yetu tumeyajua;
Jeremiah 14:20 Ee Bwana, tunakiri uovu wetu, na ubaya wa baba zetu; maana tumekutenda dhambi..
Mara nyingi nikiwa nasoma chuoni, wakija wanafunzi ambao walishamaliza walikuwa wanatutia moyo kwa kutuambia shule sio ngumu mtafaulu tu. Ni kweli nen hili ni muhimu na la faraja kwa wanafunzi wanaoendelea. Mimi pia nimemaliza hapa chuoni, lakini niwaambie tu bila kuumauma maneno, shule ni ngumu, ten asana tu Ndio shule sio rahisi hata kidogo. Kwa sentensi hii sina maana kwamba huwezi kumaliza au kufaulu vizuri, bali juhudi za makusudi na kujitoa sadaka ya muda lazima viwepo kwa nguvu zote.

NINI KINAFANYA CHUO/SHULE WAKATI FULANI KUWA NGUMU KUPITA KAWAIDA
Kwa ambao wamewahi kutumia computer:, ikitokea unahamisha vitu vingi  kutoka kwenye flash disk kwenda kwenye computer au kinyume chake, utaona computer inaandika two days left , ikimaanisha hiyo kazi ya kuhamisha mafaili yako itachukua siku mbili, baada ya dakika kama tatu, utaona inakambia bado siku moja, baada tena ya dakika chache inakuambia bado msaa sita, tena baada ya muda mfupi inakwambia bado nakika kadhaa, badaye sekunde na ile kazi inakwisha ndani  ya robo saa tuamaa na kuongeza juhudi hifanya iishe mapema na kwa ufanisi. Hivyo kama mtu sio mvumilivu na anasafari baada ya lisaa limoja, akiona ile 2 days left, basi anaahirisha na kuona itamchelewesha. .Kwa tafsiri rahisi ni wamba kazi yoyote mwanzo huonekana kubwa na nzito sana , na ndiyo ilivyo, lakini kutokata  Zipo sababu nyingi sana. Pamoja na changamoto ya uwezo binafsi wa mwanafunzi kitaaluma, ulevi, msongo wa mawazo na majukumu yanaayozidi uwezo, naomba nizitaje sababu kongwe mbili ambazo ni UVIVU NA NGONO.


UVIVU: Mithali 19:15 Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.
Sina sababu ya kuanza kudadavua uvivu ni nini. Kwa kifupi ni hali ya mtu kukwea kutimiza wajibu wake kwa makusudi. Mvivu hufurahia matokeo mazuri pasi na kuangalia mchakato ulioleta matokeo hayo. Uvivu upo kwenye vitu vingi sana. Huenda ni katika kusoma, au katika kusali. Mtu mvivu kusali hupima nguvu za Mungu kwa vitu vichache alivyovichagua yeye. Kwa mfano akiwa hahudhurii jumuiya, bali misa anaenda na mambo yake ynamuendea vizuri, basi anaridhika na kujiambia kuwa Mungu katosheka na donoadonoa yake kwenye mikusanyiko ya sala, hivyo wale ammbao wanaenda jumuiya na kufanya kazi kadha wa kadha za kanisa, nabado mambo yao ni magumu, anadhani hawapo sawa kiimani au wanakosea mahala fulani.

Wito wangu kwenu ni kusali misa na sala za jumiya kila siku kwa maana hujuwi lini litazungumzwa lipi ambalo litakufaa wewe wapi hasa baada ya maisha ya shule. Epuka kufanya substitution ya muda wa Mungu  na vitu vingine kama chakula, stress nakadhalika.

Mifano yenye undugu na uvivu hatari:
  • Kama ni muda wa kuanza kipindi cha dini, na wewe ndio upo kwenye foleni ya chakula na roho haikuumi kabisa, ujue kuna changamoto.
  • Kama akikukwaza mtu fulani hasa yule ambaye unadhani ndio muhimu kuliko kitu chochote, basi unafunga vyote including mambo ya Mungu, except chakula tu, ujue kuna changamoto.
  • Kama uko addicted  na kitu fulani mbacho ndio starehe yako eg mpira, movie etc na kama ndio unatazama muda wa kipindi cha dini na kuona bora uendelee kutazama, ujue kuna shida somewhere.
  • Hata kama umetoka kipindi cha mwisho darasani saa 1:20 au hata saa 1:30 jioni na kuna nafsi inakuambia ‘umechelewa sana, dakika 15 hazitoshi kwenda hadi dini, bora tu utembee taratibu, ukale upumzike’ , hiyo faraja siyo ya Kimungu.
  • Au ukisikia wimbo wa Roho Mtakatifu unaimbwa, basi unajiambia ‘nimeshachelewa, hakuna sababu ya kwenda sahizi, nitaenda tu kesho’ hapo ni tatizo, ni uvivu huo.
  • Mtu mvivu anateemea mijiza tu bila imani na mapendo, anawaza habari za kuambiwa ;POKEA MUUJIZA WAKO, WALE KUKU WAKO WATAANZA KUZALIANA KWA FUJO HADI BANDA LISITOSHE, Unajibu Aminaaaaa , wakati kuku wenyewe unawapa chakula mara moja kwa wiki, kila siku wanaumwa new castle . Hapo hata akisema KUKU WAKO WATAANZA KUTAGA MAYAI MATATU KWA SIKU ,’ Na wewe unajibu Aminaaaa. Huo ni uvivu wa kufikilia.
  • Ref, : Baba na mama walikuwa na ugomvi kwenye familia, na wakaenda kwa mtu anajiita nabii na mtumishi wa Mungu. Lengo wapokee muujiza wao wa shetani anayesumbua familia yao. Jamaa akawaambia kuwa Roho wa Bwana anamshuhudia kuwa mama ni mshirikina, kumbe mama hata hana lolote masikini,familia ikaanza kuvurugika hadi walipoenda kwa padre kusuluhisha. Tena baba ni msomi mweye PhD , nikawa najiuliza hii sio academic PhD, labda ni  PH ya soil inayokaribia acidity. Yote haya ni matokeo ya uvivu wa kufikilia na kutaka matokeo ambayo hujayatolea jasho kutafuta.
Tufunguemioyo yetu na kumtukuza Mungu kwa kazi zetu na vipawa alivyotujalia Mungu wetu


NGONO: Ni kujamiana nje ya utaratibu (kabla na nje ya ndoa). Kujamiiana ndani ya ndoa huitwa TENDO LA NDOA. Ni takatifu, halali na linatamkika kirahisi. Pia matokeo yake ni furaha kwa kila mtu, lakini matokeo ya ngono hayapokeleki hata kama mtu ni tajiri na ana kila kitu.
 Katika mazingira ya chuo, mihemko ya kuhusiana kwa pupa ni major consumer wa kuwapoteza utashi watu.  (Watched Hot Friday Movie)

Ninapozungumzia ngono ninalenga michakato yote yennye mlengo huo na mawakala wake. Mifano:
·         Mara ngapi umevaa mavazi ya makwazo na kuwavuta watu kingono. Kwa maana mwingine unaweza kumuamsha hashiki mtu na akaona wwewe hauingiliki, hivyo anagain momentum ya kwenda kumshawishi mwingine aweze kutimiza uovu wake huo.
·         Mara ngapi umekuwa kinara wa kuahidi tu watu kwamba utaolewa/kuwoa? O level, A level, JKT, wiki la registration, unayesali naye, classmate, mnayesoma naye elective course, halafu unaota eti hawana effect, subiri tu utaelewa siku moja.

·         Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza kabla hata test one hujafanya, hiyo UE ndio hata hujui inafananaje, but tayari umesema kuna mtu yupo hoi hajiwezi juu yako. Hapo inatoa picha ya moja kwa moja what is your primary goal. Sijasema kwamba mahusiano mabaya, hapaa, lakini yanahitaji kujipanga, utulivu wa nafsi na mwili yaliyopita kwenye MVUTO, MAWASILIANO na baadaye MAHUSIANO.

·         Mara ngapi umejithaminisha sura yako na kujiona wewe ni bora sana hivyo hakuna atakayekupa shida kwenye mahusiano kutokana na uzuri wako hasa kwa wasichana  (kioo hakidanganyi). Lakini ukweli ni kwamba wewe huwajui wanaume, bali unawajua wavulana tu. The sme kwa wavulana, mostly tunawajua wasichana ambao bado wako kwenye makuzi, na tunajidanganya kuwa ni wanawake.

·         Msichana, once you put your skirt off, everything is off. Ni rahisi sana, mtu akikuona na utulivu ukampotea , akija anaongea hadi anatetemeka , msichana na wewe ndio unaona unamkomeshaaaaa kwa uzuri wako kumbe mwenzako pale akili zake za kawaida hazipo, in such akianza kukusogolea towards your direction, huruma inakuingia, akisema mguu pande, unajibu mguu sawa. Baada ya kukufahamu, Yeye mweyewe tena anakuambia, nyuma geuka, mbele tembea, Kiruuuuuu, unaanza kulalamika mbona harudi, kwani aliona nini that day? Jibu ni kwamba hakuona kitu, coz angekiona kitu angekirudia tena kwa mara nyingine..

JE TUSIINGIE KATIKA MAHUSIANO?
Tuingie tu, lakini uwe kweli ni muda sahihi, mmejiandaa vya kutosha na uhakika wa kupropagate, hii inahusisha mtazamo wa kiimani na kirasilimali. Kumbuka hii ni tofauti na urafiki, kwa maana urafiki hautafutwi na hauna limitation, bali mahusiano hutafutwa na yana limitation. Lakini pia jifunze kuweka mahusiano bila ngono. Tawala mwili wako, vaa mavazi ya staha, jikubali kuwa wewe ni binadamu uliye kamili.

Katika mazingira fulani roomates wana attribute watu tuingie kwenye mahusiano kutokana na huduma ambazo wanazipata kwa hao wanaowaita wapenzi wao, wakati sio wapenzi bali ni wafanya ngono wenzao, eg wakiugua etc. Au simu zao wakiongea na kubembelezana usiku, masikinini wewe tumbo linakuunguruma na kuona kama Mungu kakusahau. Hivi umekosa vipimo vya kupma kazi za Mungu?

KAMA ANALAZIMISHA NGONO, NITAKATAAJE WAKATI NAMPENDA?
Sio kweli, huo ni unafiki. Upendo hauunganishwi na ngono, kuna kitu kimukuscorpion na unajifanya huoni huo uchfu na shimo ambalo mnajichimbia wote wawili hasa msichana.
Tukiambie kizazi chote ukweli kwamba ngono ni adui anayetutenga na MUNGU.
  • ·    Kwanza mwambie wewe sio chombo cha starehe, hivyo mkataba wa ngono unauvunja rasmi.
  • ·    Akiendelea kulazimisha mwambie haupo tayari kuendelea na hayo mahusiano.
  • ·    Punguza mawasiliano na badaye acha kabisa.
  • ·   Utaumia kidogo kwa kipindi cha mwanzo na baada ya muda fulani utagain momentum ya amani. Bora maumivu kidogo ya sasa kuliko maumivu ya kudumu badaye.
  • ·   Usikubali tena kukutana naye sehemu za faragha , anaweza  kukudhuru kwa namna yoyote endapo utakataa kutimiza matakwa yake. Mkikutana msalimie kama kaka/dada.
  • ·    Acha kukurupukia mahusiano mapya mapema, tuliza kichwa fanya mambo ya msingi sana hasa sala na shule. 


VIPI JUU YA UHAKIKA WA MTARAJIWA WANGU KUWA ANAJITUNZA HUKO ALIKO?
Haikuhusu. Wewe heshimu mwili wako, wekeza kwenye sala, Mungu atakulindia huyo ambaye humjuwi, kwa maana kujiliinda kwako ni sala pia. Once ukimpata mkakati wa kwanza wa kuuweka ni kuweka mkataba kuwa NGONO NI ADUI WA MAHUSIANO . Na utamjua siku ya ndoa,  na ukisema basi wewe unaanza taratibu majaribio ya mwili wako kisa una uhakika utamkuta used, basi wewe hautofautiani na wapiga lamli ambao wapo very detailed kuongea mambo ambayo hawawezi kuprove. Hii ni kwasabau hata mchumba wako aliyekutolea posa na mahari anaweza kufa siku moja kabla ya ndoa, na asikuoe, wala hawawezi kusema marehemu kaacha mjane mmoja ambaye alitakiwa kumuoa kesho.

Kwa hayo machache niwatakie kila la heri katika masomo yenu, na Mungu awasaidie sana, nasi tunawaombea san ili mpate wepesi katika masomo yenu. KARIBUNI KWENYE MAHAFALI KESHOKUTWA 25/11. Tumsifu Yesu Kristo. ( 23/11/2016- TMCS SUA NEW HOSTELS)

Eng Herman Nguki wa Malekela (Bsc Irrigation & Water Resources Engineering  2012-16- SUA)

Tembelea www.ngukiherman.blogspot.com mara kwa mara kujisomea mada mbali mbali za vijana, mahusiano na kanisa. Karibu ujifunze.
Thank you for visiting my blog. Click home/ view the web version to see other topics on list ( in case you don't), which have been categorized by months posted. Eg to see the topics posted on October , just click October. You are welcome. Also for Professional information about Agriculture, water resources, soil and environmental conservation visit www.wadcotanzania.blogspot.com  Eng Nguki  

Saturday 12 November 2016

REJESHA TABASAMU LAO, KRISMAS HII

Wahitaji wanakutegemea wewe, jifunze kuhudumia makundi maalumu

Nakumbuka wakati niko mdogo, tena nikiishi katika familia ya kipato cha chini sana, bibi alijitahidi sana wakati wa sikukuu hasa Krismas na Pasaka angalau kupika wali ili majirani wenye uwezo watakavyoanza kunukisha vyakwao basi nisijisikie vibaya, au kuingia kwenye mtego wa kuchoropokea huko, si unajua tena utoto. Lakini ni ukweli usiopingika kwamba pale unapokuwa na uduni fulani au kuishi maisha magumu unaishi kwa hofu na kuona watu wote hawakupendi (defensiveness). Ikitokea mtu fulani kajitolea kukusaidia nawewe ufurahi angalau siku maalumu kama sikukuu, hakika unatenga muda wa ziada kusali kwaajili yake ili afanikiwe zaidi.
Logo ya Jumuiya ya Sant' Egidio

CHRISTMAS LUNCH NI NINI?
Chama cha kitume cha Sant' Egidio kilicho chini ya Kanisa Katoliki kinawaita waliobarikiwa kuwa na uwezo kidogo kuliko wenzao ili kujitoa kuwasaidia wahitaji. Ninapozungumzia uwezo sijasema pesa pekee, bali hata kusali kwaajili ya wengine, kujitolea muda kwaajili ya kuwasaidia wengine kwa huduma, faraja na sala. Miongoni mwa misingi au nguzo ya jumuiya hii ni sala na huduma. Kwenye kipengele cha huduma hii inahusisha kwenda kuwatazama wagonjwa majumbani au hospitalini, kuwatazama wafungwa na wakimbizi. Unaenda kusali nao na kama una zawadi yoyote bila kujali ni ndogo kiasi gani, kwa maana Mungu aliyekuwezesha kuvipata anajua vyema kuliko wanadamu wanaokutazama kwa nje. 

Kwaajili hiyo chama hiki cha kitume huandaa chakula cha mchana kila tarehe 25 Desemba na kuwalisha makundi ya wahitaji mahali pale walipo, kuwapa zawadi na kufurahi pamoja nao. Makundi haya huhusisha watoto ytima, wazee, walemavu na watindiwa ubongo. Mfano kwa chuo kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) wao huwakusanya wahitaji kutoka nyumba ya wazee na wasiojiweza Fungafunga, vituo vya watoto wenye ulemavu wa mwili na akili Mehayo na Amani, Kituo cha watoto cha Rosalia wa Sowano nakadhalika.
Ninaposema wahitaji wote ieleweke ni WOTE bila kujali dini wanazotoka wala kituo kiianzishwa na watu gani.



Upendo wa Mungu hudhihirika katika nyuso za wahitaji pale wanapokumbatiwa na kuambiwa wanapendwa na wana nafasi ya kuendelea kuishi. Ikumbukwe huduma ya namna hii sio ya kikundi fulani pekee, hapana watu wa dini zote wapo walemavu na wahitaji. vivyo hivyo suala la kujitoa kwa wahitaji halina mipaka.
 Kama unapata shida sana kuelewa suala la Christmas Lunch , tumia simu yako au Computer yako nenda kwenye google na undike CHRISTMAS LUNCH OF SANT' EGIDIO , utaletewa video na maelezo ya jinsi tukio hili linavyofanyika nzhi mbalimbali duniani kwa maana sio Tanzania pekee, na utagundua unachelewa tu kuungana na kundi kubwa la watu linalojichotea neema kwa Mungu kila uchwao kwa kuwasaidia wahitaji.
Wengine hawana miguu wala mikono, hivyo wewe ndio wakuwachukulia chakula na kuwalisha kama ambavyo hapa dada Dorice Stanford anavyofanya katika Christmas Lunch ya jumuiya ya Sua
Viongozi wa jumuiya za wanafunzi wakatoliki vyoni TMCS na jumuiya ya Sant' Egidio wanahangaika kila kona kutafuta michango kila kona ili kuwezesha utoaji wa chakula hiki cha mchana anagalau kila mhitaji apate sahani moja ya chakula siku ya Christmas. Wapo wachache, na hawawezi kufika kila mahali kuhamasisha, ikumbukwe ni wanafunzi na wanabanwa na ratiba za chuo, lakini  uwe mwanafunzi au sio mwanafunzi unaweza kuchangia leo hata kuwalisha wahitaji wawili tu siku hiyo kwa njia rahisi nitakayokwambia leo humu.
Sio Tanzania tu hata Burundi, Malawi na nchi nyinginezo wanajitolea kufanya huduma hii, hata wewe waweza ifanya kama sehemu ya kumshukuru Mungu. Anza leo.
Jumuiya inajitahidi kupandikiza moyo huu wa huruma kuanzia kwa vijana wadogo kabisa ili wakue huku wakitambua kuwa wajibu wa kusaidia wahitaji ni wa lazima kwa kila ambaye Mungu kamuweka hai. Hii itapunguza unyanyasaji na pengo kati ya walio nacho na wasio nacho. Hebu fikiria wewe binafsi ikitokea kuna sherehe fulani muhimu, ukajiandaa vizuri sana na kusafisha viatu vyako kisha kuviweka nje vikauke vizuri. Dakika chache kabla ya shamrashamra kuanza unagundua viatu vyaki nje vimeibwa na hauna viatu vingine, hivyo utalazimika kuvaa malapa au ubaki ndani umejifungia kwa maana wenzako wote wameulamba vizuri nje huko. Yote tisa, la kumi anatokea mtu anaviatu jozi mbili au tatu, na unamuangalia kwa jicho la huruma lakini hakuelewi, unamwambia shida yako, lakini anakuambia hivi vingine atavivaa wiki ijayo hivyo hawezi kumgawia mtu. Sijuwi utawaza nini au utajisikiaje
Uwe sauti yao. Uwezo unao. kidogo ulichonacho gawana na wahitaji.
JE UNGEPENDA KUUNGANA NA MAMIA YA WATU KUCHANGIA CHRISTMAS LUNCH YA MWAKA 2016?

Nirahisi sana. Mchango wako wa kiasi chochote utakaotoa utafanya mambo yafuatayo:

  1. Usafiri kwenda na kurudi kuwachukua wahitaji kutoka katika vituo vyao na kuwaleta eneo moja. Hawa ni wazee, watoto na walemavu kutoka Fungafunga, Mehayo, Amani Center na Kihonda.
  2. Mapambo ya ukumbi.
  3. Chakula na vinywaji kwa wahitaji tajwa hapo juu.
  4.  Zawadi kwa wahitaji ambapo baada ya chakula kila kituo hupewa zawadi kama unga, mchele,  mafuta, maharage na vifaa vya shule kwa watoto wanaosoma.
KUCHANGIA----Tumia mawasiliano hayo hapo juu kuchangia. Kumbuka kuwasiliana na viongozi hao mara baada ya kuchangia hasa kwa walio mbali. Kwa wale walio karibu, kuna wanafunzi wachache wanatembea na fomu za kuchangisha huduma hii, tafadhari changia kwa kadiri Mungu alivyokuwezesha. Pia jitolee sadaka ya muda kufanya usafi, maandalizi na kwenda ukumbini siku hiyo 25/12 mara baada ya misa ili usaidie kuwahudumia wahitaji wakati wa chakula. wahitaji ni wengi hivyo watu wa kuwasaidia pia wanatakiwa kuwa wengi. Waweza wasiliana hata na mimi nitakupa maelezo zaidi na kukuunganisha nao.
Mungu wa mbinguni anatambua uwezo wako kuwa ni mdogo, na anakuhitaji ujitoe kwa pale utakapoweza. Jitoe tafadhari. Nakutakia tafakari njema kwa hayo machache niliyokushirikisha, naamini utaungana nami kuhakikisha hili linawezekana. Waweza kumhudumia hata mzee au mlemavu mmoja tu au familia fulani isiyojiweza hapo karibu na kwenu. Sasa usikubali shetani akupige mtama ukaanza kusingizia eti hakuna wahitaji karibu na kwenu, hapo utakuwa unamtukuza ibilisi ambaye ni baba wa uongo.
Uwezo unao, fanya mabadiliko kwa jamii inayokuzunguka, iaminishe kuwa maisha mazuri ni yakujitoa kwa wahitaji ambao watasali kwaajili yako na Mungu atakufungulia milango ya baraka zake. Sant' Egidio huwa hatuhitimu, ni huduma hadi siku ya kufa kwako, ukiishiwa vinavyoshikika, hudumia kwa sala na faraja, utabarikiwa.
Thank you for visiting my blog. Click home/ view the web version to see other topics on list ( in case you don't), which have been categorized by months posted. You are welcome. Also for Professional information about Agriculture, water resources,soil and environmental conservation visit www.wadcotanzania.blogspot.com  
Eng Nguki wa Malekela. O763639101/0679639101/ ngukiherman@ymail.com 

Saturday 5 November 2016

POTELEA MBALI, MIMI SIO WA KWANZA

Halahala mti na jicho

Potelea mbali, ndio, potelea mbali. Wapi huko? Sijuwi hata mimi.
Naam. habari ya wakati huu ndugu yangu, Siku moja mama mmoja akaniomba niongee na binti yake wa miaka 18 ambaye yuko kidato ch tano kwa maana anaona tabia zake zimeanza kuwa ndivyo sivyo na yeye anajitahidi kuongea naye lakini haoni mabadiliko. Huyooooooooooo hadi nyumbani kwaao. Nikakaa mahali pa utulivu kabisa na kuanza kupiga stori. Nikaanza na utani mwingi na comedy ndani yake huku nikitaka kujua mwanzo wa hizi sarakasi, anapenda nini, hapendi nini n.k.

NILIYOYAPATA
Miaka miwili iliyopita dada yake ambae yupo chuo kikuu alikwa hapa nyumbani na alishakuwa na mahusiano na wanaume wa kuhusiana naye huko chuoni na pia hapa nyumbani. Dada alikuwa anaongea kwenye simu na hawa wanaume kwa nyakati tofauti bila kuwachanganya. Dada alikuwa akimsimulia waziwazi anavyofarijiwa na kupewa anavyohitaji kwa wanaume hawa. Muda mwingi alikuwa akisoma message za watsapp na hizi za kawaida au kuongea na simu, basi alitabasamu na kumpa mshawasha mdogo wake kujua kulikoni, ambapo dada jibu lake lilikuwa 'mdogo wangu kuwa utayakuta, it is more than sweet'. Wakati mwingine alikuwa anamuuliza dada yake 'sasa muda wa kuolewa atafanyeje na haoni kama anamkosea huyo mme atakayekuja kumuoa'. Dada alikuwa akiangua kicheko na kumuambia ataelewa mara muda wa kuonja ukifika,kwa maana wanaume wote wanafanya ngono sana tu, tena wao huwa hawagunduliki hivyo hutumia hiyo nafasi kufanya uchafu  mwingi, hivyo kwa msichana anayejidanganya eti hafanyi ngono kwa kuwa ataolewa na mvulana ambaye hajawahi kufanya ngono anajidanganya, vinginevyo ajiumbie huyo mwanaume mwenyewe ni bora tu afanye, but awe makini sana kusiwe na madhara, kama mimba na ukimwi. Na ikitokea bahati mbaya kapata kati ya hivyo au vyote, POTELEA MBALI KWA MAANA MATATIZO YAPO KWA AJILI YA WATU NA YEYE HATA KUWA MTU WA KWANZA KUYAPATA HAYO, BADO MAISHA YANAENDELEA KWA MAMIA YA WATU AMBAO WALIFURAHIA MAPENZI. Tena kuna watu walijifanya kuwabania wavulana wanaowapenda eti hawataki kufanya mapenzi, lakini mwisho wa siku wakaja kuolewa na mijanadume milevi na mihuni isiyojari na pengine ukaenjoy kwa muda mfupi tu na kufa kwa presha au magonjwa. Bora nini sasa? Ni bora tu kufurahia maisha yamapenzi, na pia akamwambia ukishaanza sio rahisi kuacha. 

Hivyo na yeye mwaka jana wavulana walianza kumtongoza wengi kama nyuki, kwanza aliona ni usumbufu ulioibuka ghafla, na bora amkubali mmoja ili kupunguza usumbufu kwa wengine, ikawa hivyo, akaendelea na kwa kuwa aliambiwa akianza hawezi kuacha, hivyo hata alipoenda rikizo kwa bibi yake akitongozwa alijitahidi angalau kumkubalia mmoja ili mambo yaende, na hadi sasa wanagombana na mama yake kwakuwa anambana sana na kutompa muda wa kuwa huru ili akaonane na mmoja kati ya wapenzi wake. Na naamini kuwa akiacha moyo utaumia sana na pengine mambo mengi hayataenda sawa.

Tuliongea mengi sana, ambayo yalinipa picha kamili ya kilemba cha ukoka alichovalishwa yule binti na dada yake na kujikuta anageuka mtumwa wa ngono na kujidanganya kwa kusema anawapenzi kumbe anawafanya ngono wenzake. Nilimshauri mengi sana na kumuhakikishia kuwa yeye ni binadamu aliyekamili, kuwa na hisia sio dhambi, bali ishara ya ukamilifu, na kamwe sio tiketi ya kufanya ngono, shule na ngono haviendi, sala na ngono haviendi, lazima useme HAPANA yenye kumaanisha hutaki kuwa chombo cha starehe, jiheshimu jisitiri, jitawale, furahia ujana wako kwa kufanya mambo mema.
Ni kweli mtu akifanya ngono hata kuwa mtu wa kwanza, kama kulivyo kufa, mtu akifa sio yeye wa kwanza, swali linakuja Mungu alikuumba ili uje upotee kirahisi hivi jamani? Na wewe msichana aliyekwambia kuwa wavulana wote wanafanya ngono ni nani? hizo takwimu mwenzetu ulizikusanyia wapi? Bila shaka umeanza na wale ambao wamefanya na wewe, au kwakuwa wengi wamekutongoza basi unajua kilakijiji, kila kata, tarafa. wilaya na mkoa  na nchi nzima wanafanya ngono? Unajidanganya. Wenye akili wamejitoa sadaka kuishinda tamaa ili waje kufurahia katika ndoa? Ishu ya nitaolewa na nani, muachie Mungu aliyekuumba ndiyo anajua ubavu wako uliko na  ndiye aliyeutoa, sasa wewe kilanga chako cha kuvania maubavu ya watu, ukija na ule wa kwako utauweka wapi? Au mbavu nyingine unataka kutengeneza mishikaki ule? Muache Mungu afanye yake kwako, usifanye ngono hadi siku ya ndoa, huwezi kuugua huwezi kuwa chizi, bali utakuwa na nafsi ya kutafakari vizuri namna utakavyofurahia tendo la ndoa ndani ya ndoa. 

Ishu ya kutongozwa na wengi pia ni kawaida tu kwa maana kila mtu anavutia, na wakati mwingine watu wanakujaribu tu, na wewe kichwakichwa unaingia kukaa kwa mashabiki wa Yanga wakati umevaa jezi ya Simba, mimi simo yatakayokukuta huko.Wavulana wenyewe wanatongozwa sasa wewe unshangaa nini? KATAA KWA KINYWA CHAKO DADA. Kwa taarifa yako, maisha ya kujitawala bila kufanya ngono ni sala, kwamba unamuomba Mungu akuletee anayejilea kama wewe. Na ukisema huwezi kuacha basi ni shwangwe na vigeregere kwa shetani kwa maana atakuja mfanyangono sugu ili chuma kinoe chuma., Kama huamini endelea, na UTANIKUMBUKA NGUKI MIMI.

Wakati fulani hata wavulana nimekuwa nikiwasikia bila aibu wanasema wasichana wote wanafanya ngono na kwamba kama haufanyi ngono kwa kudai eti utakuja kuoa msichana ambaye hajawahi kufanya ngono basi ni ndoto za mchana. Labda ujiumbie wewe mwenyewe. Mnaumwa nyinyi wenye hayo mawazo, MBONA MNALIPA KISASI KWA MTU MSIYEMJUA? ni dhambi hiyo. Wewe ni nani ambaye umeshajua utaoa mtu wa aina gani? au ndio sala yako? unadhani kwasababu kila msichana unayemtongoza anakubali tena unamkuta wewe sio wa kwanza basi wote ni hivyo? NI MUNGU TU ANAWAEPUSHA WALIO SAFI ILI USIWACHAFUE WAKUTWE SAFI NA WASAFI WENZAO WAFURAHIE NDOA TAKATIFU. Pole unayezidi kujichafua, hata hivyo una nafasi ya kuanza mfumo mpya wa maisha na ndio maana kuna wengine tendo moja la ngono linawapa matatizo yote na pengine kifo, wewe umebaki mzima kwa maana Mungu alijua kua siku utabadilika tu, huenda ikawa ni leo hii.
Subiri muda ufike, mfunge ndoa na kuvishana pete za ndoa ishara ya ulinzi kutoka kwa mwenzi wako ambapo matokeo ya tendo la  ndoa kila mtu atayapokea kwa furaha.


HATA MIMI NINA HISIA KALI
Ikumbukwe kuwa hatuachi ngono kwaajili tu ya mke au mme mtarajiwa, bali ni kwaajili ya afya yako na ustawi wa maisha yako pia mfumo wa kufikili na kutenda kazi za kawaida za kijamii unakuwa na ufanisi mkubwa sana kwa mtu asiyefanya ngono. Hata mimi Nguki usidhani naandika haya labda mwili wangu umelala, ah, weeee, hisia zipo tu tena kali sana kwa maana nipo kamili kijinsia na kila kitu. Je hiyo ni tiketi kwamba nitafute mtu wa kufanyanaye ngono?, hapana. Huwa nafanya nini sasa mwili ukiwaka????? Sikia
  • Kwanza nafurahi na kumshukuru Mungu kwa maana ni ishara kuwa nitakuwa mtendaji mzuri wa wizara ya mambo ya ndani from the wedding night.honeymoon etc.
  • Ninajiambia kuwa mimi sijaoa bado, na pia kuna mtu anajinyima kwaajili yangu na Mungu kaniandalia.
  • Ninajiambia kuwa hisia hizi atakuja mtu sahihi ,tutahudumiana muda wote sahihi na mazingira sahihi.
  • Ninajiambia kuwa matokeo ya ngono sasa ni fedheha, aibu,  na kuwahuzunisha wazazi, walezi na jamii kwa ujumla.
  • Ninajiambia nataka kuwa baba bora wa familia yangu muda ukifika, ishu ya kwamba mke wangu atakuwaje hayanihusu, Mungu aliyenimba anajua, kazi yangu ni kusali na kufanya uchaguzi sahihi wa kuomba mahusiano,.
  • Ninajiambia pia kuendekeza hisia hizi zikiniendesha na kufanya ngono sasa naweza kujikuta  napata magonjwa ya ajabu ajabu na madhara mengine ambayo yanawezaa kuniua, hata kama nitasema potelea mbali mimi sio wa kwanza.
  • Kwa kifupi sigombani na mwili wangu kwa maana mimi ndiyo mwenye hatimiliki ya mwili wangu na mtoa maamuzi, hivyo nauambia huna chako kwa sasa, hadi siku ya ndoa.
  • Nabaadilisha mazingira niliyokuwepo kwa wakati huo, najiweka busy kusoma vitabu na mambo mengine mengi ya kijamii na kidini hivyo kuhamisha kabisa mawazo, na pengine namuuliza mama kama kuna vitu vya kufuata sokoni ili niende kuvinunua na kubadilisha mazingira..
Tena hata sio lazima yote yafanyike kwa pamoja, mwili unapoa wenyewe nakuhakikishia. Kwa mtu aliyezoea ngono anashangaa kuwa labda nasema nadharia, badilika, vinginevyo unajichimbia shimo la kukufukia mwenyewe na kizazi chako, kwani mdogo wako hasa wa kike akiwa anafanya ngono na limwanaume fulani barabarani huko unachekelea na kumpongeza? na binti yako je? Badilika sasa, kwa wa mfano. Hata wanaokuona wewe ni mhuni wanaweza kuanza kukuheshimu na kukupa nafasi ya kukuamini, na Mungu atawaaminisha kuwa wewe sio yule wa zamani. Anza leo kuamini kuwa wewe ni wa muhimu sana na you will have a wonderful moment with your wife/husband in the marriage. Usiseme Potelea mbali, utapotea wewe mwenyewe na kizazi chako,wala sio mtu mwingine.
NAKUTAKIA TAFAKARI NJEMA. Kama una swali usisite kuniuliza hapo chini, au kama unataka ushauri binafsi, nitafute kwa simu au email, watsaap nipo kwa hiyo number ya voda.


Eng Herman Nguki wa Malekela
0763639101/0679639101
ngukiherman@ymail.com
UCE Tanzania Volunteer.
Thank you for visiting my blog. Click home/ view the web version to see other topics on list ( in case you don't), which have been categorized by months posted. You are welcome. Also for Professional information about Agriculture, water resources, soil and environmental conservation visit www.wadcotanzania.blogspot.com  Eng Nguki

Wednesday 2 November 2016

Nampataje Mchumba Mwema?-Dr Godbless Nicetus Massawe

Mshirikishe Mungu katika kuanza mipago ya kuingia  kwenye mahusiano, utafurahi daima

SEMINA: KANUNI SABA ZA KUMTAMBUA MCHUMBA ANAYETOKA KWA MUNGU

MAANA YA MCHUMBA
Mchumba ni mvulana au msichana ambaye ameweka ahadi ya kuoa au kuolewa baada ya kipindi Fulani.Ili uchumba uwepo lazima yawepo makubaliano baina ya watu wawili mvulana na msichana

HATUA ZA UCHUMBA
Ili uchumba utambulike rasmi ni unatakiwa kupitia hatua zifuatazo:-

(A)URAFIKI
Urafiki si uchumba bali unaweza kuzaa uchumba wapo waliokuwa marafiki baada ya kutakiana uchumba na wapo walokuwa marafiki wa kawaida lakini baadaye wakaamua kuwa wachumba.ni kawaida mtu kuwa na marafiki wengi lakini mchumba ni mmja tu sifa za mchumba ni tofauti sana na sifa za rafiki Marafiki wa jinsia tofauti ni lazima wajue nini kusudi la urafiki wao mfano wa makusudi ya urafiki ni
 BIASHARA
 MASOMO
 MAOMBI

(B)TAARIFA KWA WAZAZI
Hii ni hatua ya pili ana ya juu sana katika marafiki wa uchumba kumbuka kuwa marafiki wa uchumba si wachumba mpaka hapo taratibu zote zitakapokamilika .Ni hatari sana kuwapa taaarifa wazazi bila ya kuwa na hakika ya kuoana au kabla ya kufanya uchunguzi wa kutosha kuwa huyu ndiye chaguo sahihi toka kwa Mungu.kiafrika ukimchagua mtu umechagua familia na ukoo wake na kabila pia kuna ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu watu walimpenda mtu na si familia na ukoo pia .kiafrika ukoo unaweza kukataa au kumkubali mtu hivyo mwombe Mungu kwani hakuna linaloshindikana kwake.Baada ya wazazi kukubaliana ndipo taratibu nyingine hutolewa kama mahari hapa uchumba huanza kuhusisha familia mbili na kuingia kwenye uchumba

(C)MAHARI
Ni kitu au vitu ambavyo wazazi wamekubaliana kitolewe kwaajili ya binti yao japo kuna makabila ambayo mahari hutolewa na mwanamke hayo ni makubaliano tu na ni taratibu za watu ambazo ni nzuri kadiri yao.Mahari ni jambo la kibiblia Mw 29:18-26 hivyo haina sabab ya kuipinga bali utu wa mtu utazamwe .Baada ya mahari uchumba hukamilika na ndipo pete ya uchumba huvalishwa,yafuatayo ni maneno ya kusema wakati wa kuvishana pete ya uchumba
”FULANI……..NAKUVISHA PETE HII KUONESHA NA KUTANGAZA HADHARANI KWAMBA NAKUPENDA,TENA NAKUAHIDI KUWA UTAKUWA MKE WANGU WA MAISHA SIKU ZA KARIBUNI,KILA UNAPOIONA PETE HII UKUMBUKE AHADI YETU,BWANA YESU TUNAKUOMBA UTUSAIDIE TUWE WAAMINIFU.”

TOFAUTI YA MAHARI NA POSA
Mahari ni kitu au vitu ambavyo hutolewa na mwanamme kwa wazazi wa mwanamke kwa makubaliano ya kuoana watoto wao, hii hutolewa mbele ya mashahidi wa familia zote mbili ,mahari si lazima iwe pesa inategemeana na makubaliano ya wazazi.Kwa wakristo kuweni makini kwa maana kuna baadhi ya taratibu za mahari huambatana na ibada kwa mizimu hii ni hatari kwa mstakabali wa wanandoa watarajiwa,
POSA hii huitwa pia kishika uchumba hiki ni kitu chochote kinachotolewa na kijana anayetaka kuoa kwenda kwa wazazi wa msichana chenye thamani yoyote.Posa haina majadiliano yaweza kuwa kukuk,mbuzi ,njiwa nk,kwa baadhi ya makabila wanapotaka kuoa hupeleka barua kwa wazazi wa mwanamke na kueleza nia yao ya kutaka kuoa na kuweka kiasi Fulani cha pesa barua hiyo husomwa kisha binti huulizwa kama anajua lolote juu ya kijana huyo anapokubali ndipo utarartibu wa kupanga mahari hufanyika.Baada ya uchumba kuvunjika mahari inaweza kurudi kutegemeana na kabila na makubaliano lakini posa hairudi
(D)KUTANGAZA KANISANI
Baada ya makubalian ya wazazi watoto waoane wachumba watakwenda kwa uongozi wa kanisa kuwaeleza japo ni vema kuwashirikisha viongozi wa kiroho mapema zaidi kabla hata ya mahari. Ushauri kutoka kwa watu wafuatao ni muhimu kwa wachumba kabla ya kuoana
 Mtu aliyekomaa katika maisha ya kiroho ,aliyetulia katika Roho mt
 Mtu asiye mmbea
 Mtu aliyedumu katika ndoa sio chini ya miaka 5-10 mwenye uzoefu ktk familia
 Awe katika familia isiyo na migogoro
Ni vema wakati wa kutangaza kanisani taratibu zote ziwe zimekamilika hata tarehe yaa ndoa

UMRI WA KUPATA MCHUMBA
Hili ni jambolinalowatatiza wengi hata wengine hujikuta wakichukua uamuzi usio sahihi kwa kudhani wanachelewa kuoa au kuolewa,. Mara nyingine wazazi marafiki na ndugu wamekuwa wakiwatia pressure vijana wkisema utaoa lini wewe? Kumbuka hatuongozwi kwa msukumo bali ROHO MT Yoh16:13; Rum 8:14 MH 3:1
Kiafya umri mzuri kwa msichana kuolewa ni miaka 20-30 umri huu msichana atajifungua pasi na hatari kubwa za uzazi umri mkubwa una matatizo mengi ya uzazi
Kwa upande wa wanaume miaka 25-40 kwa sababu katika umri huu kijana anaweza kutimiza majukumu yake kama baba
Pamoja na hayo yote umri sahii ni pale majira ya Bwana yanapotimia Is 49:8.watu wasikutishe waambie majira ya bwana hayajatimia.

KANUNI ZA KUMTAMBUA MCHUMBA ALIYETOKA KWA BWANA NA AMBAYE SIYE
Tangu mwanzo Adamu hakutafuta mke bali Mungu ndiye aliyemtafutia Mw 2:21-23 Biblia inasema mke mwema mtu hupewa na Bwana Haisemi mtu akatafute maana anayemwandalia mtu mke au mume ni Mungu na sio watu Mith 19:14
Hata hivyo suala la kufahamu huyu anatoka kwa Bwana ni kitendawili maaana vijana wengi tunaangaika sana Mungu hawezi kutuachia mtihani ambao tutafeli ila ni kwa kutojua tu kanuni tumejikuta tunaangukia kwenye mitego mibaya na kujutia maisha ya ndoa .Na wengine wapo kwenye uchumba huku wakiwa na wasiwasi kama huyo aliye naye ndiye au la .

Zifuatazo ni kanuni zitakazo kusaidia:-

(1)TAFUTA KWANZA UFALME WA MUNGU NA SIO MKE AU MUME
MT 6:33 Mungu anasema tuutafute kwanza ufalme wake na maengine yote akiwamo mke au mume tutapewa kwa ziada ,ndani ya ufalme wa Mungu ndipo kuna mke na mume bora MITH 19:14 ufalme wa mungu unapatikana kwa sala na maombi kwa kuambatana na matendo mema yaani kutimiza mapenzi ya Mungu. Mungu alipoona utendaji wa Adamu aliridhika akasema”Si vema mtu huyu awe peke yake ” Mw 2:18 ADAMU HAKUSEMA SI VEMA NIKAE PEKEYANGU. Dhambi zinatutenga na uso wa MUNGU NA TUKIWA KATIKA DHAMBI HATUPO KATIKA UFALME WA MUNGU ,Mke au mume mwema hapatikani nje ya ufalme wa Mungu IS 59:1-2 Jiulize kwa siku unasali mara ngapi unaomba mara ngapi kasha utajua unautafuta ufalme wa Mungu au la.

(2)UWE NA MACHO YA ROHONI
Mungu ni ROHO Yoh 4:24 hivyo huonekana kwa macho ya roho, kutumia macho ya roho ni kuangalia Mungu anasema nini na kutofuata watu wanasema nini.Kwa Mungu hakuna neon lisilowezekana Luk1:37. Tusiangalie mambo katika mtizamo wa kidunia mf Sara alitazama kidunia ndio maana hakuamini MUNGU ALIPOSEMA ATAPATA MTOTO Mw 18:6-12 .Zakariia hali kadhalika Luk 1:8-25 Hakika kwa Mungu yote yanawekana MT 7:7-9

(3)UJUE SAUTI YA MUNGU
Manabii na makuhani waliweza kusikia sauti ya Mungu Kut3:1-10,Yer 3:6,11 .mtume Paulo katika Mdo16:17 anakatazwa na Roho mt je alijuaje? Samueli pia alipata shida kujua sauti ya Mungu 1Sam 3:1-10 Ili ujue sauti ya Mungu ni lazima rohoni mwako lijae neno la MUNGU, ukikaa ndani ya Mungu na maneno ya Mungu yakikaa ndani yako omba chochote nawe utakipata Yoh15:7 Mungu anapotaka kusema na mtu anasema na roho yake, neno la Mungu ndani yetu ndilo litakalotuwezesha kusikia sauti yake.Zifuatazo ni njia ambazo Mungu hutumia kufikisha ujumbe kwa watumishi wake:-
 NENO LAKE
 MAONO
 NDOTO
 MAFUNUO
 WAJUMBE
 MAWAZO YAKO
 SAUTI NK
Tahadhari hata shetani au nafsi hutumia njia hizo pia,ili kujua hilo unapaswa kuwa mtu wa maombi na sala mara nyingi na kujitahidi kuishi maisha matakatifu.ili usikie sauti ya Mungu unapaswa uwe katika roho.Vijana wengi wameumizana na kuleteana madhara kwa maana walisikiliza nafsi zao wakidhani ni sauti ya Mungu
Ukiingia katika mahusiano kichwakichwa, kwa jeuri ya pesa au uzuri wako wa nje, utaelewa  vizuri kwanini Simba na Yanga wanaombeana njaa kila kukicha. Utajuta.


(4)ZIJUE SHERIA ZA NAFSI
Mungu alimuumba mtu katika utatu usiogawanyika akiwa hai yaani mwili,roho na nafsi MW1:26-27 Mungu aliumba roho maana MUNGU ni Roho ,MW1:1,Yoh4:24.mwili uliumbwa katika MW2:7 na pumzi ya MUNGU IKAMFANYA MTU NAFSI HAI MW 2:7B Nafsi ina nguvu sana na mara nyingi tunaongozwa na nafsi tukidhani ni Mungu Vijana wengi huongozwa na nafsi wakati wa uchumba wakidhani ni MUNGU.Mungu anaposema na watu husema na roho zao na sio nafsi RUM8:16 .

ZIFUATAZO NI SHERIA ZA NAFSI:-

SHERIA YA KWANZA
KILA KITU KIZURI NAFSI INA TAKA KUKIMILIKI
(Mf wa noti mbili za 5000/=)Yesu anasema ukitaka kumfuata ikane nafsi yako Mt16:24 kumpenda mtu mara nyingine si kibali cha kuoana wala si kwamba utamjua mchumba kwa kumpenda tu.Kumbuka hata wasiomjua MUNGU wanapendana kwa sababu wana nafsi.Upendo wa kweli ni lazima uletwe na ROHO MT GAL5:22.Nafsi nayo inapenda hivyo mchumba anayetoka kwa BWANA ni Zaidi ya kumpenda.

SHERIA YA PILI
NAFSI HUTOA MAFUNUO
Biblia inasema yamtokayo mtu ndiyo yanaujaza moyo wake hii ni sawa na kusema kuwa yamtokayo mtu ndiyo yaliyoijaza nafsi yake .Mf umegombana na mtu mchana usiku ukiwa peke yako umelala ugomvi unajirudia na unaweza kuona yule mtu anakuja na mnagombana tena.Nafsi ina tabia ya kudaka na kuhifadhi na kisha kutoa hivyo kama mtu anasikia mambo mabaya nafsi yake itayahifadhi na baadaye kuyatoa ,linganisha watoto wanaotoka katika familia zinazosali na wale wanaotoka katika familia zenye magomvi.Hali kadhalika kwa vijana unapomuona msichana au mvulana halafu ukampenda unapokuwa nyumbani nafsi yako inakuletea mtu huyo ili ajadiliwe na akili pamoja na mwili ,mjadala unaanza huyu anafaa sababu ni msomi kama mimi ,kabila langu,ni mzuri mpole nk.wakati huo pia mwili unakuwa mdau mkubwa akili na nafsi zinamwonesha mwili alivyo na maumbile mazuri ghafla mwili unaanza kudai haki yake hapo ndipo kijana anasema nimeona maono.Hayo ni maoni ya nafsi na si maono ya Roho mt.Ili kuyashinda hayo neon la Mungu lazima likae kwa wingi ndani yako KOL3:16.Mwili na nafsi vikiungana kumpenda mtu huwa ni hatari sana katika maisha ya kiroho mtu mtu haombi tena hasali na huondoa hofu ya Mungu na ni muda wa hatari mtu huanguka kiroho.Ukiona umepata mchumba halafu maisha yako kiroho yanadidimia ujue huyo si wa kutoka kwa Mungu.

SHERIA YA TATU
NAFSI NI KIGEUGEU NA HAINA MSIMAMO
Mtume Paulo anasema kuna jambo hataki kulifanya lakini hujikuta anafanya RUM 7:16-19 Nafsi inapokumbana na jambo zito hugeuka, YUSUPH alipojua Maria ana mimba nafsi yake iligeuka na kuamua kumwacha Mungu asingeingilia kati Maria angekuwa ameshaachwa Mt 2:19 -20 Ukiongozwa na nafsi kila msichana ukimwona utamwambia nataka kukuoa.

SHERIA YA NNE
NAFSI HUKINAISHWA
Kwa kawaida nafsi ya mtu kabla haijakipata kitu huwa na shauku kubwa sana na ikishakipata huwa inakinaishwa nacho na kutamani kingine kipya au kizuri Zaidi.mf simu.Pia ukioa au kuolewa kwa msukumo wa nafsi ukikinaishwa na mwenzako unadhani nini kitafuata? Roho wa Bwana anapokupa mwenza hutakinaishwa naye kwa maana anakuja na upako wa Mungu na matunda ya Roho mt mf Ibrahimu aliishi na Sara mpaka uzeeni japokuwa Sara alikuwa tasa.Adamu aliishi na Eva kwa miaka 900

SHERIA YA TANO
NAFSI INAWEZA KUPINGANA NA MAPENZI YA MUNGU
Hebu tazama Yesu katika mafundisho yake alisema yampasa kufa kwaajili ya watu lakini muda ulipofika alisema baba ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke nafsi ilikuwa inapingana na mpango wa Mungu MT26:38-39 Lakini alipogundua kuwa anapingana na mpango wa Mungu akasema si kama nitakavyo mimi bali mapenzi yako yatimie.mf wa MARIAM LK1:38 hata Sara pia Mw18:9-15

SHERIA YA SITA
NAFSI HAINA IMANI
Kuna uwekano Mungu ameongea na wewe lakini nafsi inakataa kuamini Mdo 12:5-14 wakristo waliomba Petro aachiwe aliachiwa wanakosa Imani.Pia Yoh11:20-27.Kumbuka usiangalie watu wanasemaje bali angalia Mungu anasemaje?
Mungu asipohusika, utajikuta unasema uko sawa wakati unavuja chozi usiku na mchana.

SHERIA YA SABA
NAFSI HUCHUKIA NA KUFURAHI
Nafsi inaweza kukufanya umchukie uliyeletewa na Mungu na kwa sababu haijaridhika naye kwa vigezo vya kimwili.Kumbuka Mungu anapomleta mtu kabla ya kuisikiliza nafsi yako msikilize kwanza yeye MUNGU hakulazimishi wewe umpende mtu huyo bali akikuletea mtu hata kama ulikuwa humpendi atatoa kibali kwenye nafsi yako umpende.kumbuka sio kila maombi yanapata majibu kutoka kwa Mungu majibu mengine yanatoka kwa nafsi.Nafsi inapenda sana kusifiwa naikitokea kila siku mtu ankuambia wewe ni mzuri maneno haya yakirudiwa mara kwa mara nafsi huyapokea na kuyapenda.Mtu akikusifia usirembue macho bali mpe sifa Mungu

SHERIA YA NANE
NAFSI INAJUA KUPENDA
Rej Mark 12:30-31 nafsi hupenda kwa sababu, na kitu inachokipenda kikitoweka upendo huisha pia KAMA UNA MCHUMBA JIULIZE kitu gani kinakufanya umpende na je kikiondoka upendo bado utakuwepo

(5)Usimkubali bali mchunguze
Wapenzi neno la Mungu linasema msizikubali kila roho bali mzipime 1 Yoh4:1-2 Mtu akikufuata utampima kwa kuangalia sheria za nafsi utajua kama anaongozwa na Roho au nafsi.Pia fanya maombi muulize Roho kama huyo mtu anatoka kwake na kama sivyo kemea ashindwe kwa jina la Yesu na ,Na wakati unaomba kibali cha Roho mt usimshirikishe omba peke yako

(6)Jiulize maswali yafuatayo na uyapatie majibu
Swala la kuoa na kuolewa ni agano na si mkataba uchumba ni mkataba lakini ndoa ni agano :-
1. Je atakuwa msaada wa kiroho kwangu? Kusudi kuu la Mungu kila mtu aingie mbinguni Ez18:23-24,Yoh 3:16, kuna watu wamekufa kiroho baada ya kuoa na kuolewa .angalia Mke si msaidizi wa kuosha vyombo nk ni msaidizi wa kufika mbinguni.Delila hakuwa msaada wa kiroho kwa Samson Waamuzi16:4-22

2. Je Imani yetu inafanana? Tofauti ya kiimani huathiri ndoa na maisha ya watoto kiujumla tofauti ya kiimani huweza kuleta migogro baina ya familia Malezi kwa watoto yatayumba tu. Mf 1falme19:1-3 ,Mith 22:6

3. Je maongezi yake yanamwinua Kristo? Kumbuka ukitaka kujua tabia ya mtu angalia rafiki zake na maongezi yake .Yale anayoongea ndiyo yanaujaza moyo wake. Moyo ulio na kristo utaongea habari za Kristo na moyo wa shetani utaongea uzinzi na umbea

4. Je ni msaidizi kweli? Mw 2:18 usaidizi si wa kazi wakati wa Adamu hakukuwa na sahani na masufuria wala mashamba ya kulima usidizi ni wa kiroho.Msaidizi wako mtafanana kimawazo.

5. Je amezama katika Kristo? Kuzama katika Krsto si kufanya huduma za kanisa pekeyake bali ni kuishi kadiri impasavyo mkristo

6. Je mawazo yenu yanafanana? Ikiwa mawazo hajafanana ni rahisi sana kutokea ugomvi ,mfano mume anapenda aina Fulani ya watoto na mwanamke vilevile

7. Je unapoongea naye unakua kiroho? Je unapokuwa naye unapata hamu ya kusoma neon la Mungu?

(7) Angalia mazingira mliyokutana, je ni kanisani? bar? disco? Au kwenye kwaya au kikundi cha sala? Je kama umempenda sababu anaimba vizuri siku akiacha kuimba itakuwaje? Ujue unaoa mtu na sio kipaji Mf wa dada aliyepooza baada ya ajali.Hakuna kitakachotutenga na upendo wa Kristo Rum8:35-39

MAISHA YA UCHUMBA
MAMBO YA KUZINGATIA ILI KUKWEPA VISHAWISHI WAKATI WA UCHUMBA
 Zawadi zenye hisia za mapenzi
 Kuagalia picha za mapenzi
 Epuka mazingira ya hatari
 Epuka maongezi yanayochochea mapenzi
 Epuka kushikanashikana
Zawadi zisitumike kama mtego wa kupelekana katika vishawishi. Zimetumika sana kuwavalisha miwani ya kuona karibu wakati tunatakiwa kuona mbali. Waichana baadhi wamejikuta wakitoa zawadi  ya ngono ili kulipa fadhira za wavulana wao.


JINSI YA KUISHI MAISHA MATAKATIFU YA UCHUMBA
 Kaeni eneo la wazi
 Kila mnapokutana fanyeni maombi
 Mkikutana someni neno la Mungu
 Peaneni ujumbe wa neneo la Mungu na sio mapenzi
 Pangeni mipango ya maisha yajayo
 Jadilini suala la kazi
 Jadilini suala la watoto
 Msishirikiane kimwili kabla ya ndoa

MAMBO MUHIMUYA KUJUA KABLA YA KUOA NA KUOLEWA
 Mfumo wa maisha yako utabadilika
 Marafiki watabadilika
 Maumbile yatabadilika
 Majukumu yataongezeka
 Jiandae kuwa kiongozi

USHAURI
 Usioe au kuolewa sababu ya kuiga
 Jiandae kabla ya kuoa na kuolewa
 Usifanye haraka kuoa au kuolewa
 Usioe wala kuolewa kwa( kulazimishwa
 Kaa na Mungu vizuri


MWENYEZI MUNGU AKUSAIDIE UUTAMBUE WITO WAKO NA AUPALILIE ILI UWEZE KUUFIKIA MUNGU AWABARIKI NA NAWAPENDA SANA
REFERENCE
1. HOLY BIBLE
2. Mwl Joseph Urio
@
Dr Godbless Emeritha Nicetus Massawe
Bachelor of Veterinary Medicine 2011-2016
0752684380
AD MAJOREM DEI GLORIUM (For the greater glory of God)

Edited by  Eng Herman Nguki wa Malekela.
www.ngukiherman.blogspot.com
0763639101/0679639101
Thank you very much for visiting my blog. In case you don't see other topics, just click home/ view the web version, it will display the home page and topics list which have been categorized by months posted. You are welcome. Share and comment, questions will be answered. Eng Nguki