I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Wednesday 23 November 2016

SIO RAHISI HATA KIDOGO.

Mungu yuko upande wetu. Tujibidiishe kusali na kufanya kazi.

Tumsifu Yesu Kristu.
Namshukuru Mungu paoja nanyi kwa neema ambazo anatujalia kila siku ingawa hatustahili. Maovu yetu mara kadhaa yametutenga mbali na Mungu na kutusogeza kubaya ambako haukuwa mpango wa Mungu Zaburi  103:12 Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi
Ni kweli, tumefanya maovu na lazima tukiri wazi kwa vinywa vyetu
Zaburi 106:6 Tumetenda dhambi pamoja na baba zetu, Tumetenda maovu, tumefanya ubaya.
Isaiah 59:12 Maana makosa yetu yamezidi kuwa mengi mbele zako, na dhambi zetu zashuhudia juu yetu; maana makosa yetu tunayo pamoja nasi, na maovu yetu tumeyajua;
Jeremiah 14:20 Ee Bwana, tunakiri uovu wetu, na ubaya wa baba zetu; maana tumekutenda dhambi..
Mara nyingi nikiwa nasoma chuoni, wakija wanafunzi ambao walishamaliza walikuwa wanatutia moyo kwa kutuambia shule sio ngumu mtafaulu tu. Ni kweli nen hili ni muhimu na la faraja kwa wanafunzi wanaoendelea. Mimi pia nimemaliza hapa chuoni, lakini niwaambie tu bila kuumauma maneno, shule ni ngumu, ten asana tu Ndio shule sio rahisi hata kidogo. Kwa sentensi hii sina maana kwamba huwezi kumaliza au kufaulu vizuri, bali juhudi za makusudi na kujitoa sadaka ya muda lazima viwepo kwa nguvu zote.

NINI KINAFANYA CHUO/SHULE WAKATI FULANI KUWA NGUMU KUPITA KAWAIDA
Kwa ambao wamewahi kutumia computer:, ikitokea unahamisha vitu vingi  kutoka kwenye flash disk kwenda kwenye computer au kinyume chake, utaona computer inaandika two days left , ikimaanisha hiyo kazi ya kuhamisha mafaili yako itachukua siku mbili, baada ya dakika kama tatu, utaona inakambia bado siku moja, baada tena ya dakika chache inakuambia bado msaa sita, tena baada ya muda mfupi inakwambia bado nakika kadhaa, badaye sekunde na ile kazi inakwisha ndani  ya robo saa tuamaa na kuongeza juhudi hifanya iishe mapema na kwa ufanisi. Hivyo kama mtu sio mvumilivu na anasafari baada ya lisaa limoja, akiona ile 2 days left, basi anaahirisha na kuona itamchelewesha. .Kwa tafsiri rahisi ni wamba kazi yoyote mwanzo huonekana kubwa na nzito sana , na ndiyo ilivyo, lakini kutokata  Zipo sababu nyingi sana. Pamoja na changamoto ya uwezo binafsi wa mwanafunzi kitaaluma, ulevi, msongo wa mawazo na majukumu yanaayozidi uwezo, naomba nizitaje sababu kongwe mbili ambazo ni UVIVU NA NGONO.


UVIVU: Mithali 19:15 Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.
Sina sababu ya kuanza kudadavua uvivu ni nini. Kwa kifupi ni hali ya mtu kukwea kutimiza wajibu wake kwa makusudi. Mvivu hufurahia matokeo mazuri pasi na kuangalia mchakato ulioleta matokeo hayo. Uvivu upo kwenye vitu vingi sana. Huenda ni katika kusoma, au katika kusali. Mtu mvivu kusali hupima nguvu za Mungu kwa vitu vichache alivyovichagua yeye. Kwa mfano akiwa hahudhurii jumuiya, bali misa anaenda na mambo yake ynamuendea vizuri, basi anaridhika na kujiambia kuwa Mungu katosheka na donoadonoa yake kwenye mikusanyiko ya sala, hivyo wale ammbao wanaenda jumuiya na kufanya kazi kadha wa kadha za kanisa, nabado mambo yao ni magumu, anadhani hawapo sawa kiimani au wanakosea mahala fulani.

Wito wangu kwenu ni kusali misa na sala za jumiya kila siku kwa maana hujuwi lini litazungumzwa lipi ambalo litakufaa wewe wapi hasa baada ya maisha ya shule. Epuka kufanya substitution ya muda wa Mungu  na vitu vingine kama chakula, stress nakadhalika.

Mifano yenye undugu na uvivu hatari:
  • Kama ni muda wa kuanza kipindi cha dini, na wewe ndio upo kwenye foleni ya chakula na roho haikuumi kabisa, ujue kuna changamoto.
  • Kama akikukwaza mtu fulani hasa yule ambaye unadhani ndio muhimu kuliko kitu chochote, basi unafunga vyote including mambo ya Mungu, except chakula tu, ujue kuna changamoto.
  • Kama uko addicted  na kitu fulani mbacho ndio starehe yako eg mpira, movie etc na kama ndio unatazama muda wa kipindi cha dini na kuona bora uendelee kutazama, ujue kuna shida somewhere.
  • Hata kama umetoka kipindi cha mwisho darasani saa 1:20 au hata saa 1:30 jioni na kuna nafsi inakuambia ‘umechelewa sana, dakika 15 hazitoshi kwenda hadi dini, bora tu utembee taratibu, ukale upumzike’ , hiyo faraja siyo ya Kimungu.
  • Au ukisikia wimbo wa Roho Mtakatifu unaimbwa, basi unajiambia ‘nimeshachelewa, hakuna sababu ya kwenda sahizi, nitaenda tu kesho’ hapo ni tatizo, ni uvivu huo.
  • Mtu mvivu anateemea mijiza tu bila imani na mapendo, anawaza habari za kuambiwa ;POKEA MUUJIZA WAKO, WALE KUKU WAKO WATAANZA KUZALIANA KWA FUJO HADI BANDA LISITOSHE, Unajibu Aminaaaaa , wakati kuku wenyewe unawapa chakula mara moja kwa wiki, kila siku wanaumwa new castle . Hapo hata akisema KUKU WAKO WATAANZA KUTAGA MAYAI MATATU KWA SIKU ,’ Na wewe unajibu Aminaaaa. Huo ni uvivu wa kufikilia.
  • Ref, : Baba na mama walikuwa na ugomvi kwenye familia, na wakaenda kwa mtu anajiita nabii na mtumishi wa Mungu. Lengo wapokee muujiza wao wa shetani anayesumbua familia yao. Jamaa akawaambia kuwa Roho wa Bwana anamshuhudia kuwa mama ni mshirikina, kumbe mama hata hana lolote masikini,familia ikaanza kuvurugika hadi walipoenda kwa padre kusuluhisha. Tena baba ni msomi mweye PhD , nikawa najiuliza hii sio academic PhD, labda ni  PH ya soil inayokaribia acidity. Yote haya ni matokeo ya uvivu wa kufikilia na kutaka matokeo ambayo hujayatolea jasho kutafuta.
Tufunguemioyo yetu na kumtukuza Mungu kwa kazi zetu na vipawa alivyotujalia Mungu wetu


NGONO: Ni kujamiana nje ya utaratibu (kabla na nje ya ndoa). Kujamiiana ndani ya ndoa huitwa TENDO LA NDOA. Ni takatifu, halali na linatamkika kirahisi. Pia matokeo yake ni furaha kwa kila mtu, lakini matokeo ya ngono hayapokeleki hata kama mtu ni tajiri na ana kila kitu.
 Katika mazingira ya chuo, mihemko ya kuhusiana kwa pupa ni major consumer wa kuwapoteza utashi watu.  (Watched Hot Friday Movie)

Ninapozungumzia ngono ninalenga michakato yote yennye mlengo huo na mawakala wake. Mifano:
·         Mara ngapi umevaa mavazi ya makwazo na kuwavuta watu kingono. Kwa maana mwingine unaweza kumuamsha hashiki mtu na akaona wwewe hauingiliki, hivyo anagain momentum ya kwenda kumshawishi mwingine aweze kutimiza uovu wake huo.
·         Mara ngapi umekuwa kinara wa kuahidi tu watu kwamba utaolewa/kuwoa? O level, A level, JKT, wiki la registration, unayesali naye, classmate, mnayesoma naye elective course, halafu unaota eti hawana effect, subiri tu utaelewa siku moja.

·         Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza kabla hata test one hujafanya, hiyo UE ndio hata hujui inafananaje, but tayari umesema kuna mtu yupo hoi hajiwezi juu yako. Hapo inatoa picha ya moja kwa moja what is your primary goal. Sijasema kwamba mahusiano mabaya, hapaa, lakini yanahitaji kujipanga, utulivu wa nafsi na mwili yaliyopita kwenye MVUTO, MAWASILIANO na baadaye MAHUSIANO.

·         Mara ngapi umejithaminisha sura yako na kujiona wewe ni bora sana hivyo hakuna atakayekupa shida kwenye mahusiano kutokana na uzuri wako hasa kwa wasichana  (kioo hakidanganyi). Lakini ukweli ni kwamba wewe huwajui wanaume, bali unawajua wavulana tu. The sme kwa wavulana, mostly tunawajua wasichana ambao bado wako kwenye makuzi, na tunajidanganya kuwa ni wanawake.

·         Msichana, once you put your skirt off, everything is off. Ni rahisi sana, mtu akikuona na utulivu ukampotea , akija anaongea hadi anatetemeka , msichana na wewe ndio unaona unamkomeshaaaaa kwa uzuri wako kumbe mwenzako pale akili zake za kawaida hazipo, in such akianza kukusogolea towards your direction, huruma inakuingia, akisema mguu pande, unajibu mguu sawa. Baada ya kukufahamu, Yeye mweyewe tena anakuambia, nyuma geuka, mbele tembea, Kiruuuuuu, unaanza kulalamika mbona harudi, kwani aliona nini that day? Jibu ni kwamba hakuona kitu, coz angekiona kitu angekirudia tena kwa mara nyingine..

JE TUSIINGIE KATIKA MAHUSIANO?
Tuingie tu, lakini uwe kweli ni muda sahihi, mmejiandaa vya kutosha na uhakika wa kupropagate, hii inahusisha mtazamo wa kiimani na kirasilimali. Kumbuka hii ni tofauti na urafiki, kwa maana urafiki hautafutwi na hauna limitation, bali mahusiano hutafutwa na yana limitation. Lakini pia jifunze kuweka mahusiano bila ngono. Tawala mwili wako, vaa mavazi ya staha, jikubali kuwa wewe ni binadamu uliye kamili.

Katika mazingira fulani roomates wana attribute watu tuingie kwenye mahusiano kutokana na huduma ambazo wanazipata kwa hao wanaowaita wapenzi wao, wakati sio wapenzi bali ni wafanya ngono wenzao, eg wakiugua etc. Au simu zao wakiongea na kubembelezana usiku, masikinini wewe tumbo linakuunguruma na kuona kama Mungu kakusahau. Hivi umekosa vipimo vya kupma kazi za Mungu?

KAMA ANALAZIMISHA NGONO, NITAKATAAJE WAKATI NAMPENDA?
Sio kweli, huo ni unafiki. Upendo hauunganishwi na ngono, kuna kitu kimukuscorpion na unajifanya huoni huo uchfu na shimo ambalo mnajichimbia wote wawili hasa msichana.
Tukiambie kizazi chote ukweli kwamba ngono ni adui anayetutenga na MUNGU.
  • ·    Kwanza mwambie wewe sio chombo cha starehe, hivyo mkataba wa ngono unauvunja rasmi.
  • ·    Akiendelea kulazimisha mwambie haupo tayari kuendelea na hayo mahusiano.
  • ·    Punguza mawasiliano na badaye acha kabisa.
  • ·   Utaumia kidogo kwa kipindi cha mwanzo na baada ya muda fulani utagain momentum ya amani. Bora maumivu kidogo ya sasa kuliko maumivu ya kudumu badaye.
  • ·   Usikubali tena kukutana naye sehemu za faragha , anaweza  kukudhuru kwa namna yoyote endapo utakataa kutimiza matakwa yake. Mkikutana msalimie kama kaka/dada.
  • ·    Acha kukurupukia mahusiano mapya mapema, tuliza kichwa fanya mambo ya msingi sana hasa sala na shule. 


VIPI JUU YA UHAKIKA WA MTARAJIWA WANGU KUWA ANAJITUNZA HUKO ALIKO?
Haikuhusu. Wewe heshimu mwili wako, wekeza kwenye sala, Mungu atakulindia huyo ambaye humjuwi, kwa maana kujiliinda kwako ni sala pia. Once ukimpata mkakati wa kwanza wa kuuweka ni kuweka mkataba kuwa NGONO NI ADUI WA MAHUSIANO . Na utamjua siku ya ndoa,  na ukisema basi wewe unaanza taratibu majaribio ya mwili wako kisa una uhakika utamkuta used, basi wewe hautofautiani na wapiga lamli ambao wapo very detailed kuongea mambo ambayo hawawezi kuprove. Hii ni kwasabau hata mchumba wako aliyekutolea posa na mahari anaweza kufa siku moja kabla ya ndoa, na asikuoe, wala hawawezi kusema marehemu kaacha mjane mmoja ambaye alitakiwa kumuoa kesho.

Kwa hayo machache niwatakie kila la heri katika masomo yenu, na Mungu awasaidie sana, nasi tunawaombea san ili mpate wepesi katika masomo yenu. KARIBUNI KWENYE MAHAFALI KESHOKUTWA 25/11. Tumsifu Yesu Kristo. ( 23/11/2016- TMCS SUA NEW HOSTELS)

Eng Herman Nguki wa Malekela (Bsc Irrigation & Water Resources Engineering  2012-16- SUA)

Tembelea www.ngukiherman.blogspot.com mara kwa mara kujisomea mada mbali mbali za vijana, mahusiano na kanisa. Karibu ujifunze.
Thank you for visiting my blog. Click home/ view the web version to see other topics on list ( in case you don't), which have been categorized by months posted. Eg to see the topics posted on October , just click October. You are welcome. Also for Professional information about Agriculture, water resources, soil and environmental conservation visit www.wadcotanzania.blogspot.com  Eng Nguki  

No comments:

Post a Comment