I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Monday 31 October 2016

USHUHUDA-Mt Rita wa Kashia kwa Nguki**

Mt Rita wa Kashia, mwombezi wetu mwenye nguvu kwa mambo yaliyoshindikana

Tumsifu Yesu Kristu, leo hii natamani nikushirikishe kitu juu ya nguvu ya Novena. Bila shaka kwa Mkristo Mkatoliki neno hili novena sio geni, wala sihitaji kulidadavua kirefu. Kwa kifupi NOVENA NI SALA YENYE NGUVU ISIYOSHINDWA KAMWE KUTOA MAJIBU IWAPO UTASALI KWA IMANI. Zipo novena nyingi kama za Roho Mtakatifu, Pentekoste, za watakatifu kama Rita wa Kashia nakadharika. Kwa wanafunzi wa chuo novena ya Roho Mtakatifu najua lazima huwa inakumbukwa kipindi cha kukaribia mitihani. Ipo pia novena ya kushukuru baada ya kufungua chuo kwa kumshukuru Mungu kwa kurudi salama na matokeo ya kukuwezesha kuvuka mwaka, japo hii wengi huwa wanaipuuzia kwa kuwa hakuna wanachokiomba, walishapata tayari vyote.

 Lakini kwa waliopo au waliotoka jumuiya ya TMCS SUA-New Hostels, tangu mwaka 2014 tulianza kusali Novena kwa Mt Rita wa Kashia ambayo huchukua siku 12, yaani kuanzia Jumatatu ya kwanza ya UE hadi Ijumaa ya mwisho ya UE kwenye vipindi  vya sala za asubuhi. Yaani siku 9 za novena na 3 za shukurani, zote zipo ndani ya muongozo wa vitabu vya Mt Rita wa Kashia. Mara zote huanza  na sakrament ya Kitubio.  Novena ile kwa wenzangu ambao tumekuwa tukishiriki wote ni mashahidi, kila mtu kwa nafsi yake, Mungu amekuwa akijibu kwa upekee sana yale maombi takribani 15 kwenye muongozo wetu. Hakika Mungu atukuzwe.


AMENIJIBU TENA KWA MAOMBEZI YA MT RITA WA KASHIA
 Kama binadamu mwenye malengo na mahitaji, niliazimia tena kujichotea baraka zilizopo bure kwa Mungu wetu kupitia maombezi ya mtakatifu huyu shujaa wa kujitoa sadaka ambapo tarehe 9/9/2016 nilianza novena  kwa Mt Rita wa Kashia nikiwa na mahitaji 10 ambayo niliyaorodhesha kwenye karatasi yangu. Katika orodha yangu kulikuwa na shukurani na maombi. Yale maombi yalikuwepo yale ambayo majibu yake ni tangible (yani yakijibiwa nitajua moja kwa moja) na yalikuwepo ambayo ni intangible (siwezi kuthibitisha kwa macho kuwa kayajibu lakini kwa imani). Novena ile ilianza tar 9/9 Ijumaa na kwenda hadi 20/9/2016 na kukamilisha siku 12. Nilianza nikiwa Iringa nyumbani lakini tar 18/9/2016 Jumapili nilisafiri kwenda Mbeya kwaajili ya semina kwa wiki moja, hivyo niliimalizia nikiwa Mbeya.
Mungu anashughulika na mambo yetu usiku na mchana,  wema wake watuzunguka pande zote


MAAJABU.
  1. Baada ya kuanza novena tarehe 9/9/2016, kesho yake tarehe 10/9/2016 ombi la kwanza kuorodheshwa likatimilika vilevile nilivyoomba.
  2. Siku ya 7 ya novena yaani 15/9/2016 ,Ombi la pili kuorodheshwa kwenye karatasi yangu likatimia vilevile nilivyoomba na kuandika.
  3. Siku ya 10 ya novena tar 18/09/2016 Ombi la tatu kwenye orodha yangu lilitimia kwa mfumo uleule. Nilistaajabu mno, maana ombi hili niliwaambia hata baadhi ya marafiki zangu kuwa nimelifungia novena na lazima niibuke kidedea, likatimia vilevile.
  4. Baada ya novena kuisha, Mungu aliendelea kujibu orodha yangu ambapo yale tangible lilibaki moja ambalo ni la muda mrefu (long term goal) ambalo naamini Mungu ameshajibu lakini anasubiri tu siku nzuri ya kuniambia ili nipokee. Na yale ambayo siwezi kuona majibu kwa macho naamini Mungu ameshajibu yote kwa maombezi ya mama huyu Rita wa Kashia ambaye Kanisa katoliki kwa kusaidiana na shirika la Mtaktifu Agustino tunamuita MTAKATIFU WA MAMBO YALIYOSHINDIKANA NA MFANYA MIUJIZA MTEULE WA MUNGU.
  5. Watu wengi pia wameendelea kushuhudia mambo makubwa na yaajabu ambayo Mungu amejibu kupitia maombezi ya Mt Rita wa Kashia.
Hakika nakosa cha kusimulia zaidi, lakini jinsi Mungu alivyojibu tena kwa mtiririko uleule kama nilioandika kwenye karatasi yangu ya maombi, kweli niliamini Mungu yupo na anajibu waziwazi na tunajionea kwa macho.

LINI TUNASALI NOVENA KWA MT RITA WA KASHIA?

  1. Kuanzia kila Jumatatu ya kwanza ya mwezi. Siku ya 12  (ya mwisho) inadondokea Ijumaa ya wiki la pili la sala.
  2. MAALUMU KWA MWEZI WA MAY. Mt Rita wa Kashia alizaliwa Jumamosi ya 22/5/1377 na kufariki Jumamosi ya 22/5/1457. Hivyo kwa upekee wa mwezi huu wa tano NOVENA HUANZA SIKU 9 KABLA YA 22/5 AMBAYO NDIO SIKU YA KUMBUKUMBU YAKE (feast day), yaani tunaanza novena tarehe 14/5 ili siku ya 9 idondokee siku hiyo ya 22/5. Ukiongeza na siku tatu za shukurani (kwa mujibu wa muongozo) novena itakamilika tarehe 25/5. Tarehe hii 22/5 ni siku kubwa sana kukumbuka matendo makuu ya Mungu kupitia mteule wake huyu mkuu, ambapo kuanzia Kashia na dunia nzima misa mbalimbali hufanyika kwa heshima ya Mt Riata wa Kashia
  3. Waweza kusali wakati wowote unapokuwa na nia yoyote iwe shukurani, maombi ya kawaida, mfadhaiko mkubwa au changamoto nakadhalika. Usisahau pia kusali sala mbalimbali kupitia yeye. Jambo la msingi hakikisha unapata kitabu cha sala na novena.
Nisikilize ndugu yangu hapa chini

USHAURI WA BURE
Mungu wetu ni tajiri, na vyote tunavyovitamani kwa haki ni vyakwake  na sisi ni warithi wake (Rum 8:17, Gal 3:29, Tito 3:7) kwa maana hiyo tukiomba kwa imani anatustahilisha kuvimiliki si kwa sifa za duniani. bali kupokea kwa saburi, unyenyekevu na kuhudumia wengine. Wakati fulani Mungu anaweza asijibu maombi kwa wkati, lakini pengine anakuwa ameshafanya typing , anayo softcopy, hivyo yuko mbioni kuprint ili ukabidhiwe kwa maana anafahamu softcopy huna facility ya kuhifadhi. Sasa ukianza kulalamika na kuona kama Mungu hayupo utamtibua na kumfanya aahirishe kumtuma Malaika Gabiel kwenda  stationary kuprint ujue. Tulia, kuwa mnyenyekevu, kuwa na subira, mchukie shetani na matendo yake, jitahidi kupenda kuhudumia kuliko kuhudumiwa. Pale unapopata ugumu, washirikishe watu unaowaamini wakusaidie, sio kila mtu wa kumshirikisha kila kitu. Kwa Kristo sisi ni washindi, kwa Kristo tuko salama. TUMSIFU YESU KRISTO:


Eng Nguki wa Malelela

Sunday 30 October 2016

Are you getting difficult to leave a comment? Learn

It is my happiness when youths set goals and live Godly life

I have been receiving complains from my blog viewers that they fail to leave a comment after reading my topics. First it is obvious that google can't  allow comments from unknown people to avoid bad languages. Meaning that  you must have gmail account to be able to leave a comment down the post.

Now, if you  have a gmail count,, first write the comment at the given window, then  just at the drop down 'select account'  choose google account , it will direct you to login window, where you will insert your email and password, after login it will by default bring you back to the post where you will click 'publish', then the comment will be published with your name as a sender. After that you will simply logout from your account.

If you don't have a gmail account, (common challenge) please create it, through www.gmail.com .It is very simple and free, just few minutes, even if you have yahoo account, you can have gmail account then use yahoo account as confirmation email. After that go to the blog www.ngukiherman.blogsport.com ,after reading the post, follow the instructions above as someone with account. I hope you have understood. Thank you for visiting my blog, learn and enjoy

Eng Heman Nguki wa Malekela
ngukiherman@ymail.com
+255 763 639 101
I use this opportunity to welcome you to visit the WaDCo Tanzania official blog where you will get professional information about soil, water, agriculture and  environmental conservation. It is  www.wadcotanznia.blogspot.com    we will let you know once we will have bought a domain.. Eng Nguki
'click home'/'view the web version' to see homepage and topic list (incase you don't)

Thursday 27 October 2016

USIJINUNISHE, UTAKOSA MENGI.


Kutabasamu na kufurahi ni dawa kwako na kwa wanaokuzunguka. Smile, laugh ,,,, mama.

Kuna wakaati mada hii huwa napenda kuipa jina WEATHER STATION. Bila shaka unafahamu maana ya weather station au kituo cha hali ya hewa kwa Kiswahili. Kazi yake ni kukusanya takwimu zilizopo za hali ya hewa ili kubshiri matukio ya kihali ya hewa yatakayotokea huko mbeleni. Lakini hawa jamaa wanaofnya kazi kwenye hivi vituo au mamlaka wana rah asana, kwa maana ikitokea walichobashiri hakijatokea, maelezo yao ni marahisi tu, utasikia, ‘kulitokea mgandamizo wa hewa wapi huko ukasababisha upepo ubadili muelekeo badala ya kuvuma kwa 25km/hr kwenda Multpurpose hall, ukavuma kwa 200 km/hr kwenda freedom square Mazimbu. Na tena ikitokea walichobashiri mmepuuzia na kikatokea, pia neno lao fupi tu, ‘tuliwaambia mkabisha’ . Kwa kifupi muda wote wapo sahihi.

Tabia ya binadamu kuna wakati inafanana na weather parameters kama temperature, humidity na ndugu zao, japo kamwe haiwezi kujengewa weather station ili ku predict trend ya ubadilikaji na kuchora graph zake. Kwa maana hiyo, kamwe huwezi kubashiri kwamba kwa maneno haya, huyu atayaishi anayozungumza au la! Siku mgandamizo ukizidi kaskazini atatoa majibu rahisi ya badiliko lake, wakati wewe ulishamchorea graph tena kwa peni, hata kifutio hakina kazi. Kuna wakati watoto wanabadilika hata kwa wazazi wao walio wazaa, fikiria graph iliyochorwa na mzazi hasa mama aliyekulea kuanzia tumboni miezi 9 na wengine miezi 12 sijuwi, sembuse kwa wewe mliyekutana tu hapa au pale? Mh, sasa kumbe ni bora kujijengea indoor self-weather station ya kujichunguza wewe binafsi na kujichorea migraph yako mwenyewe ili hata ukipredict upepo, lakini ikaja mvua ya kokoto, au ulipredict manyunyu ya mvua, lakini likaja tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 20 kipimo cha lichter ikuhusu mwenyewe. Kuna siri kubwa moja tu, ya kuhakikishaa muda mwingi unakuwa una furaha na graph zako zinakaa vizuri.

  •  Mithali 15:13 Moyo wa furaha huchangamsha uso; Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
  • Joel 1:12 Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu.
  • 2Corinthians 7:4 Ninao ujasiri mwingi kwenu; naona fahari kuu juu yenu. Nimejaa faraja, katika dhiki yetu yote nimejaa furaha ya kupita kiasi.


SIRI NI KUWA MCHESHI (SENSE OF HUMOUR) KWA KILA AWAYE MBELE YAKO HUKU UKISALI NA KUMTEGEMEA MUNGU KWA KILA KITU.

Kwanini uwe mcheshi?

1. It Attracts People To You. Watu wanapenda kukutana na nyuso zenye furaha, kufurahi ni dawa hasa pale ambapo mmoja anakuwa na msongo wa mawazo kwa namna moja au nyingine. Kucheka ni tiba kwa mtu aliyekosa tumaini na hatia ya kukataaliwa. 

2. It Attracts The Right Kinds Of People. Mtu mcheshi Mungu humkutanisha na watu sahihi. Ukijifanya fundi wa kujinunisha na shetani atawanunilize watakaokujia ili chuma inoe chuma. Kujifanya wewe ni watofautisana kuliko wenzako sio tabia nzuri. 

3. Cope With Stress. Mtu mcheshi yuko frexible, hata anapopata magumu ucheshi wake humsitiri. “A person without a sense of humor is like a wagon without springs. “A person without a sense of humor is like a wagon without springs. It's jolted by every pebble on the road. “ Henry Ward Beecher.

 4. Health Benefits. Laughing has been shown to improve your immune system by helping your body produce more infection fighting materials and lower the amount of stress hormones in your body.
Furaha ikitoka moyoni, uso hauna uwezo wa kuficha ujue, teh,teh. With my young sister ,,,Damiana

 5. Humor Improves Your Mood. Mtu mcheshi mood yake iko vizuri katika utendaji kazi, tena hakwziki mara kwa mara na akikwazika anasamehe mara moja, pia akimkwaza mtu yupo huru kuomba msamaha.

6. It's Good For Your Brain.Utafiti unaonesha utani mpya na kucheka huamsha sehemu ya ubongo ambayo ni muhimu kwa kujifunzia na kutafakari.( University of London of Neurology). “Humor is by far the most significant activity of the human brain.”• Edward de Bono.• Edward de Bono. Huo ni ukweli wa mchana. Kama huamini fuatilia mtu aliye na stress na hasira, halafu apewe kazi ya group kutype, msiruhusu akaiprint, pitieni kwanza pamoja nayeye akitlia. Mtajionea vituko, kwenye O ataweka sifuri, problem kaandika bloplem etc,,,, 

7. It Strengthens Friendships. People feel closer to others who they are able to have a good laugh with. By joking around with friends and family you are not only enjoy a good time with someone you care about, you are also building a bond and a memory that you guys will be able to come back to later on. We jinunishe tu, watu watakuwa hawaji kwako mara kwa mara kukushauri au kushare na wewe chochote.

 8. Diffuse Anger. Mtu mcheshi hufanya watu wasiwe na hasira juu yake hata akifanya kosa (kwa bahati mbaya), ni rahisi kusamehewa. Ni afya kujishusha hasira zako, na kushusha za wengine pia.   " You can't stay mad at someone who makes you laugh- it's as simple ast that."- Jay Leno.

 9. Lowers Other People's Resistance. Kama binadamu, tuna ugumu/ resistance kwa mambo fulani fulani. Kwa mfano kuintroduce jambo fulani muhimu kwa mara ya kwanza kwa mtu fulani. Mtu mcheshi anafanya iwe rahisi watu kumshirikisha au kumwambia mambo mengi. Eg kupropose urafiki/uchumba etc. By using humor and being funny you can break through these lines of resistance, or at least lower them, so that you can meet new people, ask important questions, or whatever you want to get done. Humor is a rubber sword - it allows you to make a point without drawing blood. ~Mary Hirsch.

 10. Help Those Around You. Kuwa mcheshi kunafanya uwasaidie wanaokuzunguka na kutatua matatizo yao. Knowing that you are making someone else's day and you are helping them relax and enjoy life for a minute can be rewarding all by itself. The friendships you can build are just a nice added bonus to that. Kufurahi na kuwa mcheshi ni dawa ya kuboresha maisha yako, tena kutakufanya uishi kwa amani hata kama kuna ugumu fulani unapitia. Furahi,furahi,furahi. 
Ukiwa mtu wa tabasamu na furaha muda mwingi, utakuwa na marafiki wa kweli.

Nakutakia ujenzi mwema wa INDOOR SELF WEATHER STATION’ na Mungu atakusimamia.

TUMSIFU YESU KRISTO.

Eng Herman Nguki 0763 639 101/0679 639 101/ ngukiherman@ymail.com
www.ngukiherman.blogspot.com
click  home/view the web version down the page to see other topics list (incase you don't)


Tuesday 25 October 2016

10 WAYS TO WIN THE BATTLE FOR PURITY

10 WAYS TO WIN THE BATTLE FOR PURITY
It is possible, begin practicing today
Someone can amaze, Nguki why ‘BATTLE?’ Yes, it’s a battle, just relax, you will understand the concept after thorough scanning on the arms. First Read the whole chapter at 2Thim 4:1-22. Flashy billboards, provocative dress and apparel, Hollywood fashions (Yet adopted by Bongo movies and music artists) spread far and wide, suggestive innuendos, off-colored jokes, indecent movies, and the ever-present danger of the Internet to visit the numerous and poisonous websitesall of these and a plethora of other alluring and seductive temptations can trap even the best of us into falling into the sin against the virtue of purity. In a certain sense, the world can be depicted as a moral land-mine, where at every turn and corner in the road there is an immoral spiritual bomb that can be stepped on and explode!  Let us be honest and to the point—we live in a society of dangerous and often pernicious images. We live in a pornographic society!
Almost 100 years ago Our Lady appeared in Fatima to three innocent Shepherd children—Blessed Jacinta, Blessed Francisco and their cousin Lucia de los Santos. Our Lady appeared to the children six times—from May 13th up to October 13th on which the great miracle of the sun occurred witnessed by close to 80,000 people.
One of the subsequent messages of Our Lady to the world at large referred to the salvation as well as perdition of humanity. Our Lady stated in the year 1917 that most souls were lost to the fires of hell principally due to the sins against the 6th and 9th commandments—that is to say the sins of impurity.
This being the present danger we would like to offer a spiritual strategy that we can use; a plan applicable for parents, teens, and even children so that we can avoid the ever-present danger of the attacks against purity, and if we have fallen, to gently and confidently return to the Lord, through the intercession of Mary, with all our hearts.
Say NO to pre marital sex.. Invest in prayers.
 Spiritual Arms to Win the Battle for Purity
1. Weapons of Prayer (SILAHA YA SALA). We are weak, very weak! Jesus reminded the Apostles as well as the whole world in the Garden of Gethsemane with these precise words: “The spirit is willing but the flesh is weak. Pray that you will not enter in the test.”(Mt 26:40-41)
2. Don’t play with fire(USICHEZE NA MOTO). A key reason why many fall into sins of impurity is a failure to avoid the near occasion of sin. Proverbs are not lacking:  “He who plays with fire will get burnt”… and “He who walks on thin ice will fall in” … once again… “He who walks on a slippery slope will fall.”  We have to use common sense and prudence.
3. Modesty (KIASI). The Catechism of the Catholic Church states that modesty is the guardian of the virtue purity. (CCC # 2521-2524) All must practice modesty. Through Baptism our bodies become temples of the Holy Spirit, still more, temples of the Blessed Trinity and after Holy Communion living Tabernacles of the Blessed Sacrament.
4. Penance (MALIPIZI). Jesus stated:  “Some devils can be expelled only through prayer and fasting.” On one occasion I was taking a walk and in my path was a big black bird—a Crow.  As I drew closer the bird did not take flight. Always having a strong devotion to St. Francis, I thought that maybe I had a latent special gift with animals. This was not the case at all. The reason for the lack of flight was the simple reason that the poor bird had a broken wing! The scene brought me to a spiritual reflection.
5. Avoid Laziness. (ACHA UVIVU) Another huge opening for the devil of impurity is the capital sin of sloth or call it laziness. Once again maxims are at our beck and call: “Idleness (laziness) is the workshop of the devil.”
6. Improper Language (LUGHA CHAFU).  In all times and places and circumstances we should control our tongue. Saint James admonishes us: “We should be slow to speak and quick to listen.” (Read St. James 3—the sins of the tongue) But this is especially pertinent with respect to purity.
7. Constant Vigilance—especially of the eyes.(KUWA MACHO/MUANGALIFU) Pope Francis in his messages is constantly reminding us that we must keep vigilance over our persons. The Ignatian daily examen is key. This superb practice invites us to rewind the film of our day and see where God has been present and give thanks, but also to see where our hearts have wandered from our loving God.
8. Confession & Renewed Hope (KITUBIO & TUMAINI JIPYA). Human weakness does prevail over us and we can all fall. Worst of all, above and beyond the fall into any sin,  is that of despair.  The gravest fault of Judas was not his betrayal of Jesus, but his despair and failing to trust in the infinite mercy of Jesus.
 9. Frequent Holy Communion (KUPOKEA EKARISTI MARA KWA MARA). Of the greatest importance in safeguarding the virtue of chastity is our relation to Jesus in the most Holy Eucharist.  The Holy Eucharist is really, truly and substantially the Body, Blood, Soul and Divinity of Jesus, the Son of the living God.
10. Our Lady: Our model and intercessor for all virtues. (BIKIRA MARIA: MFANO WA KUIGWA NA MWOMBEZI WETU KWA MAADILI/ WEMA WOTE). Of course it would be far from complete our treatise on the virtue of purity if we did not invite Our Lady, the Mother of holy and pure love to be with us, pray for us, and intercede on our behalf. 
I wish you nice meditation.
It begins with me.


Eng Nguki, Herman <0763 639 101>/ngukiherman@ymail.com.

Ref//Catholic exchange.com (Fr. ED Broom, OMV)


 click home or web version to see others topics (in case you don't)

Monday 24 October 2016

RAHA, KARAHA??? TUSIWAUMIZE.

RAHA, KARAHA??? TUSIWAUMIZE.
Kwanini asinenepe kwa mfano? Hapo atajifungua salama mtoto mwenye afya.
Katika mizunguko yangu ya siku zote, huyooooooo hadi hospitali ya  mkoa wa Njombe maarufu kama Kibena. Wakati nimekaa nje ya hospitali kando ya barabara nikamuona mama mmoja (sio mkubwa sana, ni binti kijana) ambaye alikuwa mjamzito. Alikaa chini kabisa kwenye nyasi huku akiwa mpole na akionekna kutafkari na mwenye mawazo mengi sana. Kiufupi ilionekana kuna kitu kinamuumiza kichwani kwake, au anamaumivu ya mwili, si unajua tena hawa ndugu zetu wakiwa katika hali hiyo complications kibao.
Baada ya muda mfupi watu wakatokea hospitalini kuja upande wa barabarani. Ni kijana mmoja na binti mmoja ambaye alikuwa mjamzito pia. Bila shaka walikuwa mtu na mkewe kwa maana niliona Yule mkaka kamshikia mkoba huyu dada, pia kamshika mkono huku wakiwa wanatazamana usoni kwa bashasha na matabasamu ya kukata na shoka. Kha, nikajua ni mimi tu ndio nilikuwa nawangalia wale watu kama sehemu ya tuition, kumbe hata yule dada aliyekaa kinyonge pale chini alikuwa anawakodolea macho vizuri tu. Muonekano wa wawili hawa ulitoa picha ya moja kwa moja kuwa wanaishi maisha ya furaha na walijipanga vya kutosha, tena hawajutii maamuzi yao na matokeo yake. Yule dada pale chini liendelea kuwaangalia kwa uchungu huku machozi yakimlengalenga (sina hakika kama ni Kiswahili sahihi), aliwangalia hadi walipovuka barabara na kuendelea kuwasindikiza kwa macho hadi walipoingia kwenye gari la kuelekea Njombe mjini. Kisha akajiinamia chini huku ameshika shavu lake.
Mimi kama kijana nilijiuliza maswali mengi mepesimepesi na kujijibu mwenyewe. Kwa mfano huyu mama hapa chini tena akiwa kachafuka na vumbi huenda kaolewa lakini mumewe hajuwi majukumu yake kwa matokeo ya kile ambacho alikifanya yeye mwenyewe. Au yamkini akawa hii mimba kapewa na mtu ambaye hajamuoa bado hivyo mhusika kakataa kushughulikia lolote nakadhalika, au pengine jamii nzima inayomzunguka imemtenga kwa mfumo fulani.

Ni jukumu la kila mtu kuhakikisha mama mjamzito anakuwa nafuraha wakati wote, bila kujali amepata mimba yake kihalali au sio. Lakini ole wako wewe ambaye uko salama, lakini hutaki kubadili mwenendo wako.


Ndugu zangu mama mjamzito mwenye msongo wa mawazo  sio tu huathiri mfumo wa kawaida wa maisha yake, lakini pia huathiri afya ya mtoto tumboni nap engine kumzaa motto mwenye afya mbovu ya mwili au akili au vyote kwa pamoja. Mvulana ukikurupuka kwa kuendeshwa na hashiki za mwili kasha kumdandia kwa pupa huyo uliyemshawishi kwa pesa zako, unatengeneza bomu ambalo litakulpukia hapahapa duniani au hata ile siku utakaporudi kwa yule aliyekuleta duniani.

Mfano hebu fikiria mama mjamzito ambaye kaolewa na yuko na mumewe nymbani halafu usiku tumbo limuume kidogo, utasikia:

Mama : We baba kijacho, amka bhana mwanao kanipiga teke tumboni hapa, linauma sana.
Baba   : Oh, pole my love, kwahiyo ngoja nimpigie rafiki yangu aje na tax twende hospitali.
Mama   : Hapana acha tu usiku sahizi, nitajitahidi kuvumilia tutaenda hata asubuhi.
Baba     : Hapana, plz, au tumpigie simu Dakitari aje akucheck hapahapa nyumbani.
Mama   : Mhhh, usiku wote huu, usijisumbue, acha tu mume wangu.
Baba     : Haya mama, basi ngoja tukae wote, silali hadi muanze  kulala wewe na kijacho wangu.
Mama   : Hahaaa, acha bhana, unadhani tumbo lenyewe linauma sana basi, nilitaka tu uamke        nikusikie kidogo baba kijacho waangu.
Baba    : Duh, jamani haya mama. Minahamu na huyo kijacho kama nini, sijui katakuwa kajogoo,au  mama ndio atajipatia mke mwenza,, teh, heh, (anacheka huku akimbusu tumboni mkewe). Akizaliwa nitamwambia ulimsingizia kuwa kakupiga teke kwa ndani kumbe ulitaka kusikia tu sauti ya baba yake. Haya mama, lala basi nikufunike shuka.                                     … …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Umeona haya majadiliano? YANA AFYA, RAHA nakadharika.

Hebu tuwe wakweli. Dada ambaye kapewa mimba na mtu ambaye hajamuoa bado. Hapo nyumbani wamemdongoa hadi basi, wamemsondea dole hadi basi, (hadi huyo motto anajiuliza kwani huko nje kuna vita?) tumbo likiuma usiku anamuamsha nani? HAKUNA KITU ZAIDI YA KUJIONA MKOSAJI NA KUMCHUKIA MTOTO ANGALI YUKO TUMBONI. Kwa bahati mbaya mtu ambaye hayajamkuta, anaona ni kitu cha kufikirika nay eye hakiwezi kumkuta wakati hataki kubadilika. Huo ni mtazamo wa mtu mjinga. 

Soon tutakuwa wawili, teh,teh, karibu sana mgeni, kama nakusikia hivi kwa mbaliii

Maana mwerevu hujifunza kupitia matatizo ya watu wengine, lakini mjinga haamini hadi yamkute yeye, ili werevu wajifunzie kwake kama sample space.
Badilika na uchukue hatua leo, kama ulishakosea basi usirudie tena, na kama Mungu amekuepusha hadi sasa, basi usifanye makosa kwenye kufanya maamuzi. Fanya uchaguzi sahihi, funga ndoa halali, furahia wakati wa ujauzito wako/ wa mkeo kwa raha zenu. Inawezekana…………….Tafakari njema

Upendo uwake usiku na mchana katika familia zetu. Lakini wakati wa ujauzito mwanamke anatakiwa kuoneshwa upendo mara dufu zaidi kuliko kawaida kwa maana anaujumbe wa Mungu tumboni mwake.
Watoto ni malaika. Wapewe haki ya kuishi tangu siku ya kutungwa mimba yao na kuendelea.


Eng Herman Nguki
UCE Tanzania Volunteer
+255 763 639 101/+255 679 639 101 /ngukiherman@ymail.com

ngukiherman.blogspot.com / ucetanzania.org 

click home to see the main page and other topics

Tuesday 18 October 2016

SANT’ EGIDIO- SEMINARI YANGU NDOGO

SANT’ EGIDIO- SEMINARI YANGU NDOGO
Washa mshumaa wa upendo kwa wahitaji


Hellow Herman rafiki yangu mzima? Habari za siku nyingi?. Aisee nilitaka kukwambia kuwa mwenzako wameukata na mguu wangu wa pili, kwahiyo sahizi sina miguu yote, namshukuru Mungu kwa uzima, Bado nipo Ifakara huku, vipi wewe huko, ndugu zetu wa SUA wanasemaje? Nawatakia masomo mema, na Mungu awabariki sana ndugu zetu’  Ni maneno yaliyofanya nisimame na kutetemeka kwa muda baada ya kuipokea simu iliyopigwa na rafiki yangu John,. Yeye ni mlemavu wa ngozi (Albino) pia alikuwa amekatwa mguu mmoja kutokana na ugonjwa wa kansa, pia mguu wa pili ulikuwa unamsumbua hivyo hata kutembea na magongo ilikuwa ni kwa shida. Nilifahamiana naye katika kituo cha kulelea wazee na wasiojiweza cha Fungafunga, manispaa ya Morogoro  na kubadilishana namba za simu, ambapo ulikuwa ni wajibu wetu wanajumuiya wa Sant’ Egidio na TMCS kwenda kuwafariji na kuwahudumia tunapoweza. Hata wenzetu wa CCT, SDA, hata vikundi vya madarasa walienda mara kadhaa kuwafariji na kuwahudumia.
Rafiki yangu huyu baada ya kuondoka Fungafunga alienda kuishi Ifakara ambako hali ya mguu uliosalia ilizidi kuwa mbaya na hatimye kulazimika kukatwa pia. Ajabu ni kwamba wakati ananipigia alisikika akiongea kwa furaha na amani bila wasiwasi wowote. Hakika nilijifunza kitu kupitia hali ile, kwa maana ningetegemea angeongea kwa huzuni na kukata tama kwa maana hali aliyonayo ni tete na yenye kuhitaji msaada zaidi. Lakini alimshukuru Mungu kwa uzima, tena akatumia nafasi hiyo kunijulia hali mimi niliyekuwa mzima wa afya chuoni na kunitakia masomo mema.
Kwa lugha rahisi ‘kila mtu anauwezo wa kumsaidia kila mtu’. Makundi ya wahitaji yako mengi sana, kuanzia hapo ulipo, kwa bahati mbaya huwa tunajikita kuangalia mahitaji ya vitu vya kushikika (tangible things) kumbe wahitaji wengi wanataka faraja yetu, wanahitaji kupewa tumaini kuwa wanapendwa na Mungu na pia uzima wao ni furaha yetu sote. Kuwa na fedha nyingi sio kiashiria cha kuwa na furaha, la hasha, zipo familia tajiri wa kila kitu, lakini wakiingia ndani baba na mama kila mtu analala chumba chake. Sasa unajiuliza nini sababu? Mmoja huwa anakoroma sana na kumkosesha usingizi mwenzake, au mmoja huwa analala ovyo kitanda hakitoshi nakadharikaa, ni kwamba watu hawa wameunganishwa na vitu na sio upendo.
Mimi na wewe hasa vijana, tumshukuru Mungu kwa uzima, halafu tupige hatua, tutoke nje kuona wahitaji, Papa Francis anasemaMuda wa kukaa na kujifungia ndani haupo, uwe kasisi, uwe mtawa uwe mlei, toka nje uone kanisa linavyoteseka, toa msaada . Hata Mtakatifu Mama Teresa alipigilia msumari karama hii kwa kusema ‘Kama huwezi kuwahudumia watu mia moja, basi hudumia mmoja’. Kila mtu ana kitu cha kitofauti cha kuweza kuwasaidia wengine. Huna pesa, sawa, vipi hata kutabasamu tu kwa mgonjwa unashindwa? Hata kushauri tu pale ambapo watoto wanakosea unashindwa? Hata kusali tu kwaajili ya watu wasio na msaada nalo ni tatizo, hata kushika mashavu tu ya watoto wadogo na kuwaombea afya njema nalo ni tatizo? Mimi ni mlei na mwanandoa wa baadye, lakini kuwa katika utume wa Sant’ Egidio imekuwa kama kuwa katika malezi ya seminari ambapo unajengeka kuwa na macho ya kuona mahitaji ya makundi mengi zaidi na kuyabeba na kuwa kama yako. Wpo waliojitesa ili wewe ufike hapo, hebu jibane basi hata kidogo ili kuwapa ahueni ya maisha na wengine. ANZA LEO, INAWEZEKANA
VIVA SANT’ EGIDIO
Eng Nguki wa Malekela- ngukiherman@ymail.com

 
With my sister Mary Timoth during Christmas Lunch 2015- SUA

Tabasamu la wahitaji ni ishara ya upendo wa Mungu.-

during Christmas Lunch 2015- SUA

Tukacheza na kuimba pamoja- Christmas Lunch SUA 2015

Tukala na kuwagawia zawadi-Christmas Lunch 2015-sua

After Sunday Mass, Pamoja na Fr Aloyce na mafrateli wa Fransalian-SUA-2015

After mass, Pamoja na Fr Aloyce & my fellow Altar ministrant Carist Mwacha 2015-sua


Bofya ‘view the web version’ hapo chini ili uende main window na kujipakulia mada motomoto kutoka kwa Nguki na ujifunze mengi. COMMENT AND SHARE. 

Monday 17 October 2016

KAZI YAKO NI KUOGELEA, USIKUBALI KUUZIWA HELMET YA TOPE/UDONGO

KAZI YAKO NI KUOGELEA, USIKUBALI KUUZIWA HELMET YA TOPE/UDONGO
USIPOTEZE MUDA KWA KUWEKEZA KWENYE NGONO, WEKEZA KWENYE MAISHA, MSHUMAA WAKO WA MAISHA USIKUBALI KUUZIMISHA KIRAHISI

Habari yako ndugu, Nguki nakusalimu, najua kichwa chako chamotoooo kwa habari za Scorpion mtoboa macho  na sarakasi za walimu wa field Mbeya day. Inawezekana kabisa mimi na wewe tuna madudu yetu tunayafanya kwa siri na Mungu anatuepusha tu na mchukua video, maana tukinaswa na kufanikiwa kuingia watsup, basi nina uhakika aibu tutakayopata ni yakiwango cha lami, bila shaka itatulaza na viatu kwa fedheha. Hivyo tujifunze kupitia makosa  yawengine kwa maana ndiyo sifa ya mtu mwerevu, lakini kwa mjinga haamini  hadi ya mkute yeye ili wengine wajifunzie kwake.


Naam. Katika pitapita zangu  huku kwetu aridhi ya Mkwawa nikakuta kijana mmoja wa kiume amevaa vizuri na kapendeza sana. Kiufupi nilimfurahia kwa uvaaji wake. Baada ya sekunde kadhaa akatokea binti mmoja na kuanza kumfutafuta kichwani kanakwamba jamaa anavumbi, japo alikuwa msafi. Binti mwingine alikuwa pembeni akamwambia ‘Unazingua wewe, mfute na viatu basi’ Yule dada kweli kwa mikono yake akaanza kumfuta viatu yule kaka ambavyo vilikuwa na vumbi. Sikushangaa kwa maana mambo haya ni kawaida mjini na vijijini na yule dada hakujali watu wanaoshangaa pale. Moyoni mwangu nikajiwazia, ‘ lazima kuna kitu kimemscorpion huyu dada na kujitoa ufahamu’. Kaka mmoja akasikika akisema ‘Duh, huyu mshikaji noma, yani akipata hela , dada zetu wa hapa utulivu huwa unapotea kabisa, anawachezea anapotaka, yani utadhani ataishi milele, ni aibu sana, tana familia yao inauwezo sana kifedha, bora tu angeoa na kutulia, kama ni magonjwa basi atasambaza vya kutosha, kama unavyoona fulani pale (akamtaaja jina) anatamani hadi kumlamba miguu huyu jamaa, kisa hela. Hatari sana’. Ahaa, kumbeeeee, nimeshakipata kilichomtoboa macho ya utashi na kujifanya chizi, ndio ni FEDHA ZA WATU AMBAZO HAZITOLEI JASHO KUZIPATA. Maisha ya kijana ni yakupambana, maisha ya kijana ni ya kuwaza mbali na kujitabiria mazuri na makubwa. Lakini aina ya uwekezaji wetu unakatisha tamaa, tumewekeza kwenye vitu vya aibu, vitu ambavyo hatuwezi kujisifia mbele za kadamnasi kuwa tunafanya. Sijuwi kama unanielewa. Kama kweli unajiwazia mazuri wewe na wenzako, huwezi kutumia fedha zako kuwekeza kwenye ngono, ni ujinga huo, the same kwa msichana mwenye akili hawezi utumia mwili wake kama ulimbo wa kuvuta wafanya ngono. Huo ni utamaduni wa kilevi na nimeufananisha na mtu anayenunuua helmet ya udongo wakati kazi yake ni kuogelea, bila shaka mara atakapogusa maji tu, italowana na kubomoka hivyo kuchafua maji na pia uchafu utamuingia machoni hivyo kutoona mbalihaving limited spectrum’. Tamani kila mtu akutabirie mema kwa maana wewe sio muharibifu wa maisha ya watu. Ishi maisha ya kusaidia wenzako, sio tu kifedha, hata mawazo na kumsihi Mungu awatoe katika mateso wanayopitia ili nao waone kuna umuhimu wa kuishi. USIKUBALI KUUZIWA HELMET YA UDONGO WAKATI KAZI YAKO NI KUOGELEA  . ………………Eng Nguki wa Malekela 

UKIMUA KUBADILIKA USIGEUKE TENA.

UKIMUA KUBADILIKA USIGEUKE TENA.
Washa mshumaa wa kujielewa, usifaanye ngono kabla na nje ya ndoa.

Nimekutana na rafiki yangu kipenzi, kwa uchungu akaniambia hili ambalo limempa ushujaa wa maamuzi. NAMNUKUU

‘ Nguki my friend, mwenzako wakati nipo O lever, sikuwa na mahusiano mazuri sana na Mungu. Nilikuwa navutwa sana na tama za mwili. Nilikuwa na mahusiano na msichana mmoja, japo hatukudumu sana, na baadaye msichana mwingine ambaye huyu yeye alikuwa ananilazimisha yeye, na alinitongoza yeye na nilishindwa kujizuia, tukafanya ngono kama ilivyo yule wa kwanza. Niliendelea kuwatongoza wasichana wengine kama watatu hivi, japo kwa msaada wa Mungu sikufanikiwa kufanya nao ngono. Nasema ni msaada wa Mungu kwakuwa mazingira yalikuwa yananiruhusu kufanya uchafu huo na pesa kiasi cha kumudu uwezeshwaji nilikuwa nayo. 

Niliendelea na tabia ile kwa muda, na baadaye nikajifunza kuwa nafanya ujinga na nitakufa endapo nitaendelea. Siku moja nilikaa na kujiuliza hivi siwezi kujizuia? Hivi kwanini wasichana niliofanya nao ngono sijawajaza mimba? Kwa nini sijaathirika na magonjwa? (baada ya kupima).. Nikajijibu mwenyewe kuwa Mungu alikuwa kazini usiku na mchana kunitafuta nisipotee. Ili kuthibitisha  kuwa haya yanatoka moyoni au la, sikumoja nikaingia kwenye mtego. 

Kuna sehemu tulikutana wawili tu mimi na Yule msichan ambaye hata sikumpenda ila alinitongoza  na kunitengenezea mazingira ya kufanya ngono naye hapo awali. Sasa hii ni awamu nyingine ambapo nimejiapia kubadilika,tena tupo sehemu ya faragha kabisa. Mapigo ya moyo yalinienda mbio na sikutaka kurudi uchafu ule. Hali ilizidi kuwa mbaya pale alipotoa nguo zake zote , moja baada ya nyingine. Joto lilinipanda na kijasho chembamba kilianza kunitiririka kikianzia mgongoni na hatimaye kwenye kwapa na maeneo mengine. Nikajiuliza hivi Mungu wangu nataka kufanya nini hapa? Alinivuta ili nimkaribie. Lakini nilikataa kwa nguvu na kubaki pale nilipokuwa nimekaa. Alinivuta tena mara kadhaa, nikagoma huku nikimuomba Mungu anitoe salama katika midomo ile ya shetani ambayo nimejipeleka mwenyewe. Huku akishindwa kuamini kinachotokea, akijua labda natafuta momentum ya kumuendea, alianza kukasirika, na akaja kukaa miguuni mwangu akiwa vile. Mapigo ya moyo sasa yaliacha kudunda kwa mfumo wa nukta na kuhamia mfumo wa mstari nyoofu. HISIA ZILINIPANDA SANA KWAKUWA MIMI NI MWANAUME NILIYE KAMILI, LAKINI NLIIBANA MIGUU YANGU VYEMA NA KUMWAMBIA MUNGU SITAKI KUKOSEA LEO. Yule dada akaamini kuwa leo sio mimi wa siku zote. Kwa hasira akasimama na kuvaa nguo zake na kuondoka. Nilishusha pumzi ndefu na kukurupuka huku nikimshukuru Mungu. Na kuanzia siku ile nikaamini kuwa KUACHA KABISA NGONO INAWEZEKANA hata kama ulizoea. MIAKA SABA BADAYE nimekutana na mmoja wa wsichana niliyowahi kuwatongoza lakini sikufanya naye ngono, ambaye pia anajua kuwa nimewahi kumtongoza na rafiki yake enzi hizo. Alinikuta nikiwa mtulivu sana, huku nina Rozali yangu shingoni ambayo kipindi hicho nilikuwa sivai. Walikuwa wawili na mwenzake, na watu wengi pia walikuwepo na shughuli zao. Sikustaajabu kukutana naye, but akasema kwa nguvu ‘FULANIIIIII, NAKUONA, ZA MIAKA MINGI? NAONA ROZALI NYINGI KAMA PASTOR VILE, KUMBE WIZI MTUPU’. Maneno yale yalinichoma sana hasa ukizingatia ni mbele za watu. Kwa ujasiri nikasema ASANTE SANA NASHUKURU’ .Yeye alidhani anaonge na yule wa miaka saba iliyopita, lakini kumbe nilibadilika totally na kuwa mtu mwingine kabisa,najiheshimu na kumtegemea Mungu, tena nimefanikiwa katika nyanja mbalimbali  nayeye anahangaika tu, kwa maana hata shule ilimshinda akaishia form four. Lakini sikujutia kwakuwa alijua niliendelea na tabia ile.’ MWISHO WA KUNUKUU.

 Nilimtia moyo na kumwambia UKIAMUA KUBADILIKA, BASI USIGEUKE TENA , nikapongez ujasiri wake wa kunieleza mambo ya ndani kabisa haya,. Ukiacha njia mbaya wapo watu watakao sema unaigza, na wengine kukushawishi urudi ulikokuwa. Kaza mwendo, ngono inachakaza, ngono inapoteza rasilimali  hasa fedha na muda. Ngono inakufanya usione umhimu wa kuifikia ndoa takatifu,ngono inavuruga mahusiano yetu na Mungu, ngono inakufanya uwe wakala kamili wa shetani kuishabikia zinaa,ngono inakufanya uishi kwa wasiwasi muda wote, ngono inakufanya uone kila aliye mbele yako anafanya kama wewe , kumbe masikini uko peke yako mahali hapo. Inawezekana. Kama jana hujafanya, leo pia na kesho hufanyi, basi unauwezo na keshokutwa na wiki, mwezi ,mwaka hadi siku ya ndoa kufurahia tendo la ndoa. Ufanyishe mazoezi ya kujitawala, na Mungu atakupa nguvu zaidi. Tumsifu Yesu Kristu……………………….

 Eng. Nguki wa Malekela.
ngukiherman@ymail.com/0763639101

APPOINTMENT , PATAMU HAPOOOOO


APPOINTMENT
Talking to TMCS SUA-Mazimbu campus

Napata kigugumizi kutoa tafsiri halisi ya hilo neno la kigeni lililochukua kichwa cha mafundisho yangu mafupi, lakini nina uhakika wa zaidi ya 95% kwamba unaelewa lina maana gani kwa upande wako. Kwa upande wangu naweza kusema ni ahadi waliyowekeana watu wawili au zaidi (mara nyingi ni kukutana) ili kupeana au kujadili kitu au jambo muhimu sana. Mara nyingi yule aliyeahidiwa kamoyo huwa kanamkereketa na kutamani kubashiri nini kitazungumzwa, napengine kujiambia ‘bila shaka atanipa bonge la surprise leo’ au ‘ mh, Mungu wangu, sijuwi kuna baya gani nimefanya, atanishushuaje leo?’ .Kama ni binti kapewa hiyo appointment na mvulana asiyempenda, tayari anaandaa makombora ya maneno ya kumrushia maana jamaa huenda anataka kufanya application, au kama huyu mtoa appointment anapendwa basi binti anajiandaa vyema kupokea application na pia anafanya screening ya maswali ya interview kwa huyu jamaa, yasije kuwa mengi yaka m-boa na kubadili mawazo.
Lengo langu sio kujadili aina za  appointment, la hasha! Bali ‘HUWA UNAJIAANDAAJE KUHAKIKISHA UNATEKELEZA APPOINTMENT ULIYOWEKEWA NA MTU UNAYEMPENDA SANA?’ Kuna rafiki yangu alikuwa anapenda sana kulala. Ikifika saa nne usiku, yuko fofofo square kitandani, hakuna alarm wala mtu anaweza kumuamsha hadi saa 12 alfjiri. Siku moja aliambiwa na mtu fulani muhimu kwake. ‘Please saa 6 kamili usiku nitakupigia nikwambie jambo muhimu sana, out of that utajutia na tusilaumiane’. Mh patamu hapo. Jamaa aliwaza sana. Aliweka mikakati ya kutosha, aliweka alarm nyingi mno, tena akaweka maximum volume, na akaweka karibu na kichwa chake. Akawaambia na roommate wote, ikifika saa tano na dk 50 hajaamka, wammwagie hata maji ili mradi tu aamke asikilize ahadi aliyopewa. Kama kawaida saa 4 usiku akauchapa, chapiiiii. Heh, makubwa, saa 5 na nusu mtu kaamka mimacho kodoo, kaenda kuoga  kabisa ili asisizie tena na sauti isije kukwaruza wakati wa mazungumzo, teh,teh, Nguki mie, kama hiyo haitoshi akawaambia wenzake waliokuwa wanasoma, ‘plz sitaki mikelele kuna mtu muhimu nitaongea naye soon’. Eh, sawa alarm zote zilikuwa zinaita akiwa kashaamka tayari. Saa sita ikafika, hakuna simu iliyoingia, mh, kuangalia kwenye simu hana salio, duh, kaomba simu kwa wenzake wakasema hawana salio, akaomba mwenzake amrushie mia tano ili aunge kifurushi, ile kurushiwa kumbe alikuwa na deni, kamiatano kakaishia juu kwa juu huko. Kha, alilia kwa hasira na uchungu, akaangalia saa yake au kachelewa kuamka, aku, alikuwa kawahi tu. Hakupata usingizi hadi asubuhi. Kwenye saa 12, simu ikapigwa na yule mdada, ile jamaa kupokea kwa hasira akaanza kulalama we nyau why uliniweka that night mimi nahangaika usiku mzima haunipigii, chizi kabisa wewe, ehe, ulikuwa unaongea na nani? Binti akajibu kwa upole, ‘Nisamehe, saa nne ile mama alikuwa na tatizo nikampigia salio likaisha, nikategemea kuwa labda utanipigia wewe, uliposhindwa nikasema nitakupigia asubuhi nikwambie, lakini sasa naona umepokea kwa shari as if nilifanya makusudi, basi tena nakata simu na sitakuambia tena! Mh, kilichoendelea nitakuambia next time. 
Umeona huyu jamaa fundi wa kulala alivyothamini appointment na kutumia mbinu zote kuhakikisha inatimia? Ehe vipi kwenye mambo ya kanisa mara ngapi tunapewa wito mbalimbali wa kutekeleza lakini visingizio kibao kuwa tumepitiwa na usingizi, mara tulikuwa busy, mara sio lazima kutekeleza mara kwa mara? Mara ngapi tumejitesa na kukosa usingizi ili kujibidiisha na mambo ya kanisa? Mara ngapi hata kusoma nakala na vitabu vya kanisa tunaona uvivu?. Kwenye appointment za kuleta raha za mwili tunakwenda hata kama kuna mvua ya kokoto, na tukifika huko hata tukiulizwa. ‘vipi umeumia?’ utasikia ‘Wala sijaumia, the way nakujali hata mvua sikuisikia, ilikuwa kama hali ya hewa nzuri ya kunipa nguvu ya kufika hapa kwako wewe nikupendaye!’ mh, sawa, Vipi mara ngapi Yesu wa Ekaristi anaweka appointment na sisi katika tabernacle , lakini tunazima simu na kutoa betri kabisa ili tusisikie alarm ya dhamiri yetu inapotuamsha. 2 Samuel 22:31 ‘Mungu njia yake ni kamilifu; Ahadi ya Bwana imehakikishwa; Yeye ndiye ngao yao Wote wanaomkimbilia.’ Sasa ahadi ya Kristu tunaipiga teke. Sijajua wewe mwenzangu unachukuliaje huku kuhakikishiwa kwa ahadi ya Bwana, maana mikono yake i wazi kutuambia jambo mhimu kwa manufaa yetu, sisi tunaotegemea wingi wa huruma zake. Vijana wa Kikristu tumke, tuweke maximum volume kwenye dhamiri zetu, ili tusikawie kukutana na Kristu.
Tumsifu Yesu Kristo,
NGUKI Herman. Bsc Irrigation & Water Resources Engineering , SUA,2012-16
0763 639 101/0679 639 101/ngukiherman@ymail.com

Talking to TMCS SUA-New Hostels students.

Talking to TMCS SUA-Main campus students.

Talking to TMCS SUA-Main campus students.

Talking to CCT-SUA New Hostels students

Talking to CCT-SUA Main campus students




USIONE AIBU, WEWE NI SHUJAA WA UHAI, MTETEZI WA MAISHA.

USIONE AIBU, WEWE NI SHUJAA WA UHAI, MTETEZI WA MAISHA.

Usidhaani kafumba macho, anakuona sana. Sema anawaza lini atakuwa kama wewe

Soma taratibu………………….
Duh, aisee, kweli usijihesabie kuwa una duka eti kwasababu upo kwenye gari kwenda kununua vitu. Mama J anasimulia :

Kaka Nguki we acha tu ndugu yangu, yani hii dunia usikutane na mtu anacheka barabarani huko, ukadhani mambo yake ni mazuri tangu kuzaliwa kwake. Mwaka juzi nilibahatika kupata mchumba ambaye alikuwa ananipenda sana, na nilimshukuru zaidi Mungu kwa maana tulipoweka mezani suala la kutofanya ngono hadi tufunge ndoa, wote tulilipokea vizuri, alikuwa ananihudumia kwa mambo madogo madogo huku tukizidi kufahamiana tabia na vitu kama hivyo. Mwaka jana mwezi wa nane baba yangu alikuwa anaumwa sana kijijini huko wilaya ya Ifunda. Si unajua mimi naishi hapa Iringa mjini na nimepanga chumba mimi na rafiki yangu na tunafanya kazi zetu ndogondogo za ujasiliamali. Basi hiyo mwaka jana mwezi wa nane nikaamua kwenda kumuona baba yangu ambaye alikuwa anaumwa sana na anauguzwa na mama yangu mzazi. Kule kwetu gari linaenda moja tu na linatokea Mafinga, ukilikosa hilo basi. Nilifanikiwa kwenda hadi kule, nikawapa pole kwa mgonjwa, pia nikamwambia mama kuhusu huyu mchumba wangu ambaye yupo tayari muda wowote kuanzia sasa kuja kutoa kila kitu huku, na mimi nifunge ndoa mama, heheeeeee, (tulicheka na kugongesha viganja vya mikono yetu mimi na mama). Basi baada ya siku kadhaa, niliaga ili nirudi nyumbani. Bhati nzuri jirani yetu kuna baba mmoja  ana gari na alikuwa na safari ya kwenda Mafinga, na aliposikia nasubiri gari la kwenda huko alishauri nipate lift kwenye gari lake. Nikashukuru na kufurahi maana nauli imepona hapa.
Safari ikaanza, kwenye gari lake tulikuwa na vijana wengine watatu, jumla watano. Basi wakati safari inaendelea kumbe wale vijana walikuwa hawafiki Mafinga, walishuka njiani mmoja baada ya mwingine vijiji vya njiani na nikabaki mimi na Yule baba mwenye gari, safari ikaendelea. Tulipofika katikati ya msitu alianza kunitazama kwa kunitamani na kuniongelesha maneno ya kunitaka. Nilianza kupata hofu na kutetemeka, nikajua anatania, nilimjibu kuwa sitaki na ninamuheshimu kwa kuwa ana mke na watoto. Alijifanya hasikii na kuendelea kunisemesha, nikaomba kushuka kwenye gari, akakataa. BAADA YA MUDA AKASIMAMISHA GARI PEMBEZONI MWA BARABARA, KUANZA KUNISHIKA, NILILIA SANA HUKU NIKIWAZA MADHARA YAKE PAMOJA NA HATIMA YANGU NA MCHUMBA WANGU MTARAJIWA. NILIPIGA KELELE, NA SIKUPATA MSAADA, NA AKAFANIKIWA KUFANYA UCHAFU WAKE PASIPO RIDHAA YANGU. Akaendelea uendesha gari hadi mafinga na kunishusha hapo. Niliahirisha safari ya kwenda Iringa mjini ambapo kesho yake nilipaanda tena gari kurudi kijijini kwa mama kumwambia yaliyonikutaMAMA ALILAANI SANA KITEND HIKI CHA KITATILI. PIA AKASEMA NIFANYE MCHAKATO WA KUPIMA, NA ANAMUOMA SANA MUNGU AWE HAJANIAMBUKIZA MAGONJWA, LAKINI KAMA AKIWA KANIPA MIMBA, NI BORA NIKAITOE ILI NISIMKOSE MCHUMBA WANGU KULE IRINGA MJINI. MAMA ALISISITIZA NISIKUBALI KUBEBA MIMBA AMBAYO NI ZAO LA UBAKAJI NIKIIKUTA, NITOE HARAKA SANABasi nikapanda tena basi kesho yake hadi mafinga na kupanda jingine hadi Iringa mjini. Nilikaa siku chache na kwenda kupimwa, Mungu wangu, NILIKUTWA NINA MIMBA! Kha, jamani masikini mimi,yani mra mmoja tu!! nililia sana. Lakini sikukutwa na ugonjwa mwingine.Ushauri wa mama ukaanza kunijia, lakini nikasema SITAMUUA MTOTO ASIYE NA KOSA, NITAKAA KIMYA NA MAMA NITAMWAMBIA TUMBO LIKIWA KUBWA AMBAPO USHARI WA KUTOA UTAMAANISHA KUNIUA MIMI PIA MCHANA KWEUPE!! Niliwaza kumficha mpenzi wangu Yule, lakini nikaona moyo unaniuma sana, na usafi wa moyo niliomuahidi Mungu nay eye ,haupo tena. Nikajiwazia liwalo na liwe, NINAMWAMBIA UKWELI. Nikamuita nyumbani yule  mchumba wangu mtarajiwa, huku nikivuja chozi lililochanganikana na jasho jingi nilimueleza kila kitu, na kumpa uhuru kama ataendelea na mimi sawa, kama ataniacha sawa. NIPO TAYARI KWA YOTE. Yule mkaka alisikitika sana, japo hakunilalamikia, hakunitukana, wala kunlaumu. Lakini alinipa pole na kuuondoa mguu wake moja kwa moja, na hakurudi tena, iakawa ndio kuachwa kwenyewe. Nilianza kuishi kwa shida, lakini rafiki niliyekuwa naishi  naye alikuwa ananifariji  na kunitia moyo sana na kwamba nipige moyo konde na Mungu mtoa vyote ataleta tumaini badaye  na mateso haya yana siri ndani yake. Nilitafuta namba ya yule mbaba aliyenibaka na kunipa mimba, kila nikimpigia, alikuwa akinitukana na kunikatia simu, nilikuwa naumia sana, lakini sikuwa na jinsi nyingine.
Mimba ilivyokuwa kuwa kubwa nilimtaarifu mama. Alisikitika sana,lakini wazo lake la kuitoa lilikuwa limechelewa. Hakuwa na la kusema. Mwezi wa sita mwaka huu nikajifungua mtoto wa kike kwa msaada wa mama mzazi wa huyu rafiki yangu (Ndio huyu J unayemuona) anamiezi mine sahizi. Namshukuru Mungu kwa huli jaribu kubwa lililotaka kunitoa uhai wangu. Baada ya kusikia nimejifungua motto, Yule aliyenipa mimba mara mojamoja huwa ananipigia simu kuulizia hali, nakasirika sana na ananikumbusha machungu muuaji yule.Namuachia Mungu yote. @@@@@@@@@@@@@@@ Nguki baada ya pumzi ndefuuuuuu, nikamshika J , mwenye miezi mine, katoto kazuri, kerembo, kanavutia, kamebeba siri ya Mungu. Niliongea mengiiiiiiii ya kumpa nguvu, na kwamba Mungu atampa mume bora kabisa ambaye atawapenda yeye na J wake. Kuwa na mtoto huyo hakuna maana yeye ni mdhambi, wala asimchukie mtoto huyo, huyo huenda akawa ni tumaini na msaada mkubwa kwa watu wengi. Kristu ni mzima, wanaume tuache tama za mfumo huu, huu ni uuaji, uwe umeoa au hujaoa, tawala nafsi yako, wekeza kwenye sala. Ukiwa na tabia za aina hii wewe hauna utofauti na mchawi kwa maana kazi yako ni kutengeneza matatizo kwa wangonge.
BADILIKAAAAAAAAAAAAAA Tafakari Njema…..Eng Nguki wa Malekeala

ngukiherman.blogspot.com , Email- ngukiherman@ymail.com/0763 639 101


Bofya view the web version chini ya document ikupeleke main window, ujipakulie mada nyingine motomoto. Comment and SHARE
Washa mshumaa wa mawazo chanya. Kuwa mtetezi wa uhai, acha ukatili