I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Monday 24 October 2016

RAHA, KARAHA??? TUSIWAUMIZE.

RAHA, KARAHA??? TUSIWAUMIZE.
Kwanini asinenepe kwa mfano? Hapo atajifungua salama mtoto mwenye afya.
Katika mizunguko yangu ya siku zote, huyooooooo hadi hospitali ya  mkoa wa Njombe maarufu kama Kibena. Wakati nimekaa nje ya hospitali kando ya barabara nikamuona mama mmoja (sio mkubwa sana, ni binti kijana) ambaye alikuwa mjamzito. Alikaa chini kabisa kwenye nyasi huku akiwa mpole na akionekna kutafkari na mwenye mawazo mengi sana. Kiufupi ilionekana kuna kitu kinamuumiza kichwani kwake, au anamaumivu ya mwili, si unajua tena hawa ndugu zetu wakiwa katika hali hiyo complications kibao.
Baada ya muda mfupi watu wakatokea hospitalini kuja upande wa barabarani. Ni kijana mmoja na binti mmoja ambaye alikuwa mjamzito pia. Bila shaka walikuwa mtu na mkewe kwa maana niliona Yule mkaka kamshikia mkoba huyu dada, pia kamshika mkono huku wakiwa wanatazamana usoni kwa bashasha na matabasamu ya kukata na shoka. Kha, nikajua ni mimi tu ndio nilikuwa nawangalia wale watu kama sehemu ya tuition, kumbe hata yule dada aliyekaa kinyonge pale chini alikuwa anawakodolea macho vizuri tu. Muonekano wa wawili hawa ulitoa picha ya moja kwa moja kuwa wanaishi maisha ya furaha na walijipanga vya kutosha, tena hawajutii maamuzi yao na matokeo yake. Yule dada pale chini liendelea kuwaangalia kwa uchungu huku machozi yakimlengalenga (sina hakika kama ni Kiswahili sahihi), aliwangalia hadi walipovuka barabara na kuendelea kuwasindikiza kwa macho hadi walipoingia kwenye gari la kuelekea Njombe mjini. Kisha akajiinamia chini huku ameshika shavu lake.
Mimi kama kijana nilijiuliza maswali mengi mepesimepesi na kujijibu mwenyewe. Kwa mfano huyu mama hapa chini tena akiwa kachafuka na vumbi huenda kaolewa lakini mumewe hajuwi majukumu yake kwa matokeo ya kile ambacho alikifanya yeye mwenyewe. Au yamkini akawa hii mimba kapewa na mtu ambaye hajamuoa bado hivyo mhusika kakataa kushughulikia lolote nakadhalika, au pengine jamii nzima inayomzunguka imemtenga kwa mfumo fulani.

Ni jukumu la kila mtu kuhakikisha mama mjamzito anakuwa nafuraha wakati wote, bila kujali amepata mimba yake kihalali au sio. Lakini ole wako wewe ambaye uko salama, lakini hutaki kubadili mwenendo wako.


Ndugu zangu mama mjamzito mwenye msongo wa mawazo  sio tu huathiri mfumo wa kawaida wa maisha yake, lakini pia huathiri afya ya mtoto tumboni nap engine kumzaa motto mwenye afya mbovu ya mwili au akili au vyote kwa pamoja. Mvulana ukikurupuka kwa kuendeshwa na hashiki za mwili kasha kumdandia kwa pupa huyo uliyemshawishi kwa pesa zako, unatengeneza bomu ambalo litakulpukia hapahapa duniani au hata ile siku utakaporudi kwa yule aliyekuleta duniani.

Mfano hebu fikiria mama mjamzito ambaye kaolewa na yuko na mumewe nymbani halafu usiku tumbo limuume kidogo, utasikia:

Mama : We baba kijacho, amka bhana mwanao kanipiga teke tumboni hapa, linauma sana.
Baba   : Oh, pole my love, kwahiyo ngoja nimpigie rafiki yangu aje na tax twende hospitali.
Mama   : Hapana acha tu usiku sahizi, nitajitahidi kuvumilia tutaenda hata asubuhi.
Baba     : Hapana, plz, au tumpigie simu Dakitari aje akucheck hapahapa nyumbani.
Mama   : Mhhh, usiku wote huu, usijisumbue, acha tu mume wangu.
Baba     : Haya mama, basi ngoja tukae wote, silali hadi muanze  kulala wewe na kijacho wangu.
Mama   : Hahaaa, acha bhana, unadhani tumbo lenyewe linauma sana basi, nilitaka tu uamke        nikusikie kidogo baba kijacho waangu.
Baba    : Duh, jamani haya mama. Minahamu na huyo kijacho kama nini, sijui katakuwa kajogoo,au  mama ndio atajipatia mke mwenza,, teh, heh, (anacheka huku akimbusu tumboni mkewe). Akizaliwa nitamwambia ulimsingizia kuwa kakupiga teke kwa ndani kumbe ulitaka kusikia tu sauti ya baba yake. Haya mama, lala basi nikufunike shuka.                                     … …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Umeona haya majadiliano? YANA AFYA, RAHA nakadharika.

Hebu tuwe wakweli. Dada ambaye kapewa mimba na mtu ambaye hajamuoa bado. Hapo nyumbani wamemdongoa hadi basi, wamemsondea dole hadi basi, (hadi huyo motto anajiuliza kwani huko nje kuna vita?) tumbo likiuma usiku anamuamsha nani? HAKUNA KITU ZAIDI YA KUJIONA MKOSAJI NA KUMCHUKIA MTOTO ANGALI YUKO TUMBONI. Kwa bahati mbaya mtu ambaye hayajamkuta, anaona ni kitu cha kufikirika nay eye hakiwezi kumkuta wakati hataki kubadilika. Huo ni mtazamo wa mtu mjinga. 

Soon tutakuwa wawili, teh,teh, karibu sana mgeni, kama nakusikia hivi kwa mbaliii

Maana mwerevu hujifunza kupitia matatizo ya watu wengine, lakini mjinga haamini hadi yamkute yeye, ili werevu wajifunzie kwake kama sample space.
Badilika na uchukue hatua leo, kama ulishakosea basi usirudie tena, na kama Mungu amekuepusha hadi sasa, basi usifanye makosa kwenye kufanya maamuzi. Fanya uchaguzi sahihi, funga ndoa halali, furahia wakati wa ujauzito wako/ wa mkeo kwa raha zenu. Inawezekana…………….Tafakari njema

Upendo uwake usiku na mchana katika familia zetu. Lakini wakati wa ujauzito mwanamke anatakiwa kuoneshwa upendo mara dufu zaidi kuliko kawaida kwa maana anaujumbe wa Mungu tumboni mwake.
Watoto ni malaika. Wapewe haki ya kuishi tangu siku ya kutungwa mimba yao na kuendelea.


Eng Herman Nguki
UCE Tanzania Volunteer
+255 763 639 101/+255 679 639 101 /ngukiherman@ymail.com

ngukiherman.blogspot.com / ucetanzania.org 

click home to see the main page and other topics

2 comments:

  1. Wakaka nasi tufikiri kwa makini sio lawama kuwapa wadada tu,kwani mimba walikunywa kwenye maji? basi tubadilike wote .Kaka Nguki elimu unayotupa sijui wanaelewa wangapi,duuuuh! God be with you all the lifetime

    ReplyDelete
  2. Thanks indeed Cletus. Mungu atusaidie sana kaka tupate kuelewa haya.

    ReplyDelete