I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Monday 17 October 2016

UKIMUA KUBADILIKA USIGEUKE TENA.

UKIMUA KUBADILIKA USIGEUKE TENA.
Washa mshumaa wa kujielewa, usifaanye ngono kabla na nje ya ndoa.

Nimekutana na rafiki yangu kipenzi, kwa uchungu akaniambia hili ambalo limempa ushujaa wa maamuzi. NAMNUKUU

‘ Nguki my friend, mwenzako wakati nipo O lever, sikuwa na mahusiano mazuri sana na Mungu. Nilikuwa navutwa sana na tama za mwili. Nilikuwa na mahusiano na msichana mmoja, japo hatukudumu sana, na baadaye msichana mwingine ambaye huyu yeye alikuwa ananilazimisha yeye, na alinitongoza yeye na nilishindwa kujizuia, tukafanya ngono kama ilivyo yule wa kwanza. Niliendelea kuwatongoza wasichana wengine kama watatu hivi, japo kwa msaada wa Mungu sikufanikiwa kufanya nao ngono. Nasema ni msaada wa Mungu kwakuwa mazingira yalikuwa yananiruhusu kufanya uchafu huo na pesa kiasi cha kumudu uwezeshwaji nilikuwa nayo. 

Niliendelea na tabia ile kwa muda, na baadaye nikajifunza kuwa nafanya ujinga na nitakufa endapo nitaendelea. Siku moja nilikaa na kujiuliza hivi siwezi kujizuia? Hivi kwanini wasichana niliofanya nao ngono sijawajaza mimba? Kwa nini sijaathirika na magonjwa? (baada ya kupima).. Nikajijibu mwenyewe kuwa Mungu alikuwa kazini usiku na mchana kunitafuta nisipotee. Ili kuthibitisha  kuwa haya yanatoka moyoni au la, sikumoja nikaingia kwenye mtego. 

Kuna sehemu tulikutana wawili tu mimi na Yule msichan ambaye hata sikumpenda ila alinitongoza  na kunitengenezea mazingira ya kufanya ngono naye hapo awali. Sasa hii ni awamu nyingine ambapo nimejiapia kubadilika,tena tupo sehemu ya faragha kabisa. Mapigo ya moyo yalinienda mbio na sikutaka kurudi uchafu ule. Hali ilizidi kuwa mbaya pale alipotoa nguo zake zote , moja baada ya nyingine. Joto lilinipanda na kijasho chembamba kilianza kunitiririka kikianzia mgongoni na hatimaye kwenye kwapa na maeneo mengine. Nikajiuliza hivi Mungu wangu nataka kufanya nini hapa? Alinivuta ili nimkaribie. Lakini nilikataa kwa nguvu na kubaki pale nilipokuwa nimekaa. Alinivuta tena mara kadhaa, nikagoma huku nikimuomba Mungu anitoe salama katika midomo ile ya shetani ambayo nimejipeleka mwenyewe. Huku akishindwa kuamini kinachotokea, akijua labda natafuta momentum ya kumuendea, alianza kukasirika, na akaja kukaa miguuni mwangu akiwa vile. Mapigo ya moyo sasa yaliacha kudunda kwa mfumo wa nukta na kuhamia mfumo wa mstari nyoofu. HISIA ZILINIPANDA SANA KWAKUWA MIMI NI MWANAUME NILIYE KAMILI, LAKINI NLIIBANA MIGUU YANGU VYEMA NA KUMWAMBIA MUNGU SITAKI KUKOSEA LEO. Yule dada akaamini kuwa leo sio mimi wa siku zote. Kwa hasira akasimama na kuvaa nguo zake na kuondoka. Nilishusha pumzi ndefu na kukurupuka huku nikimshukuru Mungu. Na kuanzia siku ile nikaamini kuwa KUACHA KABISA NGONO INAWEZEKANA hata kama ulizoea. MIAKA SABA BADAYE nimekutana na mmoja wa wsichana niliyowahi kuwatongoza lakini sikufanya naye ngono, ambaye pia anajua kuwa nimewahi kumtongoza na rafiki yake enzi hizo. Alinikuta nikiwa mtulivu sana, huku nina Rozali yangu shingoni ambayo kipindi hicho nilikuwa sivai. Walikuwa wawili na mwenzake, na watu wengi pia walikuwepo na shughuli zao. Sikustaajabu kukutana naye, but akasema kwa nguvu ‘FULANIIIIII, NAKUONA, ZA MIAKA MINGI? NAONA ROZALI NYINGI KAMA PASTOR VILE, KUMBE WIZI MTUPU’. Maneno yale yalinichoma sana hasa ukizingatia ni mbele za watu. Kwa ujasiri nikasema ASANTE SANA NASHUKURU’ .Yeye alidhani anaonge na yule wa miaka saba iliyopita, lakini kumbe nilibadilika totally na kuwa mtu mwingine kabisa,najiheshimu na kumtegemea Mungu, tena nimefanikiwa katika nyanja mbalimbali  nayeye anahangaika tu, kwa maana hata shule ilimshinda akaishia form four. Lakini sikujutia kwakuwa alijua niliendelea na tabia ile.’ MWISHO WA KUNUKUU.

 Nilimtia moyo na kumwambia UKIAMUA KUBADILIKA, BASI USIGEUKE TENA , nikapongez ujasiri wake wa kunieleza mambo ya ndani kabisa haya,. Ukiacha njia mbaya wapo watu watakao sema unaigza, na wengine kukushawishi urudi ulikokuwa. Kaza mwendo, ngono inachakaza, ngono inapoteza rasilimali  hasa fedha na muda. Ngono inakufanya usione umhimu wa kuifikia ndoa takatifu,ngono inavuruga mahusiano yetu na Mungu, ngono inakufanya uwe wakala kamili wa shetani kuishabikia zinaa,ngono inakufanya uishi kwa wasiwasi muda wote, ngono inakufanya uone kila aliye mbele yako anafanya kama wewe , kumbe masikini uko peke yako mahali hapo. Inawezekana. Kama jana hujafanya, leo pia na kesho hufanyi, basi unauwezo na keshokutwa na wiki, mwezi ,mwaka hadi siku ya ndoa kufurahia tendo la ndoa. Ufanyishe mazoezi ya kujitawala, na Mungu atakupa nguvu zaidi. Tumsifu Yesu Kristu……………………….

 Eng. Nguki wa Malekela.
ngukiherman@ymail.com/0763639101

2 comments:

  1. Replies
    1. Nashukuru, tuko pamoja, asante kwa kutembelea blog hii. Na endelea kufurahia mada mbalimbali za kukujenga.

      Delete