I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Tuesday 18 October 2016

SANT’ EGIDIO- SEMINARI YANGU NDOGO

SANT’ EGIDIO- SEMINARI YANGU NDOGO
Washa mshumaa wa upendo kwa wahitaji


Hellow Herman rafiki yangu mzima? Habari za siku nyingi?. Aisee nilitaka kukwambia kuwa mwenzako wameukata na mguu wangu wa pili, kwahiyo sahizi sina miguu yote, namshukuru Mungu kwa uzima, Bado nipo Ifakara huku, vipi wewe huko, ndugu zetu wa SUA wanasemaje? Nawatakia masomo mema, na Mungu awabariki sana ndugu zetu’  Ni maneno yaliyofanya nisimame na kutetemeka kwa muda baada ya kuipokea simu iliyopigwa na rafiki yangu John,. Yeye ni mlemavu wa ngozi (Albino) pia alikuwa amekatwa mguu mmoja kutokana na ugonjwa wa kansa, pia mguu wa pili ulikuwa unamsumbua hivyo hata kutembea na magongo ilikuwa ni kwa shida. Nilifahamiana naye katika kituo cha kulelea wazee na wasiojiweza cha Fungafunga, manispaa ya Morogoro  na kubadilishana namba za simu, ambapo ulikuwa ni wajibu wetu wanajumuiya wa Sant’ Egidio na TMCS kwenda kuwafariji na kuwahudumia tunapoweza. Hata wenzetu wa CCT, SDA, hata vikundi vya madarasa walienda mara kadhaa kuwafariji na kuwahudumia.
Rafiki yangu huyu baada ya kuondoka Fungafunga alienda kuishi Ifakara ambako hali ya mguu uliosalia ilizidi kuwa mbaya na hatimye kulazimika kukatwa pia. Ajabu ni kwamba wakati ananipigia alisikika akiongea kwa furaha na amani bila wasiwasi wowote. Hakika nilijifunza kitu kupitia hali ile, kwa maana ningetegemea angeongea kwa huzuni na kukata tama kwa maana hali aliyonayo ni tete na yenye kuhitaji msaada zaidi. Lakini alimshukuru Mungu kwa uzima, tena akatumia nafasi hiyo kunijulia hali mimi niliyekuwa mzima wa afya chuoni na kunitakia masomo mema.
Kwa lugha rahisi ‘kila mtu anauwezo wa kumsaidia kila mtu’. Makundi ya wahitaji yako mengi sana, kuanzia hapo ulipo, kwa bahati mbaya huwa tunajikita kuangalia mahitaji ya vitu vya kushikika (tangible things) kumbe wahitaji wengi wanataka faraja yetu, wanahitaji kupewa tumaini kuwa wanapendwa na Mungu na pia uzima wao ni furaha yetu sote. Kuwa na fedha nyingi sio kiashiria cha kuwa na furaha, la hasha, zipo familia tajiri wa kila kitu, lakini wakiingia ndani baba na mama kila mtu analala chumba chake. Sasa unajiuliza nini sababu? Mmoja huwa anakoroma sana na kumkosesha usingizi mwenzake, au mmoja huwa analala ovyo kitanda hakitoshi nakadharikaa, ni kwamba watu hawa wameunganishwa na vitu na sio upendo.
Mimi na wewe hasa vijana, tumshukuru Mungu kwa uzima, halafu tupige hatua, tutoke nje kuona wahitaji, Papa Francis anasemaMuda wa kukaa na kujifungia ndani haupo, uwe kasisi, uwe mtawa uwe mlei, toka nje uone kanisa linavyoteseka, toa msaada . Hata Mtakatifu Mama Teresa alipigilia msumari karama hii kwa kusema ‘Kama huwezi kuwahudumia watu mia moja, basi hudumia mmoja’. Kila mtu ana kitu cha kitofauti cha kuweza kuwasaidia wengine. Huna pesa, sawa, vipi hata kutabasamu tu kwa mgonjwa unashindwa? Hata kushauri tu pale ambapo watoto wanakosea unashindwa? Hata kusali tu kwaajili ya watu wasio na msaada nalo ni tatizo, hata kushika mashavu tu ya watoto wadogo na kuwaombea afya njema nalo ni tatizo? Mimi ni mlei na mwanandoa wa baadye, lakini kuwa katika utume wa Sant’ Egidio imekuwa kama kuwa katika malezi ya seminari ambapo unajengeka kuwa na macho ya kuona mahitaji ya makundi mengi zaidi na kuyabeba na kuwa kama yako. Wpo waliojitesa ili wewe ufike hapo, hebu jibane basi hata kidogo ili kuwapa ahueni ya maisha na wengine. ANZA LEO, INAWEZEKANA
VIVA SANT’ EGIDIO
Eng Nguki wa Malekela- ngukiherman@ymail.com

 
With my sister Mary Timoth during Christmas Lunch 2015- SUA

Tabasamu la wahitaji ni ishara ya upendo wa Mungu.-

during Christmas Lunch 2015- SUA

Tukacheza na kuimba pamoja- Christmas Lunch SUA 2015

Tukala na kuwagawia zawadi-Christmas Lunch 2015-sua

After Sunday Mass, Pamoja na Fr Aloyce na mafrateli wa Fransalian-SUA-2015

After mass, Pamoja na Fr Aloyce & my fellow Altar ministrant Carist Mwacha 2015-sua


Bofya ‘view the web version’ hapo chini ili uende main window na kujipakulia mada motomoto kutoka kwa Nguki na ujifunze mengi. COMMENT AND SHARE. 

5 comments:

  1. God bless you brother..
    You inspire me alot..

    ReplyDelete
    Replies
    1. Thank you bro Zeno,we are together, we are one!!

      Delete
  2. Asante kaka kwa ujumbe mzuri mungu azidi kukupa nguvu katika utume wako

    ReplyDelete
  3. Amina, asante pia. Tuko pamoja my mwenyekiti Elius

    ReplyDelete