I am targeted to change youth's mind set towards positivity.

I am targeted to change youth's mind set towards positivity.
I am targeted to change youth's mind set towards positivity

Monday 17 October 2016

KAZI YAKO NI KUOGELEA, USIKUBALI KUUZIWA HELMET YA TOPE/UDONGO

KAZI YAKO NI KUOGELEA, USIKUBALI KUUZIWA HELMET YA TOPE/UDONGO
USIPOTEZE MUDA KWA KUWEKEZA KWENYE NGONO, WEKEZA KWENYE MAISHA, MSHUMAA WAKO WA MAISHA USIKUBALI KUUZIMISHA KIRAHISI

Habari yako ndugu, Nguki nakusalimu, najua kichwa chako chamotoooo kwa habari za Scorpion mtoboa macho  na sarakasi za walimu wa field Mbeya day. Inawezekana kabisa mimi na wewe tuna madudu yetu tunayafanya kwa siri na Mungu anatuepusha tu na mchukua video, maana tukinaswa na kufanikiwa kuingia watsup, basi nina uhakika aibu tutakayopata ni yakiwango cha lami, bila shaka itatulaza na viatu kwa fedheha. Hivyo tujifunze kupitia makosa  yawengine kwa maana ndiyo sifa ya mtu mwerevu, lakini kwa mjinga haamini  hadi ya mkute yeye ili wengine wajifunzie kwake.


Naam. Katika pitapita zangu  huku kwetu aridhi ya Mkwawa nikakuta kijana mmoja wa kiume amevaa vizuri na kapendeza sana. Kiufupi nilimfurahia kwa uvaaji wake. Baada ya sekunde kadhaa akatokea binti mmoja na kuanza kumfutafuta kichwani kanakwamba jamaa anavumbi, japo alikuwa msafi. Binti mwingine alikuwa pembeni akamwambia ‘Unazingua wewe, mfute na viatu basi’ Yule dada kweli kwa mikono yake akaanza kumfuta viatu yule kaka ambavyo vilikuwa na vumbi. Sikushangaa kwa maana mambo haya ni kawaida mjini na vijijini na yule dada hakujali watu wanaoshangaa pale. Moyoni mwangu nikajiwazia, ‘ lazima kuna kitu kimemscorpion huyu dada na kujitoa ufahamu’. Kaka mmoja akasikika akisema ‘Duh, huyu mshikaji noma, yani akipata hela , dada zetu wa hapa utulivu huwa unapotea kabisa, anawachezea anapotaka, yani utadhani ataishi milele, ni aibu sana, tana familia yao inauwezo sana kifedha, bora tu angeoa na kutulia, kama ni magonjwa basi atasambaza vya kutosha, kama unavyoona fulani pale (akamtaaja jina) anatamani hadi kumlamba miguu huyu jamaa, kisa hela. Hatari sana’. Ahaa, kumbeeeee, nimeshakipata kilichomtoboa macho ya utashi na kujifanya chizi, ndio ni FEDHA ZA WATU AMBAZO HAZITOLEI JASHO KUZIPATA. Maisha ya kijana ni yakupambana, maisha ya kijana ni ya kuwaza mbali na kujitabiria mazuri na makubwa. Lakini aina ya uwekezaji wetu unakatisha tamaa, tumewekeza kwenye vitu vya aibu, vitu ambavyo hatuwezi kujisifia mbele za kadamnasi kuwa tunafanya. Sijuwi kama unanielewa. Kama kweli unajiwazia mazuri wewe na wenzako, huwezi kutumia fedha zako kuwekeza kwenye ngono, ni ujinga huo, the same kwa msichana mwenye akili hawezi utumia mwili wake kama ulimbo wa kuvuta wafanya ngono. Huo ni utamaduni wa kilevi na nimeufananisha na mtu anayenunuua helmet ya udongo wakati kazi yake ni kuogelea, bila shaka mara atakapogusa maji tu, italowana na kubomoka hivyo kuchafua maji na pia uchafu utamuingia machoni hivyo kutoona mbalihaving limited spectrum’. Tamani kila mtu akutabirie mema kwa maana wewe sio muharibifu wa maisha ya watu. Ishi maisha ya kusaidia wenzako, sio tu kifedha, hata mawazo na kumsihi Mungu awatoe katika mateso wanayopitia ili nao waone kuna umuhimu wa kuishi. USIKUBALI KUUZIWA HELMET YA UDONGO WAKATI KAZI YAKO NI KUOGELEA  . ………………Eng Nguki wa Malekela 

3 comments:

  1. Wadada jamani mwanaume sio mtaji! Tujifunze kuwa na nidhamu na pia tujiheshimu! Hongera Hermani. Naamini wengi watapona kupitia blog yako

    ReplyDelete
  2. Kweli kaka asante kutuelimisha na kutukumbusha kwa hili vijana tunajisahau sana, Mungu azidi kukutianguvu.

    ReplyDelete